Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Leo, wakati anajibu maswali kutoka kwa wawakilishi wa vituo vya TV, Mgombea urais kwa tiketi ya CCM rais JK, alisema kwamba sababu iliyomsukuma kuwanadi wagombea wa CCM wanaokabiwa na kesi za ufisadi huko mahakamani, kutokana na ukweli kwamba watu hao bado ni watuhumiwa tu, kwakuwa bado hawaja hukumiwa. Pamoja na kukubaliana na kauli yake hiyo, napenda nimkumbushe rais wangu Kikwete, ya kwamba watuhumiwa hao wako mahakamani, kwakuwa serikali anayeiongoza yeye, ilizifanyia uchunguzi tuhuma zinazowakabili watu hao na kuridhika pasipo shaka lolote kuwa wanayo hatia. Ilikuwa ni kutokana na sababu hiyo, ndipo uamuzi wa kuwafikisha mahakamani ukafikiwa. Ikiwa hivi sasa unautilia mashaka uamuzi huo wa serikali unayoiongaza, unataka umma wa watanzania ukueleweje! Wana JF nisaidie kwa hili. Napenda kuwasilisha.