bibikuku
JF-Expert Member
- Feb 16, 2011
- 832
- 495
WanaJF
Nimesikiliza kwa kituo hotuba ya JK. Naamini ilikuwa na malengo yafuatayo:
1. Kuwadhalilisha madaktari kuwa hawana uzalendo kwa kudai mishahara isiyowezekana (Sh Milioni 7 na milioni 17 kwa mwezi)
2. Kuwagombanisha madaktari na wananchi ili jamii iwaone kama watu wasiofaa ndani ya jamii.
3. Kuwashuhudia uongo madaktari kwa kueleza na kupotosha historia nzima ya mgomo na kudai watendaji wake akiwemo katibu mkuu waliwajibika ipasavyo. Mfano sakata la interns kudai eti waliondolewa muhimbili kwa sababu kulikuwa kumejaa wakati si kweli, na mengine mengi
4. Kuwageuka madaktari ambao walirejea kazini kwa kuelezea kuwa na imani na Rais baada ya mazungumzo yao, lakini leo amekuja kuwachambua na kuwasemea mbovu mbele ya wananchi na hata kupoteza dhana nzima ya makubaliano yaliyofanyika Ikulu last weekend.
5. Kumshambulia Dr Ulimboka kama alivyomshambulia Mgaya personally mwaka 2010. Hata hivyo ameshindwa kujua kuwa MAT ni chama cha madaktari Tanzania na sio chama cha madaktari wa serikali.
Katika maelezo yake yote hakuna hata sehemu moja ambapo JK ameelezea namna alivyosuluhisha ama atakavyosuluhisha na kutekeleza madai ya madaktari na hasa dai la kuwawajibisha waziri na naibu wake ili mazungumzo yaweze kuendelea baina ya pande mbili zinazoaminiana. Kutokana na hali hiyo, tutarajie yafuatayo muda wowote kuanzia sasa:
1. Madaktari kuitisha mkutano na wanahabari kuelezea uongo ulioshuhudiwa na Rais kuhusu chanzo cha mgomo.
2. Madaktari kuelezea ukweli juu ya makubaliano yaliyofikiwa Ikulu ambayo yalifanya mgomo usitishwe.
3. Madaktari kuelezea kutokuwa na imani na Rais siku mbili baada ya kuongea naye na baada ya kuwageuka na hivyo kuitisha mgomo mkubwa zaidi ya yote iliyotangulia.
4. Na mengineyo meeengi pia......//
Matatizo yote haya chanzo ni hotuba yake ya leo. Madaktari wasilaumiwe kwa hatua yoyote watakayoichukua sababu Rais wetu ameonyesha kutokuwajali wananchi kwa namna yoyote.
Hata hivyo, sitashangaa kama madaktari wakiamua kuchukua uamuzi wa kuudhihirisha uongo wa JK na kisha wakampuuza na kuendelea na majukumu yao.
Nimesikiliza kwa kituo hotuba ya JK. Naamini ilikuwa na malengo yafuatayo:
1. Kuwadhalilisha madaktari kuwa hawana uzalendo kwa kudai mishahara isiyowezekana (Sh Milioni 7 na milioni 17 kwa mwezi)
2. Kuwagombanisha madaktari na wananchi ili jamii iwaone kama watu wasiofaa ndani ya jamii.
3. Kuwashuhudia uongo madaktari kwa kueleza na kupotosha historia nzima ya mgomo na kudai watendaji wake akiwemo katibu mkuu waliwajibika ipasavyo. Mfano sakata la interns kudai eti waliondolewa muhimbili kwa sababu kulikuwa kumejaa wakati si kweli, na mengine mengi
4. Kuwageuka madaktari ambao walirejea kazini kwa kuelezea kuwa na imani na Rais baada ya mazungumzo yao, lakini leo amekuja kuwachambua na kuwasemea mbovu mbele ya wananchi na hata kupoteza dhana nzima ya makubaliano yaliyofanyika Ikulu last weekend.
5. Kumshambulia Dr Ulimboka kama alivyomshambulia Mgaya personally mwaka 2010. Hata hivyo ameshindwa kujua kuwa MAT ni chama cha madaktari Tanzania na sio chama cha madaktari wa serikali.
Katika maelezo yake yote hakuna hata sehemu moja ambapo JK ameelezea namna alivyosuluhisha ama atakavyosuluhisha na kutekeleza madai ya madaktari na hasa dai la kuwawajibisha waziri na naibu wake ili mazungumzo yaweze kuendelea baina ya pande mbili zinazoaminiana. Kutokana na hali hiyo, tutarajie yafuatayo muda wowote kuanzia sasa:
1. Madaktari kuitisha mkutano na wanahabari kuelezea uongo ulioshuhudiwa na Rais kuhusu chanzo cha mgomo.
2. Madaktari kuelezea ukweli juu ya makubaliano yaliyofikiwa Ikulu ambayo yalifanya mgomo usitishwe.
3. Madaktari kuelezea kutokuwa na imani na Rais siku mbili baada ya kuongea naye na baada ya kuwageuka na hivyo kuitisha mgomo mkubwa zaidi ya yote iliyotangulia.
4. Na mengineyo meeengi pia......//
Matatizo yote haya chanzo ni hotuba yake ya leo. Madaktari wasilaumiwe kwa hatua yoyote watakayoichukua sababu Rais wetu ameonyesha kutokuwajali wananchi kwa namna yoyote.
Hata hivyo, sitashangaa kama madaktari wakiamua kuchukua uamuzi wa kuudhihirisha uongo wa JK na kisha wakampuuza na kuendelea na majukumu yao.