Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Sio kununuliwa mkuu ndio ari halisi hiyo inajulikana kwenye richmond alitolewa kafara lakini mhusika mkuu anajulikana hilo liko wazi
 
Vijana tunajadili Sera kuendana na mahitaji kisha tunajadili utekelezaji kuendana na nyakati kisha tunamuangalia nani wakumkabidhi kutuvusha.

Alie na matatizo na Edward akosoe na apendekeze amtakae kuendana na mahitaji Kisha utekelezaji wa mahitaji.utazunguka na utarudi katika usimamizi wa Sera na kusimamia makubaliano ya vikao hapo utamjua Edward Lowassa.

Anayesema Edward mwizi aje na ushahidi , ikiwa Dr Slaa anatangaza list ya mafisadi hakumtaja Edward Lowassa, ikiwa hata miezi miwili haija pita bado Freeman Aikael Mbowe ametueleza katika bunge kikao 16/17 kuwa bunge lilipotoshwa kuhusu Richmond na Serikali inadaiwa dola million 102 za kimarekani na serikali inaona haya maana ilikurupuka kupitia bunge na ndio maana kauli ya Feb 7, 2008 imejieleza pale Edward Lowassa alipo nena kuwa tatizo ni Uwaziri Mkuu.

Usimamizi wowote katika dhamana unayopewa lazima uwe na maamuzi na makini kuwaokoa unaowaongoza Edward alifanya maamuzi yenye tija hapa.

1.Maji kanda ya ziwa mbele ya waingereza na wa misri na sasa watu wanakunywa na kuyaoga.

2. Aulizwe Dr Dau namna walivyo shurutishwa kufikiri na Edward Lowassa katika ujenzi Wa chuo Dodoma na sasa watoto wa maskini wananufaika.

3. Alifanya maamuzi kuiokoa nchi kuto kwenda gizani na ndio maana pamoja na hila zote bado serikali inanunua kwa kulipa capacity charge kutoka katika generator zile zile, ambazo zilimilikiwa na RICHMOND , DOWANS na sasa SYMBION POWER.

Kama kijana lazima ufikiri kwa kina namna mwelekeo Wa nchi ulipo , tazama hatuja maliza miezi sita alisema ajira ni Bomu linalosubiriwa kulipuka, sasa tumeona mshimshike wa panya road.

Vijana ni wajibu tufikiri taifa lijalo la mbele ambapo sisi tutakuwa wazee ambao taifa linapaswa kutulea, lazima tufanye maamuzi makini yaliyo na matumaini kwa Watanzania na bila shaka uhitaji wetu upo kwa Edward Lowassa, ili tufanye nae kazi kujenga taifa litakalo tuenzi siku zote.

Edward Lowassa ni kiongozi makini kwani ni kiongozi pekee ambaye anaonyesha vipaumbele katika falsafa yake ya kuijenga nchi anasema haya 1. Elimu 2.Elimu 3.Elimu 4. Afya 5. Kufuta umasikini. Hapo utaona umakini dira/ vision na si kukurupuka kama wengine wanavyo Fanya.

Najua nafasi ya urais kila mtu ataitaka lakini , sisi kama vijana ni muhimu kuangalia kwa umakini dira na mahitaji yetu na pia tusione haya kuwajadili walio onyesha nia , ila kwa Edward Lowassa ndio chaguo sahihi la mahitaji ya kizazi hiki cha kati ya umri wa miaka 18 hadi 45.

Mungu atujaze Hekima sasa kwani tuana paswa kufanya maamuzi katika kuangaza matumaini mapya.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.

MAAMUZI NA MATUMAINI MAPYA 2015 NA EDWARD LOWASSA.

Ahsanteni.
 
Wadau Jf,

Nimekaa na kutafakari ile siku itakapowadia ya Lowasa kwenda kuchukua fomu ya kugombea urais wa JMT, nahisi ardhi ya Tanzania itatikisika!!, ni mwanasiasa mwenye nguvu ya ajabu mithili ya Tsunami. Kwa utafiti wangu ninaoendelea kuufanya mitaani, Mh Lowasa anakubalika sana kwa jamii, kashifa nyingi anazotupiwa hazina ushahidi wowote, kifupi ni za kutunga ndio maana wote wanaomshutumu hawamtaji direct wanaogopa kumface. Ni type ya rais anayetakiwa na Tanzania ya leo. Hatutaki umasikini wa mtu iwe ni sifa ya mtu kuwa rais. Tunataka rais mzalendo, asiyeogopa kutoa maamuzi magumu kwa manufaa ya Taifa na mwenye upeo wa masuala ya uchumi na biashara.

Nasema tena ardhi ya Tanzania itatikisika siku Lowasa akichukua fomu kuogombea urais!!
 
Mbona unacoment mwenyewe? Nchi itatikisika kweli kwani ni ajabu kwa fisadi kuthubutu kuchukua fomu!
 
Mbona unacoment mwenyewe? Nchi itatikisika kweli kwani ni ajabu kwa fisadi kuthubutu kuchukua fomu!

Mkuu m4cjb naona huyu Simchezo aka fresh ya shamba anajitekenya na kucheka mwenyewe.

Kweli mafisadi yana nguvu ya kifisadi na ndio maana nchi itatikisika kwa mshangao. Hadi kaburi la mwalimu litatikisika
 
Last edited by a moderator:
Mbona Siku alivyojiuzuru uwaziri haikutikisika. na Hapo Ndipo ukawa watakapopitia. ksb Lowasa anakubalika angefanya siasa Za harakati. na sio siasa ya kugawa pesa.
 
Akitoka CCM hiyo itakuwa mwisho wa Political Career yake.
 

Attachments

  • 1420553799747.jpg
    1420553799747.jpg
    45 KB · Views: 316
Halafu nyie sijui nani kawaambia kuwa Lowasa anasifa za kuwa Rais kwani ubaya wa lowasa wote huu kweli hamuuoni?
 
Mbona Siku alivyojiuzuru uwaziri haikutikisika. na Hapo Ndipo ukawa watakapopitia. ksb Lowasa anakubalika angefanya siasa Za harakati. na sio siasa ya kugawa pesa.
Siyo lowasa wala ukawa Rais atatoka chama tawala ila siyo miongoni mwa hawa walionesha nia ya kugombea mapema kiasi hiki.
 
jamani kiukweli huyu mbaba amebarikiwa na mungu.jamani huyu mbaba ana nywele nzuri sana,jamani sura yake ni ya uhandsome na anavutia kweli.jamani huwa akivaa na miwani yake huwa namtani sana.jamani nawaombeni tumkubalie awe rais wetu.nawasilisha
sio shoga we kweli?!
 
jamani kiukweli huyu mbaba amebarikiwa na mungu.jamani huyu mbaba ana nywele nzuri sana,jamani sura yake ni ya uhandsome na anavutia kweli.jamani huwa akivaa na miwani yake huwa namtani sana.jamani nawaombeni tumkubalie awe rais wetu.nawasilisha

Dah kumbe JF ina gays wengi sana, huyu nae ni mmoja wao...
 
Hakuna mwingine zaidi yake wa kuchukua nchi.
 

Attachments

  • 1420567100069.jpg
    1420567100069.jpg
    20.1 KB · Views: 68
  • 1420567128752.jpg
    1420567128752.jpg
    50.4 KB · Views: 70
  • 1420567157586.jpg
    1420567157586.jpg
    43.5 KB · Views: 68
  • 1420567186927.jpg
    1420567186927.jpg
    39.3 KB · Views: 71
Taarifa za kuaminika kutoka ndani vikao vinavyoendelea huko Zanzibar zinasema kuna Uwezekano wa Mbunge wa Monduli mh, Edward Lowassa kupitishwa na kuwa mgombea wa CCM mapema mwezi mei mwaka huu , taarifa hizi ambazo zimevujishwa na kiongozi mmoja na kigogo mwandamizi wa CCM ambaye yupo huko kisiwani ambaye alisikika akisema " Hakuna mtu mwenye hati miliki ya CCM wote waliopo ndani ya CCM ni wanachama na kiongozi anachagulia na wanachama , hivyo hatuwezi kumkataa ama kumfukuza EL kwasababu zipi kwakua na wafuasi wengi wanao mtaka yeye kuwa Raisi ama ?

Wananchi wana Imani na Ndugu Lowassa kwanni asipitishwe na Chama chetu , alikazia kuwa na Tumesikia wananchi wakipiga Nyimbo zake tumeona vijana wakimuunga mkono sana sisi hatuwezi kufanya kama hilo tupo makini " hatuwezi kuua CCM kwasababu yakuacha kumpitisha Lowassa kwa mfano mimi binafsi ni mjumbe CC na pia namkubali Lowassa, kwakua anakubalika na wanachama na Upinzani pia kutokana hali halisi ya mwenyekiti anapokiacha Chama kikiwa katika hali mbaya na kushndwa kufanya maamuzi katika mambo ya msingi katika Chama na Serikali alisikika akisema kiongozi huyo mwenye nafasi na sehemu kubwa ya maamuzi ndani ya CCM " kutokana na hali halisi iliyopo hapa nchini kwasasa inaonekana dhahiri kuwa Lowassa ndio kiongozi aliyenaushawishi mkubwa ndani ya CCM na Nje ya CCM na mwenye nafasi ya kuwa Raisi wa awamu ya 5 ya Tanzania ,

Tusubiri mda si mrefu baadaye Leo mtaona yatakayojiri huko Visiwani .........
 
Taarifa za kuaminika kutoka ndani vikao vinavyoendelea huko Zanzibar zinasema kuna Uwezekano wa Mbunge wa Monduli mh, Edward Lowassa kupitishwa na kuwa mgombea wa CCM mapema mwezi mei mwaka huu , taarifa hizi ambazo zimevujishwa na kiongozi mmoja na kigogo mwandamizi wa CCM ambaye yupo huko kisiwani ambaye alisikika akisema " Hakuna mtu mwenye hati miliki ya CCM wote waliopo ndani ya CCM ni wanachama na kiongozi anachagulia na wanachama , hivyo hatuwezi kumkataa ama kumfukuza EL kwasababu zipi kwakua na wafuasi wengi wanao mtaka yeye kuwa Raisi ama ? Wananchi wana Imani na Ndugu Lowassa kwanni asipitishwe na Chama chetu , alikazia kuwa na Tumesikia wananchi wakipiga Nyimbo zake tumeona vijana wakimuunga mkono sana sisi hatuwezi kufanya kama hilo tupo makini " hatuwezi kuua CCM kwasababu yakuacha kumpitisha Lowassa kwa mfano mimi binafsi ni mjumbe CC na pia namkubali Lowassa, kwakua anakubalika na wanachama na Upinzani pia kutokana hali halisi ya mwenyekiti anapokiacha Chama kikiwa katika hali mbaya na kushndwa kufanya maamuzi katika mambo ya msingi katika Chama na Serikali alisikika akisema kiongozi huyo mwenye nafasi na sehemu kubwa ya maamuzi ndani ya CCM " kutokana na hali halisi iliyopo hapa nchini kwasasa inaonekana dhahiri kuwa Lowassa ndio kiongozi aliyenaushawishi mkubwa ndani ya CCM na Nje ya CCM na mwenye nafasi ya kuwa Raisi wa awamu ya 5 ya Tanzania ,

Tusubiri mda si mrefu baadaye Leo mtaona yatakayojiri huko Visiwani .........

Hapa nimetoka kapa..
 
Back
Top Bottom