Kwa hili Rev.Gamanywa hapana

Kwa hili Rev.Gamanywa hapana

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,170
Reaction score
829,114
Jumamosi mchana nillisikiliza radio Wapo fm inayomilikiwa na Mchungaji Gamanywa wa wa Wapo internatinal

Siku hiyo mchana wote manabii, mitume na wachungaji wanaomiliki makanisa na vituo binafsi vya maombi na maombezi walikuwa wamepanga Foleni redioni wakinadi misa zao za Siku iliyofuata yaani Jumapili.yaani ilikuwa bandika bandua mpaka Usiku

Maneno yao yalifanana woote, Yani ilikuwa ni kama copy n paste, kuwa ibada itakuwa na miujiza ambayo hujawahi kuiona popote, watakaohudhuria wataombewa watoe nuksi,wapate mali,vyeo utajiri nk nk, lakini mwishoni walitaja namba zao za mpesa na tigopesa kwa ajili ya kuchangia huduma

Nikajiuliza mbona Wapo fm inatumika namna hii, lakini nikajua ni biashara hivyo wanapokea matangazo wanalipwa basi life goes on

Jumapili asubuhi kwenye kipindi cha Patapata Mchungaji gamanywa naye akarushwa hewani akaaza kuwaonya wasikilizaji kuwa wawe makini na watu watoao matangazo ya kuvutia watu waende kwenye makanisa yao, akasema wengi ni waongo na hawaaminiki. Kumbuka naye Siku hiyo alikuwa na ibada kwenye kanisa lake hivyo akawa anavutia kwake huku akikandia wenzake

Hii si nzuri; jana yake kachukua pesa ya wenzake, kawarusha hewani wakajinadi, Siku inayofuata kawakejeli huku akijifagilia mwenyewe
Mungu huyu anaona mengi...!
 
na kunatangazo kati ya klaudz au taimufm kuwa atarudisha wafu....
 
Kama maisha yamekushinda jifunze uchungaji,halafu jitahidi uende Mbeya,Congo au Nigeria ukapikwe fresh,ukirudi lazima utoke kimaisha ndani ya mwezi tu.Kama wewe ni msanii na unataka mafanikio ya faster,jipodoe vizuri,rekebisha hips,kisha imba injili.
 
Hao kwa sasa hawaminiki,hukumsikia yule Nabii wa dodoma aliyemmega denti?
 
redio wapo inawapa sana promo manabii wa uongo 1.suguye 2.nabii kijana 3.mtume nyaga 4.ndegi 5.aboubakar 6.dr.livingstone n.k. TUKUMBUKE MANENO YA KULOLA
 
Mimi namwamini Mungu tu mambo ya sijui Gamanywa, Kakobe, Mwingira mara sijui Mzee wa Upako nawaachia wenye akili zao mi na ujinga wangu ntabaki na Mungu wangu tu.. Biblia inanitosha sina mwongozo mwingine.

Wanaojiita ni wachungaji, mitume na manabii wa aina ya Gamanywa, Kakobe, Mwingira, na wengine wote kwa mahubiri yao na kwa matendo yao wanajua wanafanya kazi ya nani na kwa nguvu ya nani. Wanajua kuwa wanalitumia jina kuu la Kristo Yesu kujichumia mali za dunia hii. Wanafanya kufuru kwa udandanyifu wao, watubu kabla kikombe cha ghadhabu ya Mungu hakijafurika maana mahubiri katika mimbari zao sio katika kumwinua Mungu aliye hai, Mungu wa wokovu bali ni kuimua nafsi zao kwa kutumia jina la Yesu kwa hila ya yule mwovu. WATUBU.
 
Kama maisha yamekushinda jifunze uchungaji,halafu jitahidi uende Mbeya,Congo au Nigeria ukapikwe fresh,ukirudi lazima utoke kimaisha ndani ya mwezi tu.Kama wewe ni msanii na unataka mafanikio ya faster,jipodoe vizuri,rekebisha hips,kisha imba injili.

Injili imegeuka kuwa biashara, na makanisa yameteka umma mkubwa wa wakiristo kwa kuamini yanayohubiriwa humo ni KWELI katika kumwinua Kristo. Ukweli ulio kweli ni kwamba wanaasimama kuhubiri wanapewa nguvu hiyo na mwovu shetani ambapo hii ni kufuru kubwa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Kwa muono wangu ambao naamini ni ushuhuda alionijalia Mungu Mwenyezi, zaidi ya asilimia 90 ya wanaoijiita Wachungaji, manabii, mitume, wapakwa mafuta wamepikwa kwa nguvu za giza huko Nigeria, Kongo, Mbeya nk ili kuja kuanzisha makanisa wanayoyaita ya kiroho na ambayo yanawavutia wengi kujiunga. mahubiri yai ni kutafuta mali za hii dunia.
 
Mimi namwamini Mungu tu mambo ya sijui Gamanywa, Kakobe, Mwingira mara sijui Mzee wa Upako nawaachia wenye akili zao mi na ujinga wangu ntabaki na Mungu wangu tu.. Biblia inanitosha sina mwongozo mwingine.
Mkuu, wewe umewaza kama mimi.... nimechoka kwa kweli... naamini MUNGU ni mwaminifu na anaweza kunifanyia mimi kama Neno lake linavyosema...
 
Kutomwamin mtu si dhambi,na usisemee juu ya mtumishi wa mungu kama huna uhakika na unachokisema huyo kakobe unamfahamu maisha yake umfananishe matapeli,hakika mungu hatashuka kumlazimisha mtu kumwamin au laa (yesu), kumbuka mwisho wa maisha yetu tutatoa hesabu kwa kila neno
 
Mimi namwamini Mungu tu mambo ya sijui Gamanywa, Kakobe, Mwingira mara sijui Mzee wa Upako nawaachia wenye akili zao mi na ujinga wangu ntabaki na Mungu wangu tu.. Biblia inanitosha sina mwongozo mwingine.
nakupa 100% me too kaka nitabak na bibilia yangu tu,
 
Hurry up wachungaji pigeni hela before they come to their senses!cc gwajima,mzee wa upako,masanja,kakobe,ndegi,mama lwaks etal
 
Mimi namwamini Mungu tu mambo ya sijui Gamanywa, Kakobe, Mwingira mara sijui Mzee wa Upako nawaachia wenye akili zao mi na ujinga wangu ntabaki na Mungu wangu tu.. Biblia inanitosha sina mwongozo mwingine.

Mkuu Mossad Jaribu basi na kur-an nao ni muongozo mwingine wa Mungu.
 
Jumamosi mchana nillisikiliza radio Wapo fm inayomilikiwa na Mchungaji Gamanywa wa wa Wapo internatinal

Siku hiyo mchana wote manabii, mitume na wachungaji wanaomiliki makanisa na vituo binafsi vya maombi na maombezi walikuwa wamepanga Foleni redioni wakinadi misa zao za Siku iliyofuata yaani Jumapili.yaani ilikuwa bandika bandua mpaka Usiku

Maneno yao yalifanana woote, Yani ilikuwa ni kama copy n paste, kuwa ibada itakuwa na miujiza ambayo hujawahi kuiona popote, watakaohudhuria wataombewa watoe nuksi,wapate mali,vyeo utajiri nk nk, lakini mwishoni walitaja namba zao za mpesa na tigopesa kwa ajili ya kuchangia huduma

Nikajiuliza mbona Wapo fm inatumika namna hii, lakini nikajua ni biashara hivyo wanapokea matangazo wanalipwa basi life goes on

Jumapili asubuhi kwenye kipindi cha Patapata Mchungaji gamanywa naye akarushwa hewani akaaza kuwaonya wasikilizaji kuwa wawe makini na watu watoao matangazo ya kuvutia watu waende kwenye makanisa yao, akasema wengi ni waongo na hawaaminiki. Kumbuka naye Siku hiyo alikuwa na ibada kwenye kanisa lake hivyo akawa anavutia kwake huku akikandia wenzake

Hii si nzuri; jana yake kachukua pesa ya wenzake, kawarusha hewani wakajinadi, Siku inayofuata kawakejeli huku akijifagilia mwenyewe
Mungu huyu anaona mengi...!

Askofu Gamanywa amejibu hii jioni yaleo!""" Very good indeed!
 
Injili imegeuka kuwa biashara, na makanisa yameteka umma mkubwa wa wakiristo kwa kuamini yanayohubiriwa humo ni KWELI katika kumwinua Kristo. Ukweli ulio kweli ni kwamba wanaasimama kuhubiri wanapewa nguvu hiyo na mwovu shetani ambapo hii ni kufuru kubwa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Kwa muono wangu ambao naamini ni ushuhuda alionijalia Mungu Mwenyezi, zaidi ya asilimia 90 ya wanaoijiita Wachungaji, manabii, mitume, wapakwa mafuta wamepikwa kwa nguvu za giza huko Nigeria, Kongo, Mbeya nk ili kuja kuanzisha makanisa wanayoyaita ya kiroho na ambayo yanawavutia wengi kujiunga. mahubiri yai ni kutafuta mali za hii dunia.

Hii ni Kweli tupu isiyo na shaka yoyote ndani yake!
Lakini pia pia mtafute Mungu wake Kweli maadamu anapatikana, nimeona nimeshuhudia. Ukitaka msaada au utumishi wa kweli tuwasiliane
 
Back
Top Bottom