Kwa hotuba hii ya Rais, Tujiandae na mgomo mkubwa wa madaktari

Kwa kuwa hawa watu walishakubali kurudi kazini naona hasingesema tena kuhusu mgomo. Naona kama kalikoroga tena.

Nakubaliana na wewe 100%. hakuwa na sababu ya kuzungumza na wazee hawa wakati madokta wamerejea kazini na wamesema wana imani naye
 
Mkuu issue imeisha kwisha hii
sana sana Drs wataelezea masikitiko yao kuchongewa kwa wananchi basi

Halafu wewe jamaa ni mnafiki kichizi...nimeona ati unajipendekeza kwa Mwigulu Nchemba umem-PM kwa kusema,na hapa nakunukuu "Karibu jamvini mbunge wangu mpenzi,nilikuwa naomba sana ujiunge hapa JF tupambane na watu wasiotaka mawazo tofauti na ambao wanahisi kuwa chama tofauti na wewe ni dhambi..uwe mvumilivu maana hapa kuna watu wanaopenda matusi na kupenda fujo..." mwisho wa kumnukuu....yani kumbe kazi yako ni kujipendekeza tu kwa CCM na watawala wake,kazi yako ni kuwalamba miguu tu ili iweje?
 
dk ulimboka na wenzako msihofu kitu chochote,jipangeni vizuri ili kuhakikisha serikali inapata somo. Hii nchi imeoza.
hakuna cha kujipanga wafanye kazi basi hawana strategies, kwani mgomo haukufuata hata sheria ndio Attorney General aliomba mahakama ikatoa court injuction ya kuzuia mgomo ina maana madaktari hawajui sheria au walishindwa hata kuuliza sheria inasemaje??
 
Labda siku wanajeshi wakigoma ndio tunaweza kuona mabadiliko ya kweli madaktari walimu na wafanyakazi wengine migomo yao ni migomo mbuzi tu wala haina tija.Madktari walikuja na msimamo mkali hawatajadili chochote wakati mponda na Nkya wapo ofisini, ghafla wakabadilika hao magogoni wakiwa kule wakarudi wakatutangazia mgomo kwisha wanachapa kazi na wana imani na rais, hawakutoa details za majadiliano, sasa huyohuyo waliyemsifu wana imani nae kawanyea! Najua hawatathubutu kugoma tena ila wataendelea kutoa huduma duni chini ya mgomo baridi amabao ni mbaya sana maana wataumia wananchi wa kawaida na ni kinyume cha weledi wao wanatakiwa wawe wazi wamegoma kuliko kuumiza watu kimyakimya,. madokta wameenda shule ngumu sana na miongoni mwa cream ta taifa lakini kwa hili inabidi tuanze kuwafikiria vinginevyo, hawakuwa na strategies au plans b c hata d???

Osokoni wanajeshi huwa hawana kitu kinachoitwa mgomo, jeshi huwa LINAASI, haligomi!
 
Jamani alichoongea JK ni siasa, ukweli ni kwamba makubaliano ya kimsingi ya JK na Ma-Dk upo pale pale!
Ameongea kujisafisha kama kiongozi wa nchi asidharaulike ukweli ni kwamba hy ni propaganda kwa wa-tz kupitia wazee wa dsm!

Babaubaya mambo yalikuwa yameshapoa, kulikuwa na haja gani ya kuyafufua wakati jamii ilikuwa ikimpongeza kwa kumaliza tatizo?? huoni kama sasa amejipalia makaa zaidi?
 
Kwa njisi mgomo wa pili ulivyoisha, sitarajii mgomo mwingine mkubwa zaid ya ulw wa kwanza.
Mgomo wa pili ulikuwa mzito kuliko wa kwanza.
sema wa kwanza ulichikua siku nyingi lakini siku za effective mgomo zilikuwa mbili kama ilikuwa mgomo wa pili
 
KUTOKANA NA HILO, TUNAPENDA KUUTANGAZIA UMMA WA WATANZANIA KUWA TUNARUDI KAZINI RASMI KUANZIA LEO TAREHE 10/3/2012, WAKATI MHESHIMIWA RAIS AKISHUGHULIKIA MADAI YETU.

PIA WAKATI MADAI YETU YAKISHUGHUKLIKIWA TUNAPENDA KUSEMA KUWA HATUNA IMANI NA WAZIRI WA AFYA MH. DR. HAJI MPONDA NA MH. DR. LUCY NKYA, NA KUWA TUNAMSIMAMISHA RASMI UANACHAMA WA MAT MH. DR. LUCY NKYA.

MADAKTARI TUNATAMKA WAZI KUWA WAZIRI WA AFYA DR. HAJI MPONDA NA NAIBU WAKE DR. LUCY NKYA NI MAADUI WA MADAKTARI NA SEKTA YA AFYA KWA UJUMLA HAPA NCHINI NA TUNAAHIDI KUTOKUWAPA USHIRIKIANAO WA AINA YOYOTE WA KIBINAFSI AU WA KIUTENDAJI.

SOLIDARITY FOREVER.
RAIS(MAT)
hapa tunaweza kupata majibu ya hotuba ya jk
 
Mkuu issue imeisha kwisha hii
sana sana Drs wataelezea masikitiko yao kuchongewa kwa wananchi basi
Kwa vibwetere na vinyangarika wa akili ni kweli.... issue imeisha... hawaoni mbele wala hawawezi kuwaza athari zitakazotokea. Daktari imlazimishe afanye kazi huku ana ugiligili unaomsonga halafu utegee eti isuue imeisha.... bogus
 
Kuna sehemu JK alisema madaktari walienda kwa maaskofu na kisha wakaenda wote kwa Pinda ......... Kuna mtu anakumbuka kipengele hiki amwage details?
 
tulitaraji hotuba ya kipuuzi kutoka kwa mk...were. Tunamjua. Ila kitaeleweka tu, u dr ni taaluma sana.
hivi madaktari wetu mna akili timamu!!!? Msijione kama nyinyi ndio muhimu kuliko kada nyingine, kumbukeni mkapa aliwatimua jk ndiye akawarudishia tonge leo mnamtenda. Ama kweli fadhila za binadamu mateke. Kazi kupasua vichwa badala ya miguuuu.you are boring......kwavile ni jk ila angekua presidar machachari angewapiga chini mje vijiweni....
 
... mwandishi wa hotuba za rais, hivi kweli hatari hizi haukuziona au umeamua tu kumfanyizia kuendelea kutumia ile ile speech uliomuandikia kutumia siku kadhaa kabla hajakutana na uongozi wa Madaktari??????????

Kwa mtaji wa hotuba ya rais kwa Wazee wa CCM Tandale, naona hali si shwari tena katika hospitali zetu hivi karibuni.

This time madaktari huenda wakaonekana kuhudhuria kama kawaida tu kazini ilimradi tu kutimiza wajibu lakini kiuhakika hakuna kinachoendelea katu!!!
 
hakuna cha kujipanga wafanye kazi basi hawana strategies, kwani mgomo haukufuata hata sheria ndio Attorney General aliomba mahakama ikatoa court injuction ya kuzuia mgomo ina maana madaktari hawajui sheria au walishindwa hata kuuliza sheria inasemaje??
sheria bongo?
 
Bora angeendelea kukaa kimya kama mwanzo.pia unapokubaliana kwamba yameisha hupaswi kuyazungumzia kwa mtazamo hasi,bali utatumia mtazamo chanya bila kuzama kwa kina jinsi mlivyokubaliana.
 
Kwa kuwa hawa watu walishakubali kurudi kazini naona hasingesema tena kuhusu mgomo. Naona kama kalikoroga tena.

kweli hapo kalikologa,kama alishakubaliana na mdaktari kumaliza mgomo hakukuwa na sababu ya kuwaita hao anaowaita wazee dar.walio athilika na mgomo ni watanzania wa rika lote.angekaa kimya kwani alishamaliza.
 
JK anajua sana kuwanafika watu anakinafikia unaona kama mko mae then anakumwaga!! kawamwaga madokta....alikuwa naongea kama vile wale ni watu wasiokuwa na akili kabisa!

Alimlainisha Lowassa kuwa ajiuzulu atamsafisha......akamuita gamba!
Alimlainisha Mwakyembe kuwa ya kusema serikali yote ingeporomoka yameisha kumbe anamsogeza kwenye kona ya kummaliza....Jk ni bingwa wa sanaa hii ya kuchezeana akili!
 
Madaktari hawapimiki kwa kipimo kidogo namna hii.Chamsingi gov wanayokazi.Kama mkuu anavurunda namna hiyo.Kwenye hili madaktari ndio wenye mpini na mwananchi ana makali.Wananchi waliokuwa wanatetewa waweza kupigwa chini nakutafuta haki yao tu.
 
Kuna issue ya ukosefu wa vitendea kazi na madawa kwa ajili ya kuwatibu hasa hao wazee waliokuwa wamejaa ukumbini pale wakipiga makofi hayakuzunguziwa kabisaaaa zaidi ya kuonyesha ubinafsi wa madaktari. Si Mayuwayu ilikuwa hivi hivi baadaye kajutia kauli zakeee?

Pia hii issue ya kila jambo gumu linalohojiwa linasemekana ni Siasa (UCHADEMA) Hii ni issue
 
Back
Top Bottom