Kwa hili la Mtwara, CCM imenifariji...!

Kwa hili la Mtwara, CCM imenifariji...!

Tunataka vitendo tumechoka na maneno. Atoe muda lini atawaondoa au kuwanyang'anya hao watu/vogogo hivyo viwanda, tumpe miezi mingapi. Acha hadithi za abunuasi. Wewe hujui kwamba kuna pesa huwa zinarudi hazina?
 
safi sana endelea kufarijika 1995 walisema Maisha bora kwa kila mtanzania tena wakasisiteza ajira kwa vijana, vipi umepata? 7yrs ago!
 
you cant go back and make a new start you can start now and make a new end.
 
du ina maana mpaka leo serikali haijui wajibu wake mpaka usukumwe kama gari bovu
 
tunawapa siku 90 wajivue gamba au tutawavua kwa lazima-nape
gamba langu ni gumu halivuki hata kwa shoka,limeishia kiunoni-chenge
till this day wanavuliwa waasisi wa kuvua gamba wakina mukama lakini mafisadi wanaongezewa vyeo..chezea magamba wewe!!!
 
NAFARIJIKA...!


Nimepokea kwa furaha na amani tele ndani ya moyo na akili yangu maagizo yaliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi kwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara na Waziri wa Viwanda na Biashara juu ya kuendelea na kufufua upya viwanda vya korosho Mkoani Mtwara ambapo itasiaidia kupanua soko la zao hilo lakini pia kutoa ajira kwa vijana wa Mtwara.


Pia nimeridhika na kukiri kwa dhati kuwa sasa CCM imeamua kufanya kazi yake na wananchi wanapaswa kuunga mkona juhudi hizi, pale Katibu wa Itikadi na Uenezi Mheshimiwa Nape Moses Nnauye alipotoa maagizo kuwa sasa hakuna tena mtoto kurudishwa nyumbani kwa kukosa ada ama mchango wowote mashuleni. Agizo hili litaondoa usumbufu unaojitokeza na manyanyaso wanayoyapata watoto masikini mashuleni.


Kwa kasi, nguvu na ari hii wapinzani watasubiri sana...!


DAH,,SHUKURU MODERATORS SABABU NAOGOPA :ban:,,

NGOJA TUH NIMALIZE HASIRA ZANGU KWA KUJI :frusty::frusty: NAMNA HII,,,

UMENIHARIBIA SIKU YANGU YOTE..
 
Pamoja na uhuru wa kutoa mawazo, lakini hapa kwa hakika kuna shida ya kuhusianisha. Labda tuulize tu maswali machache ya kuongoza. Hivi ni kweli ccm ilikuwa haijui matatizo ya wakulima wa korosho au yale yanayohusu viwanda vya korosho mpaka anapotembelea katibu mkuu wa chama chao hapo Mtwara?

Kama wanayajua, ilikuwa Kinana na huyo waziri watoke Dar na kwenda kukumbushana hatua za kuchukua kuhusu hivyo viwanda baada ya kufika Mtwara? Kama siyo usanii, hicho ni nini? Tena hawa anaowaita kinana Vigogo waliouziwa viwanda ni akina nani kama si wanaccm wenzao? Wananchi wanahusika nini katika kuwachukulia hatua watu hawa, ikiwa viwanda vyenyewe viliuzwa na hao hao wanaodai leo kwamba wanataka virudishwe?

Mwenzetu umeona matumaini kwasababu mchawi anajitapa kwamba yeye ndiye aliyeua mtoto wako na kwamba sasa atamfufua, wala humuulizi kwanini basi alimuua? Hii ni ajabu. Kweli mtaji wa ccm ni uwezo wetu mdogo wa kuhusianisha mambo na kushindwa kujielewa. Naungana na Mchungaji Msigwa, Problems cannot be solved by the same level of thinking that caused them. Narudi kauli hii na ninatairudi tena.

kudhani kwamba ccm itapambana na ufisadi ni kujidanganya kwani hiyo ni kati ya nguzo muhimu inayoiweka madarakani. Ndugu yangu na jirani wa Nachingwea na wenzangu wa mtwara, mkitegemea ccm hii iwelete maendeleo, mtasubiri sana, kwasababu mtaji wao ni ujinga na umaskini wetu, hawatafanya juhudi hata siku moja itakayofilisi mtaji wao. Kazi kwenu!
 
NAFARIJIKA...!


Nimepokea kwa furaha na amani tele ndani ya moyo na akili yangu maagizo yaliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi kwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara na Waziri wa Viwanda na Biashara juu ya kuendelea na kufufua upya viwanda vya korosho Mkoani Mtwara ambapo itasiaidia kupanua soko la zao hilo lakini pia kutoa ajira kwa vijana wa Mtwara.


Pia nimeridhika na kukiri kwa dhati kuwa sasa CCM imeamua kufanya kazi yake na wananchi wanapaswa kuunga mkona juhudi hizi, pale Katibu wa Itikadi na Uenezi Mheshimiwa Nape Moses Nnauye alipotoa maagizo kuwa sasa hakuna tena mtoto kurudishwa nyumbani kwa kukosa ada ama mchango wowote mashuleni. Agizo hili litaondoa usumbufu unaojitokeza na manyanyaso wanayoyapata watoto masikini mashuleni.


Kwa kasi, nguvu na ari hii wapinzani watasubiri sana...!

Haya yote yalikuwa yanafaywa na watu hao hao, sas ni kitu gani kipya hapo, hivi kama mtu alikuwa kakunyima haki na stahiliyo yako, siku akisema anakupa kelele za nini.... CCM hawawezi kusema wanafunzi wasifukuzwe au wafukuzwe, labda tu kama uwezo wako wa kufikiria na kuchambua ni mdogo ndiyo utashangilia.

Shule zenyewe hazina waalimu sasa wafukuzwe wzsifukuzwe itasaidia nini... Michango ndiyo italipa waalimu wa muda kama hawatatoa micha na serikali haitimizi wajibu wake unafikiri nini kitaendelea?,

Usiwe mvivu wa kufikiria bwana.
 
NAFARIJIKA...!


Nimepokea kwa furaha na amani tele ndani ya moyo na akili yangu maagizo yaliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi kwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara na Waziri wa Viwanda na Biashara juu ya kuendelea na kufufua upya viwanda vya korosho Mkoani Mtwara ambapo itasiaidia kupanua soko la zao hilo lakini pia kutoa ajira kwa vijana wa Mtwara.


Pia nimeridhika na kukiri kwa dhati kuwa sasa CCM imeamua kufanya kazi yake na wananchi wanapaswa kuunga mkona juhudi hizi, pale Katibu wa Itikadi na Uenezi Mheshimiwa Nape Moses Nnauye alipotoa maagizo kuwa sasa hakuna tena mtoto kurudishwa nyumbani kwa kukosa ada ama mchango wowote mashuleni. Agizo hili litaondoa usumbufu unaojitokeza na manyanyaso wanayoyapata watoto masikini mashuleni.


Kwa kasi, nguvu na ari hii wapinzani watasubiri sana...!
1. Mkuu wa mkoa ana bajeti gani ya kufufulia kiwanda cha korosho. Hata reasoning ndogo tu huna?
2. Unajua malalamiko wanayoyatoa walimu wakuu na maheadmaster mashuleni kutokana na kushindwa kuendesha shule zao kwa kuwa serikali haipeleki pesa za kuendeshea shule? Na ada inayolipwa na wanafunzi haitoshi? Unajua kama kuna baadhi ya shule walimu wananunua chaki kwa pesa zao baada ya shule kukosa kabisa hata bajeti ya kununulia chaki?
Yaani kuna wakati ukisoma kauli za CCM unakereka kweli. Kutangaza tu kwamba wasirudishwe nyumbani pasipo kutoa alternative ya namna ya kuendesha shule inasaidia nini?
Kwanza Nape ni nani katika serikali hadi atoe agizo kwa uongozi wa shule? Shule zinaongozwa kwa taratibu zake na si kwa taratibu za CCM. Acheni ujinga bwana.
 
Nilijua kuna kilichofanyika kumbe ni maagizo, hivi maagizo ya JK mangapi yametekelezwa.

Naungana nawe katika kushangaa mkuu, nilizani ni utekelezaji kumbe maagizo tu! tushayazoe.
 
We gamba umetuzalilisha wakulima wa korosho,korosho zinalimwa masasi,tandahimba,newala,nanyumbu na tunduru.hapo mtwara mjini walienda kufanya nini? Nilikuwapo pale jana ni unafiki na kejeli kwa wakulima wa korosho,1200 kwa 600 hii biashara ya wapi? Kwa taarifa yako mkoa huu una vijiwanda vingi tu lakini bado kuna ubabaishaji wa bei,kwa kifupi huu ni mtaji wa vigogo wa ccm.anna abdallah mudhihiri mudhihiri na kundi lao.
 
Zuzu wewe.............idiot
Mimi si mtu wa Mtwara bali ni mtu wa Nachingwea wilaya iliyopo mkoa wa Lindi, lakini matatizo ama kero hizo za Mtwara juu ya korosho hazina tofauti na huku kwetu, lakini si tu kuwa matatizo yetu yanafanana lakini pia aina ya watu wake tunafafa, ninayo haki lakini pia wajibu wa kuyazungumza yale yanayowahusu watu wa kusini, haya ni yetu...!
 
NAFARIJIKA...!


Nimepokea kwa furaha na amani tele ndani ya moyo na akili yangu maagizo yaliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi kwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara na Waziri wa Viwanda na Biashara juu ya kuendelea na kufufua upya viwanda vya korosho Mkoani Mtwara ambapo itasiaidia kupanua soko la zao hilo lakini pia kutoa ajira kwa vijana wa Mtwara.


Pia nimeridhika na kukiri kwa dhati kuwa sasa CCM imeamua kufanya kazi yake na wananchi wanapaswa kuunga mkona juhudi hizi, pale Katibu wa Itikadi na Uenezi Mheshimiwa Nape Moses Nnauye alipotoa maagizo kuwa sasa hakuna tena mtoto kurudishwa nyumbani kwa kukosa ada ama mchango wowote mashuleni. Agizo hili litaondoa usumbufu unaojitokeza na manyanyaso wanayoyapata watoto masikini mashuleni.


Kwa kasi, nguvu na ari hii wapinzani watasubiri sana...!

viwanda vyote walivigawana wenyewe leo wanataka kufufua viwanda vp? wataanzia wapi kuvirudisha toka kwa mafisadi
wenzao? acha tu wale wahindi (olam) waeendelee kupiga pesa nyie mnambwelambwela tu!
 
NAFARIJIKA...!


Nimepokea kwa furaha na amani tele ndani ya moyo na akili yangu maagizo yaliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi kwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara na Waziri wa Viwanda na Biashara juu ya kuendelea na kufufua upya viwanda vya korosho Mkoani Mtwara ambapo itasiaidia kupanua soko la zao hilo lakini pia kutoa ajira kwa vijana wa Mtwara.


Pia nimeridhika na kukiri kwa dhati kuwa sasa CCM imeamua kufanya kazi yake na wananchi wanapaswa kuunga mkona juhudi hizi, pale Katibu wa Itikadi na Uenezi Mheshimiwa Nape Moses Nnauye alipotoa maagizo kuwa sasa hakuna tena mtoto kurudishwa nyumbani kwa kukosa ada ama mchango wowote mashuleni. Agizo hili litaondoa usumbufu unaojitokeza na manyanyaso wanayoyapata watoto masikini mashuleni.


Kwa kasi, nguvu na ari hii wapinzani watasubiri sana...!
Kweli wewe akili yako imechakaa, kama maagizo ya raisi mwenyewe huwa hayaheshimiwi wala kutekelezwa, itakuwa maagizo ya Kinana na mjinga Nape? Vile viwanda vya korosho vilisha uzwa zamani, sasa ni nani wa kuvifufua kama waliovinunua wananufaika kwa kuvifanya maghara?
 
wewe ray jay ni kiongozi gani wa serikali hakuwa pale kwenye mkutano mkuu wa ccm?
kwa nini wasilizungumzie pale?
anampa nani maelekezo?
ni nani aliyeshusha bei ya korosho kutoka1800 hadi 1200?

acha uzuzu mi nilikuwa nafikiri ndani ya ccm kuna mzima hata mmoja kumbe hata nyie wanachama mmeweka akili store?
 
Ray Jay nawewe ushabiki utakuua.....hata kufarijika kwako ni tetesi?
 
Back
Top Bottom