Mimi ni Mwandishi wa gazeti la Mwananchi. Wiki
mbili zilizopita tulikuwa na mjadala mkali sana
kwenye kikao cha uhariri cha kuamua habari kuu
za gazeti. Mjadala ulikuwa juu ya picha iliyotumwa
na mpiga picha wetu kutoka Dodoma. Kuna baadhi
ya wenzetu walitaka picha hiyo iwekwe ukurasa
wa mbele wa gazeti. Kuna wengine hawakutaka
kabisa iwekwe gazetini kwani gazeti lingeonekana
ni nyenzo ya propaganda za siasa za Urais ndani
ya CCM.
Muafaka ukafikiwa kwamba iwekwe nyuma
kwenye ukurasa wa michezo, ingawa nako
kulikuwa na mjadala kwamba Lowasa ni
mwanamichezo tangu lini. Wengine wakahoji
kwamba tukiulizwa kwamba ilikuwaje gazeti letu
likawa kwenye mazoezi ya Lowassa tutasemaje
kwani huwa hakuna taarifa kwa umma kuhusu lini
Lowasa anafanya mazoezi na anapitia njia zipi.
Baada ya mzozo kuisha, baadhi yetu tukaamua
kufanya uchunguzi wa kina kwamba ilikuwaje
mpiga picha wa gazeti akawa sehemu ya mazoezi
ya Lowasa? Je alialikwa? Je alikutana naye kwa
bahati mbaya? Pia wakati tunajadili kuhusu hii
picha, kulikuwa na presha kubwa sana kutoka
Kwa Mzee Lowasa mwenyewe kuja kwa viongozi
wetu wakuu kwamba kwa gharama yoyote ile
(wengine walisema milioni 10) picha hiyo lazima
itoke ukurasa wa mbele. Bahati nzuri mantiki
ikashinda na tukaliokoa gazeti kutoka kwenye aibu
ambayo tungeipata.
Katika uchunguzi wetu ilibainika kwamba Bwana
Abubakari Liongo, mbeba hela za Lowasa kwa
waandishi, aliwatafuta wapiga picha wetu na
kuwaambia kwamba kuna tukio muhimu la dakika
10 kwa Lowassa. Akatuma gari kumpeleka mpiga
picha alipokuwa anatembea Mzee. Akapiga picha
ya kutembea. Washauri wa Mzee wakamuomba
akimbie kidogo, ikapigwa picha ya kukimbia.
Mpiga picha akaambiwa arudishwe lakini
akaamua kubaki kwakuwa ilikuwa ni karibu na
mahali anapoenda. Akashuhudia Mzee akipanda
gari na kuondoka. Ukitazama picha kwa makini
utaona Landcruiser iko kwa nyuma.
Swali ni kwanini hadaa yote hii? Sababu ni
kwamba ni kweli afya ya Mzee Lowassa
imedhoofika. Kila mwezi anaenda kutibiwa
Ujerumani, mikono inatetemeka na jicho moja
linakaribia kufunga kabisa. Sababu ya kutaka
picha hii itoke kwa gharama kubwa ni kujaribu
kuuonyesha umma kwamba yeye ni mzima. Wapi
wazee wengi wanaofanya mazoezi kila siku lakini
hawahangaiki na kupigwa picha. Mzee Mwinyi
ana miaka 89 na anatembea na kukimbia kila siku.
Dr. Salim anakimbia kila siku. Jenerali Mirisho
Sarakikya ana miaka 80 na anapanda Mlima
Kilimanjaro kila mwaka kwa mwaka wa 30 sasa.
Hatuoni wakihaha kupiga picha na kuzisambaza
mitandaoni. Mazoezi magumu kwa Lowasa ni
kushika kikombe cha chai kwa dakika 3.
Binafsi nimepata woga. Nimepata woga kutokana
na uroho mkubwa wa madaraka ulioonyeshwa na
timu ya Lowassa. Wako tayari kufanya chochote
kupata madaraka. Bahati nzuri hadi sasa mambo
mengi wanayoyafanya ni maigizo tu, ikiwemo hili
la kutengeneza mazoezi feki na kuitengea bajeti
picha ili ichapwe gazetini ni kusambazwa
mitandaoni. Mungu Ibariki nchi yetu