Kwa kipekee kabisa naipongeza Serikali kwa kuanzisha kodi ya kizalendo kwenye miamala ya simu. Naomba Watanzania tuiunge mkono

msovero

JF-Expert Member
Jun 30, 2019
839
1,472
Hulka yetu watanzania tuliowengi hatupendi kulipa kodi kwa hiari ila ni wa kwanza kuilamu serikali pale inaposhindwa kuleta huduma za maendeleo.

Yaani tunafikiri pengine maendeleo yanakuja tu kama mvua ishukavyo kutoka mawinguni au labda kwamba nchi inaweza kujiendesha yenyewe pasipo watu kulipa kodi, jambo ambalo si kweli.

Inashangaza kwamba leo tunalia kwa sababu serikali imetuwekea kodi ya uzalendo kwenye miamala ya simu lakini tunasahau kwamba taifa letu bado ni changa na linakabiliwa na changamoto lukuki zikiwemo changamoto za ubovu wa bara bara mjini na vijijini, changamoto ya maji safi na salama, changamoto ya madawati, changamoto ya walimu, hospitali, madawa, umeme n.k

Kimsingi wa kutatua changamoto hizi ni sisi wenyewe, tusitegemee kwamba kuna mtu kutoka taifa lingine wa kuja kututatulia changamoto zetu. Kumbe sasa inatupasa kufunga mikanda na vibwebwe kisawa sawa ili tuweze kuzitatua, na njia pekee ya kuzitatua ni kupitia kodi.

Hata mataifa yaliyoendelea kama marekani, uingereza, na china hayakufika hapo yalipo hivi hivi nao walipitia ugumu kidogo kama ambavyo sisi tunaona taabu kulipa kodi ya uzalendo kwenye miamala ya simu lakini baada ya muda fulani walizoea na kuona kwamba kulipa kodi ni suala la kawaida na ndio maana wameweza kupiga hatua kubwa kiuchumi na kuwa hapo walipo hii leo. Hata sisi kwakuwa ndio tunaanza mwanzo utakuwa mgumu lakini baadaye tutazoea na hii kodi ya kizalendo tutakuja kuona ni suala la kawaida kabisa.

Nachotaka kuwambia Watanzania wenzangu, tuonyeshe uzalendo tulipe kodi kwa maendeleo ya Taifa letu kwa sababu bila kodi.

• Hakuna bara bara itajengwa
Hakuna hospitali itajengwa,
Hakuna shule itajengwa

• Watoto wetu wataendelea kukaa chini

• Hakutakuwa na pesa za kununua madawa

• Watumishi wa umma watashindwa kupandishwa madaraja ambayo hayajapanda kwa miaka zaidi ya mitano

• Watoto wetu watakosa vipindi kwa sababu serikali haitakuwa na uwezo wa kuajiri walimu

• Mama zetu hospitali watashindwa kujifungua salama kwa sababu serikali haitakuwa na pesa za kuboresha huduma za afya

• Vile vile hata miradi mikubwa tuliyoanzisha kama SGR, SG n.k itakwama kwa sababu ili ikamilike kunahitajika fedha ambazo zinapatikana kupitia wananchi kodi ya wananchi.

Kwahivyo watanzania wenzangu tusione kama serikali haina nia njema na sisi, La hasha! tulipe kodi na tukishalipa kodi sisi kama wananchi tuchukue jukumu la kuisimamia serikali ili kusudi kodi tuliyolipa isipotee bure au kuishia kwenye mifuko ya wachache bali itumike katika malengo yaliyokusudiwa na matunda yake yaonekane.

KODI YA UZALENDO KWA MAENDLEO YA TAIFA.

Naomba kuwasilisha.
 
Tatizo siyo kulipa kodi! Tunachotaka ni Serikali kujisafisha kwanza kabla ya kutuletea hiyo mikodi yao!

Serikali ya CCM kwa miaka mingi inachezea hizo kodi zetu kwa mambo mengi ya kipuuzi. Mfano kununua magari ya kifahari, kuitisha uchaguzi wa marudio, kuendelea kuvikumbatia vyeo vya wakuu wa mikoa, wilaya, nk. Kutamalaki kwa ufisadi, vitendo vya rushwa, utakatishaji fedha, uhujumu uchumi, ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka, nk.

Mambo haya ndiyo yanayo tufanya tupinge hizi tozo na kodi kandamizi.
 
Nina uhakika kabisa wewe ni mwajiriwa. Inawezekana unaishi kwenye nyumba ya serikali na umepewa usafiri. Vocha unawekewa kila mwezi. Hakika huwezi ukaona uchungu wa hiyo kodi.

Ili nikuunge mkono kwenye hoja yako, naomba angalau uniambie KWA MWAKA 2020 SERIKALI ILIKUSANYA SHS NGAPI KAMA KODI, NA KATIKA HAYO MAKUSANYO, SHS NGAPI ZILIENDA KWENYE MISHAHARA NA MARUPURUPU NA NGAPI ZILIENDA KWENYE MAENDELEO?

Baada ya hapo niambie kwanini unaamini hii kodi itaenda kwenye maendeleo.
 
Ningeamini hiyo kodi ina umuhimu na maana endapo tu.

Wabunge wangekubali kwa hiari yao wakatwe mshara wa mwezi + posho(Millioni 12)

Walau wafikie mshahara wa mwalimu (500k-700k) minimum.

Pia kwenye mshahara huo wabunge wakubali ukatwe kodi pia kama wakatwavyo walimu.

Na posho za kikao ziwe walau 30k

Hayo mamilioni yatakayobaki ndio uzalendo huo ! Na tunaweza kufanyia issue zingine nyingi za msingi.
 
Waangalie namna ya kubalance serikali kupunguza matumizi lakini Kama kila kinachoingia wahuni wanachota..juz bot watu wamechota na hatusikii wakiadhibiwa hela itachukuliwa na bado Cha msingi hakitafanyika washenzi tuu

hii ndio changamoto tunaona kodi zetu zinavyotumiwa hovyoo. Mkurugenzi anatumia gari la mil 400+. wabunge wananunuliwa kwa hizo hizo kodi za kizalendo. viongozi wanaiba.

matajiri, vigogo wa ccm hawalipi kodi. makampuni ya madini wanakwepa kodi. kesi zikifunguliwa zinaishia juu kwa juu. hakuna mtu asiependa kulipa kodi ila kwa usimamizi wa hizi kodi kunakatisha tamaa.

china kuna sheria kali za kodi na usimamizi wake. na sheria ni msimeno ata awe kiongozi gani akikwepa Kodi mkono wa sheria lazima umkute.

hii kodi kidogo iliyokuwa inakusanywa wameshindwa kuisimamia vyema. jeee ya kizalendo inayoongezeka ndo wataweza kuisimamia????
 
Hulka yetu watanzania tuliowengi hatupendi kulipa kodi kwa hiari ila ni wa kwanza kuilamu serikali pale inaposhindwa kuleta huduma za maendeleo.

Yaani tunafikiri pengine maendeleo yanakuja tu kama mvua ishukavyo kutoka mawinguni au labda kwamba nchi inaweza kujiendesha yenyewe pasipo watu kulipa kodi, jambo ambalo si kweli.

Inashangaza kwamba leo tunalia kwa sababu serikali imetuwekea kodi ya uzalendo kwenye miamala ya simu lakini tunasahau kwamba taifa letu bado ni changa na linakabiliwa na changamoto lukuki zikiwemo changamoto za ubovu wa bara bara mjini na vijijini, changamoto ya maji safi na salama, changamoto ya madawati, changamoto ya walimu, hospitali, madawa, umeme n.k

Kimsingi wa kutatua changamoto hizi ni sisi wenyewe, tusitegemee kwamba kuna mtu kutoka taifa lingine wa kuja kututatulia changamoto zetu. Kumbe sasa inatupasa kufunga mikanda na vibwebwe kisawa sawa ili tuweze kuzitatua, na njia pekee ya kuzitatua ni kupitia kodi.

Hata mataifa yaliyoendelea kama marekani, uingereza, na china hayakufika hapo yalipo hivi hivi nao walipitia ugumu kidogo kama ambavyo sisi tunaona taabu kulipa kodi ya uzalendo kwenye miamala ya simu lakini baada ya muda fulani walizoea na kuona kwamba kulipa kodi ni suala la kawaida na ndio maana wameweza kupiga hatua kubwa kiuchumi na kuwa hapo walipo hii leo. Hata sisi kwakuwa ndio tunaanza mwanzo utakuwa mgumu lakini baadaye tutazoea na hii kodi ya kizalendo tutakuja kuona ni suala la kawaida kabisa.

Nachotaka kuwambia watanzania wenzangu, tuonyeshe uzalendo tulipe kodi kwa maendeleo ya Taifa letu kwa sababu bila kodi,

•Hakuna bara bara itajengwa
Hakuna hospitali itajengwa,
Hakuna shule itajengwa

•Watoto wetu wataendelea kukaa chini

•Hakutakuwa na pesa za kununua madawa

•Watumishi wa umma watashindwa kupandishwa madaraja ambayo hayajapanda kwa miaka zaidi ya mitano

•Watoto wetu watakosa vipindi kwa sababu serikali haitakuwa na uwezo wa kuajiri walimu

•Mama zetu hospitali watashindwa kujifungua salama kwa sababu serikali haitakuwa na pesa za kuboresha huduma za afya

•Vile vile hata miradi mikubwa tuliyoanzisha kama SGR, SG n.k itakwama kwa sababu ili ikamilike kunahitajika fedha ambazo zinapatikana kupitia wananchi kodi ya wananchi.

Kwahivyo watanzania wenzangu tusione kama serikali haina nia njema na sisi, La hasha! tulipe kodi na tukishalipa kodi sisi kama wananchi tuchukue jukumu la kuisimamia serikali ili kusudi kodi tuliyolipa isipotee bure au kuishia kwenye mifuko ya wachache bali itumike katika malengo yaliyokusudiwa na matunda yake yaonekane.

KODI YA UZALENDO KWA MAENDLEO YA TAIFA.

Naomba kuwasilisha.
peleka upuuzi wako kwa nduguzo na si kwa jamii elewa
 
Kuna watu humu mnanufaika sana na huu udhalimu.

Na huenda ndio nyie mnaotunga Kodi za kinyonyaji mkikaa kule mjengoni.

Mngekua wazalendo kweli,
Mngekua kua mifano kwa watanzania wengine na NYIE mkatwe Kodi Kama sisi wananchi mskie uchungu unavouma.

Amaa kweli,
alieshiba hamkumbuki mwenye njaa, hizi laana zitawatafuna Mbwa nyie
 
Hulka yetu watanzania tuliowengi hatupendi kulipa kodi kwa hiari ila ni wa kwanza kuilamu serikali pale inaposhindwa kuleta huduma za maendeleo.

Yaani tunafikiri pengine maendeleo yanakuja tu kama mvua ishukavyo kutoka mawinguni au labda kwamba nchi inaweza kujiendesha yenyewe pasipo watu kulipa kodi, jambo ambalo si kweli.

Inashangaza kwamba leo tunalia kwa sababu serikali imetuwekea kodi ya uzalendo kwenye miamala ya simu lakini tunasahau kwamba taifa letu bado ni changa na linakabiliwa na changamoto lukuki zikiwemo changamoto za ubovu wa bara bara mjini na vijijini, changamoto ya maji safi na salama, changamoto ya madawati, changamoto ya walimu, hospitali, madawa, umeme n.k

Kimsingi wa kutatua changamoto hizi ni sisi wenyewe, tusitegemee kwamba kuna mtu kutoka taifa lingine wa kuja kututatulia changamoto zetu. Kumbe sasa inatupasa kufunga mikanda na vibwebwe kisawa sawa ili tuweze kuzitatua, na njia pekee ya kuzitatua ni kupitia kodi.

Hata mataifa yaliyoendelea kama marekani, uingereza, na china hayakufika hapo yalipo hivi hivi nao walipitia ugumu kidogo kama ambavyo sisi tunaona taabu kulipa kodi ya uzalendo kwenye miamala ya simu lakini baada ya muda fulani walizoea na kuona kwamba kulipa kodi ni suala la kawaida na ndio maana wameweza kupiga hatua kubwa kiuchumi na kuwa hapo walipo hii leo. Hata sisi kwakuwa ndio tunaanza mwanzo utakuwa mgumu lakini baadaye tutazoea na hii kodi ya kizalendo tutakuja kuona ni suala la kawaida kabisa.

Nachotaka kuwambia watanzania wenzangu, tuonyeshe uzalendo tulipe kodi kwa maendeleo ya Taifa letu kwa sababu bila kodi,

•Hakuna bara bara itajengwa
Hakuna hospitali itajengwa,
Hakuna shule itajengwa

•Watoto wetu wataendelea kukaa chini

•Hakutakuwa na pesa za kununua madawa

•Watumishi wa umma watashindwa kupandishwa madaraja ambayo hayajapanda kwa miaka zaidi ya mitano

•Watoto wetu watakosa vipindi kwa sababu serikali haitakuwa na uwezo wa kuajiri walimu

•Mama zetu hospitali watashindwa kujifungua salama kwa sababu serikali haitakuwa na pesa za kuboresha huduma za afya

•Vile vile hata miradi mikubwa tuliyoanzisha kama SGR, SG n.k itakwama kwa sababu ili ikamilike kunahitajika fedha ambazo zinapatikana kupitia wananchi kodi ya wananchi.

Kwahivyo watanzania wenzangu tusione kama serikali haina nia njema na sisi, La hasha! tulipe kodi na tukishalipa kodi sisi kama wananchi tuchukue jukumu la kuisimamia serikali ili kusudi kodi tuliyolipa isipotee bure au kuishia kwenye mifuko ya wachache bali itumike katika malengo yaliyokusudiwa na matunda yake yaonekane.

KODI YA UZALENDO KWA MAENDLEO YA TAIFA.

Naomba kuwasilisha.
Itakuwa uzalendo kama wabunge watalipa PAYE kwenye salary na mafao yao.
 
hii ndio changamoto tunaona kodi zetu zinavyotumiwa hovyoo. Mkurugenzi anatumia gari la mil 400+. wabunge wananunuliwa kwa hizo hizo kodi za kizalendo. viongozi wanaiba.

matajiri, vigogo wa ccm hawalipi kodi. makampuni ya madini wanakwepa kodi. kesi zikifunguliwa zinaishia juu kwa juu. hakuna mtu asiependa kulipa kodi ila kwa usimamizi wa hizi kodi kunakatisha tamaa.

china kuna sheria kali za kodi na usimamizi wake. na sheria ni msimeno ata awe kiongozi gani akikwepa Kodi mkono wa sheria lazima umkute.

hii kodi kidogo iliyokuwa inakusanywa wameshindwa kuisimamia vyema. jeee ya kizalendo inayoongezeka ndo wataweza kuisimamia????
alafu wanajisifia eti" VIONGOZI WOTE WA CCM WANAENDESHA MAVIEITI" where they get money to buy that car kama si kodi zetu
 
Hayo makusanyo wanadai yataenda kwenye account ya mshikamano! Hio account ya mshikamano ndio nahisi upigaji utafanyika kirahisi maana hizo hazipelekwi hazina hata mtu akidokoa hamna mtu wa kuhoji zaidi😂😂😂😅😅 hazitakuwa audited! Sidhani na ndio maana hazijaungwa na VAT!
 
Hulka yetu watanzania tuliowengi hatupendi kulipa kodi kwa hiari ila ni wa kwanza kuilamu serikali pale inaposhindwa kuleta huduma za maendeleo.

Yaani tunafikiri pengine maendeleo yanakuja tu kama mvua ishukavyo kutoka mawinguni au labda kwamba nchi inaweza kujiendesha yenyewe pasipo watu kulipa kodi, jambo ambalo si kweli.

Inashangaza kwamba leo tunalia kwa sababu serikali imetuwekea kodi ya uzalendo kwenye miamala ya simu lakini tunasahau kwamba taifa letu bado ni changa na linakabiliwa na changamoto lukuki zikiwemo changamoto za ubovu wa bara bara mjini na vijijini, changamoto ya maji safi na salama, changamoto ya madawati, changamoto ya walimu, hospitali, madawa, umeme n.k

Kimsingi wa kutatua changamoto hizi ni sisi wenyewe, tusitegemee kwamba kuna mtu kutoka taifa lingine wa kuja kututatulia changamoto zetu. Kumbe sasa inatupasa kufunga mikanda na vibwebwe kisawa sawa ili tuweze kuzitatua, na njia pekee ya kuzitatua ni kupitia kodi.

Hata mataifa yaliyoendelea kama marekani, uingereza, na china hayakufika hapo yalipo hivi hivi nao walipitia ugumu kidogo kama ambavyo sisi tunaona taabu kulipa kodi ya uzalendo kwenye miamala ya simu lakini baada ya muda fulani walizoea na kuona kwamba kulipa kodi ni suala la kawaida na ndio maana wameweza kupiga hatua kubwa kiuchumi na kuwa hapo walipo hii leo. Hata sisi kwakuwa ndio tunaanza mwanzo utakuwa mgumu lakini baadaye tutazoea na hii kodi ya kizalendo tutakuja kuona ni suala la kawaida kabisa.

Nachotaka kuwambia watanzania wenzangu, tuonyeshe uzalendo tulipe kodi kwa maendeleo ya Taifa letu kwa sababu bila kodi,

•Hakuna bara bara itajengwa
Hakuna hospitali itajengwa,
Hakuna shule itajengwa

•Watoto wetu wataendelea kukaa chini

•Hakutakuwa na pesa za kununua madawa

•Watumishi wa umma watashindwa kupandishwa madaraja ambayo hayajapanda kwa miaka zaidi ya mitano

•Watoto wetu watakosa vipindi kwa sababu serikali haitakuwa na uwezo wa kuajiri walimu

•Mama zetu hospitali watashindwa kujifungua salama kwa sababu serikali haitakuwa na pesa za kuboresha huduma za afya

•Vile vile hata miradi mikubwa tuliyoanzisha kama SGR, SG n.k itakwama kwa sababu ili ikamilike kunahitajika fedha ambazo zinapatikana kupitia wananchi kodi ya wananchi.

Kwahivyo watanzania wenzangu tusione kama serikali haina nia njema na sisi, La hasha! tulipe kodi na tukishalipa kodi sisi kama wananchi tuchukue jukumu la kuisimamia serikali ili kusudi kodi tuliyolipa isipotee bure au kuishia kwenye mifuko ya wachache bali itumike katika malengo yaliyokusudiwa na matunda yake yaonekane.

KODI YA UZALENDO KWA MAENDLEO YA TAIFA.

Naomba kuwasilisha.
UMETUMWA NA MWIGULU. hana new idea mawazo yamedanda kwenye makato ya kodi.
tengeneza matajiri uwakate kodi. hakuna nchi wananchi wa kawaida wanakatwa kodi kubwa kama hiz.
 
Hulka yetu watanzania tuliowengi hatupendi kulipa kodi kwa hiari ila ni wa kwanza kuilamu serikali pale inaposhindwa kuleta huduma za maendeleo.

Yaani tunafikiri pengine maendeleo yanakuja tu kama mvua ishukavyo kutoka mawinguni au labda kwamba nchi inaweza kujiendesha yenyewe pasipo watu kulipa kodi, jambo ambalo si kweli.

Inashangaza kwamba leo tunalia kwa sababu serikali imetuwekea kodi ya uzalendo kwenye miamala ya simu lakini tunasahau kwamba taifa letu bado ni changa na linakabiliwa na changamoto lukuki zikiwemo changamoto za ubovu wa bara bara mjini na vijijini, changamoto ya maji safi na salama, changamoto ya madawati, changamoto ya walimu, hospitali, madawa, umeme n.k

Kimsingi wa kutatua changamoto hizi ni sisi wenyewe, tusitegemee kwamba kuna mtu kutoka taifa lingine wa kuja kututatulia changamoto zetu. Kumbe sasa inatupasa kufunga mikanda na vibwebwe kisawa sawa ili tuweze kuzitatua, na njia pekee ya kuzitatua ni kupitia kodi.

Hata mataifa yaliyoendelea kama marekani, uingereza, na china hayakufika hapo yalipo hivi hivi nao walipitia ugumu kidogo kama ambavyo sisi tunaona taabu kulipa kodi ya uzalendo kwenye miamala ya simu lakini baada ya muda fulani walizoea na kuona kwamba kulipa kodi ni suala la kawaida na ndio maana wameweza kupiga hatua kubwa kiuchumi na kuwa hapo walipo hii leo. Hata sisi kwakuwa ndio tunaanza mwanzo utakuwa mgumu lakini baadaye tutazoea na hii kodi ya kizalendo tutakuja kuona ni suala la kawaida kabisa.

Nachotaka kuwambia watanzania wenzangu, tuonyeshe uzalendo tulipe kodi kwa maendeleo ya Taifa letu kwa sababu bila kodi,

•Hakuna bara bara itajengwa
Hakuna hospitali itajengwa,
Hakuna shule itajengwa

•Watoto wetu wataendelea kukaa chini

•Hakutakuwa na pesa za kununua madawa

•Watumishi wa umma watashindwa kupandishwa madaraja ambayo hayajapanda kwa miaka zaidi ya mitano

•Watoto wetu watakosa vipindi kwa sababu serikali haitakuwa na uwezo wa kuajiri walimu

•Mama zetu hospitali watashindwa kujifungua salama kwa sababu serikali haitakuwa na pesa za kuboresha huduma za afya

•Vile vile hata miradi mikubwa tuliyoanzisha kama SGR, SG n.k itakwama kwa sababu ili ikamilike kunahitajika fedha ambazo zinapatikana kupitia wananchi kodi ya wananchi.

Kwahivyo watanzania wenzangu tusione kama serikali haina nia njema na sisi, La hasha! tulipe kodi na tukishalipa kodi sisi kama wananchi tuchukue jukumu la kuisimamia serikali ili kusudi kodi tuliyolipa isipotee bure au kuishia kwenye mifuko ya wachache bali itumike katika malengo yaliyokusudiwa na matunda yake yaonekane.

KODI YA UZALENDO KWA MAENDLEO YA TAIFA.

Naomba kuwasilisha.
Wewe ni hopeless kabisa hujui kwamba hiyo Kofi ya miamala ni kubwa mno? Ataiwezaje maskini wa kijijini Mwenye kipato cha shs 100.000 kwa mwaka? Au we we ni mbunge ccm usiyekuwa na haruma kwa wapiga kura wako? Kwa sababu ulipita bila kupingwa?
 
Back
Top Bottom