Kwa jibu la mmoja wa wagombea Urais nchini kwetu Tanzania, hivi Katiba ya nchi inasemaje haswa juu ya uhuru wa faragha (privacy)?

Mwanamayu

JF-Expert Member
May 7, 2010
11,349
6,476
Kuna mgombea mmoja wa kiti cha Urais amekuwa akinukuu katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (toleo la 20 Juni, 2005) ibara ya 16 mara anapojibu swali la waandishi wa habari akiwemo yule wa BBC wakati wa hardtalk kuhusu masuala ya ushoga. Ibara hiyo inahusu haki ya faragha na usalama ambayo ipo kwenye fungu la haki ya kuishi. Ibara hiyo inasomeka kama ifuatavyo:

"16.- (1) Kila mtu anastahili kuheshimiwa na kupata hifadhi kwa nafsi yake, maisha yake binafsi na familia yake na unyumba wake, na pia heshima na hifadhi ya maskani yake na mawasiliano yake ya binafsi.

(2) Kwa madhumuni ya kuhifadhi haki ya mtu kwa mujibu wa ibara hii, Mamlaka ya Nchi itaweka utaratibu wa sheria kuhusu hali, namna na kiasi ambacho haki ya mtu ya faragha na ya usalama wa nafsi yake, mali yake na maskani yake, yaweza kuingiliwa bila ya kuathiri ibara hii."

Pia kifungu kidogo cha pili kinatoa ruhusa faragha kuingiliwa.

Kwa mujibu wa sheria zetu, ushoga ni kosa la jinai, hivyo kwa mujibu wa katiba kama jinai inatendeka, basi faragha hiyo itaingiliwa kwa mujibu wa sheria husika zinazoruhusiwa na katiba. Na sio kweli kuwa faragha hiyo haingiliwi kabisa kwa mujibu wa jibu la mgombea huyo.

Yaweza kuwa kumtia hatiani shoga ni ngumu kama rushwa hasa pale wote wawili wanapokubaliana, ila kwa mujibu wa mila na desturi zetu na maana ya maneno yaliyotumika kwenye katiba kama 'unyumba' yawezabainika kwa kiwango fulani. Pia sheria ya ndoa ipo wazi kwenye kutokutambua ushoga, fuatiilia hapa Sheria Kiganjani.

Je, huyo mgombea hakumbuki faragha yake iliingiliwa kisheria pale alipopekuliwa nyumbani kwake Tegeta Dar baada ya kugoma kupimwa mkojo? Na, kwa nini haisomi hiyo nukuu ya ibara ya katiba ili wananchi wanaomsikiliza wasiokuwa na muda au uwezo wa kupambanua katiba waelewe vizuri?

Kuna mfano, ingawaje katiba yao siifahamu vizuri ila ni wazuri kwenye haya mambo ya faragha, huko Uingereza, polisi walifika nyumbani kwa Boris Johnson pale walipozozana na mchumba wake, Carrie Symonds (tazama video hapo chini).

 
Ngoja nilete katiba ya mwaka 77 ili twende sawa. Huu uzi sio wa kibabaishaji wala porojo, ni neno kwa neno, nukuu kwa nukuu, nakili kwa nakili.





privacy
/ˈprɪvəsi,ˈprʌɪvəsi/
Learn to pronounce

noun
  1. a state in which one is not observed or disturbed by other people.
    "she returned to the privacy of her own home"
 
JPM wakati anapambana na Lowassa alipiga push-ups nyingi mara kadhaa, ulifahamu maana yake? Dhihaka kwa Lowassa kuhusu afya yake. Rhetorical language.

Wakati huu anapambana na amepigishwa magoti mara mbili akiomba kura, unajua maana yake??

Mataga Tafuta thamani ya X......
 
Faragha ni nini? umenukuu kifungu cha Faragha katika katiba. Weka nukuu ya kifungu cha sheria pia kuhusu ushoga ili kubalance. Sipendi ushoga na sita kujapenda ila nataka kujua hoja ya kisheria. Kama tuna mapungufu kisheria tujue ili tujisahihishe hilo tu.
 
Swali laangu kwako ,utamtambuaje kuwa Mtu flani ni Shoga !?

Uta thibitishaje hilo !?

Tuanzie hapo na Kazi ngumu ndio ipo hapo ,hata hawa Dada poa imekuwa ngumu kuthibitika ni nani anauza Mwili au ni nani yupo na Mpenzi wake.
 
Naomba unithibitishie pasi kuacha shaka yoyote kwamba Mimi ni shoga
Shoga Sio lazima ufanye tendo mkuu Bali kitendo cha kuona ni jambo la kawaida pia ni ushoga tunatakiwa tukemee kwa nguvu zote haijalishi nani kasema . Mfano Barak Obama hakuwa shoga lakini kitendo cha kubariki ushoga moja kwa moja amejikuta anapata shutma.
 
Ushoga ni jinai chini ya kifungu kipi cha sheria au katiba. Weka ibala husika mkuu. Mazoea yana taabu zake.
 
Samahani mkuu buji nakuheshimu snaa ila sijategemea kama utakuwa na mtazamo mwepesi kwenye jambo gumu kama hili .
Fafanua shoga ni Nini/ yupi? Ushoga ni Nini? Kisha thibitisha tuhuma zako kwamba Mimi ni shoga, na Sasa niache ushoga.
Post yangu, post namba mbili ilikuwa na ubaya gani Hadi uamue kunitokana?
 
Siwezi kuwa positive kwnye kujadili ungese samahani sana. Taifa hili tunakuja kuruthisha watoto wetu umewahi kufikiria kizazi chetu baadae watakuwa Vipi?

Sasa ni kwa nini unanishambulia mimi badala ya kujadili Hoja !?.Sheria zipo kazi ipo kwenye kutafsiri hivyo Vifungu vinayo maana ipi haswa ,inafaa tuulizane Maswali magumu ili kupata Majibu lakini sio kushambuliana binafsi.Sio jambo jema Mkuu kumtuhumu tu Mtu na kuacha kujadili Hoja ,haunijui sikujui meneno makali ni ya nini !?
 
Shoga Sio lazima ufanye tendo mkuu Bali kitendo cha kuona ni jambo la kawaida pia ni ushoga tunatakiwa tukemee kwa nguvu zote haijalishi nani kasema . Mfano Barak Obama hakuwa shoga lakini kitendo cha kubariki ushoga moja kwa moja amejikuta anapata shutma.
Post yangu hapo chini in kipi Cha kufanya wewe uniite shoga?
Ngoja nilete katiba ya mwaka 77 ili twende sawa. Huu uzi sio wa kibabaishaji wala porojo, ni neno kwa neno, nukuu kwa nukuu, nakili kwa nakili.





privacy
/ˈprɪvəsi,ˈprʌɪvəsi/
Learn to pronounce

noun
  1. a state in which one is not observed or disturbed by other people.
    "she returned to the privacy of her own home"
 
Shoga Sio lazima ufanye tendo mkuu Bali kitendo cha kuona ni jambo la kawaida pia ni ushoga tunatakiwa tukemee kwa nguvu zote haijalishi nani kasema . Mfano Barak Obama hakuwa shoga lakini kitendo cha kubariki ushoga moja kwa moja amejikuta anapata shutma.
Kwa hiyo baba yako unaweza kumuita shoga? Hivi inakuwaje unakurupuka na kuanza kuwatukana watu usiowajua? Nimekuuliza maswali hujayajibu hata moja.
Moderator , Mhariri Kuna kitu weird kinaendelea, komesheni lugha za matusi humu ndani. Mtu hakujui anaanza kukutukana.
 
Post yangu hapo chini in kipi Cha kufanya wewe uniite shoga?
Alfu
Kwa hiyo baba yako unaweza kumuita shoga? Hivi inakuwaje unakurupuka na kuanza kuwatukana watu usiowajua? Nimekuuliza maswali hujayajibu hata moja.
Moderator , Mhariri Kuna kitu weird kinaendelea, komesheni lugha za matusi humu ndani. Mtu hakujui anaanza kukutukana.
mbona umekuwa Bogas sasa .... Acha izo huu mjadala umeisha Sawa
 
Kuna mgombea mmoja wa kiti cha Urais amekuwa akinukuu katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (toleo la 20 Juni, 2005) ibara ya 16 mara anapojibu swali la waandishi wa habari akiwemo yule wa BBC wakati wa hardtalk kuhusu masuala ya ushoga. Ibara hiyo inahusu haki ya faragha na usalama ambayo ipo kwenye fungu la haki ya kuishi. Ibara hiyo inasomeka kama ifuatavyo:
"16.- (1) Kila mtu anastahili kuheshimiwa na kupata hifadhi kwa nafsi yake, maisha yake binafsi na familia yake na unyumba wake, na pia heshima na hifadhi ya maskani yake na mawasiliano yake ya binafsi.
(2) Kwa madhumuni ya kuhifadhi haki ya mtu kwa mujibu wa ibara hii, Mamlaka ya Nchi itaweka utaratibu wa sheria kuhusu hali, namna na kiasi ambacho haki ya mtu ya faragha na ya usalama wa nafsi yake, mali yake na maskani yake, yaweza kuingiliwa bila ya kuathiri ibara hii."

Pia kifungu kidogo cha pili kinatoa ruhusa faragha kuingiliwa.

Kwa mujibu wa sheria zetu, ushoga ni kosa la jinai, hivyo kwa mujibu wa katiba kama jinai inatendeka, basi faragha hiyo itaingiliwa kwa mujibu wa sheria husika zinazoruhusiwa na katiba. Na sio kweli kuwa faragha hiyo haingiliwi kabisa kwa mujibu wa jibu la mgombea huyo. Yaweza kuwa kumtia hatiani shoga ni ngumu kama rushwa hasa pale wote wawili wanapokubaliana, ila kwa mujibu wa mila na desturi zetu na maana ya maneno yaliyotumika kwenye katiba kama 'unyumba' yawezabainika kwa kiwango fulani. Pia sheria ya ndoa ipo wazi kwenye kutokutambua ushoga, fuatiilia hapa Sheria Kiganjani.

Je, huyo mgombea hakumbuki faragha yake iliingiliwa kisheria pale alipopekuliwa nyumbani kwake Tegeta Dar baada ya kugoma kupimwa mkojo? Na, kwa nini haisomi hiyo nukuu ya ibara ya katiba ili wananchi wanaomsikiliza wasiokuwa na muda au uwezo wa kupambanua katiba waelewe vizuri?

Kuna mfano, ingawaje katiba yao siifahamu vizuri ila ni wazuri kwenye haya mambo ya faragha, huko Uingereza, polisi walifika nyumbani kwa Boris Johnson pale walipozozana na mchumba wake, Carrie Symonds (tazama video hapo chini).


Lissu anabwabwaja tu,

Anatumia akili kuwateka wasioelewa. Anatoa tafsiri kwa kudanganya Kama ulivyoainisha hapo juu.

Kama hoja ni privacy, kwa hiyo hata mambo mengine yanayokatazwa na sheria kama mapenzi kinyume na maumbile, mapenzi kwa ndugu wa damu, kubaka ili mradi tu ubakie chumbani, inakuwa siyo kosa! Hoja ya ajabu sana!

Anachokwepa ni kuongea ukweli kwamba alishakiri kwa "mabwana" zake kuunga mkono ushoga. Sasa anajificha kwenye chaka la privacy.
 
Back
Top Bottom