Kwa hili la HESLB wabunge mtutetee

kindikwili

JF-Expert Member
Oct 5, 2016
1,862
2,871
Bodi ya mkopo wa elimu ya juu wana mpango wa kupeleka sheria bungeni itakayotaka kila mnufaika wa mkopo kuanzia 1994 hadi sasa kukatwa 15% ya mshahara wake kulipia mkopo wake.

Lengo lao la kukata 15% ni kuharakisha malipo hayo ili na wengine wanufaike. Sipingi watu kukatwa ila napinga hii 15%, hii ni pesa nyingi sana na vijana tutajikuta tunakata tamaa ya kufanya kazi maana mwisho wa mwezi vijana watakuwa na hali mbaya.

Bodi wajue kuwa hawa wanufaika wanakatwa kodi PAYE, wanakatwa Bima ya Afya, wanakatwa na mifuko ya mafao mfano NSSF, wanakula maeneo ya kazi, wana familia zinawategemea, wamepanga nyumba, wanalipa maji na umeme. Jumla ya makato halali tu yanakaribia kufika 35% kwa sasa, kama HESLB watakata 15% huenda jumla ya makato yakafika 50% ya mshahara wa hawa wadaiwa.

Naomba kwa hili wabunge watuonee huruma bila kujali vyama vyao au kama nao wanadaiwa au lah. Walau iwe hata 10% ili jumla ya makato yawe chini kidogo, wajue pamoja na kukopwa bado sisi wachache tuliobahatika kupata ajira ni walipaji wa kodi waaminifu. Nashauri bunge liwape HESLB mbinu nyingine ya kuongeza mapato kama kusaka wadaiwa wengine na si kuwanyonga hawa vijana ambao tayari wameshajitokeza.

USHAURI wangu ni kwamba kwa wale ambao tulikopeshwa na hatujaanza kulipa tujipeleke wenyewe tuanze kulipa ili walipaji wawe wengi huenda ikazuia haya makato makubwa yanayopendekezwa.
 
Bodi ya mkopo wa elimu ya juu wana mpango wa kupeleka sheria bungeni itakayotaka kila mnufaika wa mkopo kuanzia 1994 hadi sasa kukatwa 15% ya mshahara wake kulipia mkopo wake. Lengo lao la kukata 15% ni kuharakisha malipo hayo ili na wengine wanufaike. Sipingi watu kukatwa ila napinga hii 15%, hii ni pesa nyingi sana na vijana tutajikuta tunakata tamaa ya kufanya kazi maana mwisho wa mwezi vijana watakuwa na hali mbaya.

Bodi wajue kuwa hawa wanufaika wanakatwa kodi PAYE, wanakatwa Bima ya Afya, wanakatwa na mifuko ya mafao mfano NSSF, wanakula maeneo ya kazi, wana familia zinawategemea, wamepanga nyumba, wanalipa maji na umeme. Jumla ya makato halali tu yanakaribia kufika
35% kwa sasa, kama HESLB watakata 15% huenda jumla ya makato yakafika 50% ya mshahara wa hawa wadaiwa.

Naomba kwa hili wabunge watuonee huruma bila kujali vyama vyao au kama nao wanadaiwa au lah. Walau iwe hata 10% ili jumla ya makato yawe chini kidogo, wajue pamoja na kukopwa bado sisi wachache tuliobahatika kupata ajira ni walipaji wa kodi waaminifu. Nashauri bunge liwape HESLB mbinu nyingine ya kuongeza mapato kama kusaka wadaiwa wengine na si kuwanyonga hawa vijana ambao tayari wameshajitokeza.
USHAURI wangu ni kwamba kwa wale ambao tulikopeshwa na hatujaanza kulipa tujipeleke wenyewe tuanze kulipa ili walipaji wawe wengi huenda ikazuia haya makato makubwa yanayopendekezwa.
Akutetee nani, akina Livingston Lusunde,Maji Marefu au nani?
 
Naunga mkono hoja, watu wengi tayari wana mikopo lukuki kwenye salary slip zao alafu uongeze makato tena?
 
Hali ni mbaya tuendelee kumwomba Mungu ipo siku watawala wetu watatambua kuwa wanaongoza masikini maana wengi wao wameshiba na kusahau wanyonge
 
Nimepiga hesabu hapa wakiniongezea na hiyo makato yatafika kama 60% ya salary huo moyo wa kufanya kazi nitautoa wapi na mwisho wa mwezi napata hela isiyotosha hata chakula.
8% wanayokata inatosha wakiongeza huko ni kuhitaji tuwe na umasikini unaopindukia sasa.
Wabunge wetu chondechonde hili muwaeleze HESLB sisi wadaiwa tunaolipa mkopo wao kwa 8% tusingependa kufika mahali kuichukia serikali kwa kiwango hicho.
 
Akutetee nani, akina Livingston Lusunde,Maji Marefu au nani?
Aisee kaka kama kweli ulipata mkopo wa Bodi unajua ninachokisema hapa, hali ni mbaya kuliko kawaida. Hebu piga picha ya familia zetu hizi ambazo msomi ni wewe pekee yako, wazazi waliuza ng'ombe,mbuzi na mashamba kwa ajili yako. Leo umepata kazi unakatwa zaidi ya 50% ya mshahara wako huku nyumbani ushapewa wadogo zako 2 uwasomeshe, mjini huku umepanga na unalipia hadi pa kutunza haja ndogo. Mimi naona magonjwa ya akili, watu kuongea wenyewe njiani kama machizi na msongo wa mawzo huenda ukatumaliza vijana tuliokopshwa na bodi.
 
Si ndio hapo.. amtetee nani?huyu wa maono, hawa vgeugeu na wanafik wasiojal shida za wenzio?
Nisingependa hapa tuweke hisia za ushabiki wa vyama jamani, hii issue itaumiza watoto wa masikini Tanzania nzima bila kujali vyama vyao wala vya wazazi wao. Tusiwabeze hawa wabunge hata kama hatuwapendi bali tuwaelimishe huenda wakatuelewa na kutupigania.
 
Aisee kaka kama kweli ulipata mkopo wa Bodi unajua ninachokisema hapa, hali ni mbaya kuliko kawaida. Hebu piga picha ya familia zetu hizi ambazo msomi ni wewe pekee yako, wazazi waliuza ng'ombe,mbuzi na mashamba kwa ajili yako. Leo umepata kazi unakatwa zaidi ya 50% ya mshahara wako huku nyumbani ushapewa wadogo zako 2 uwasomeshe, mjini huku umepanga na unalipia hadi pa kutunza haja ndogo. Mimi naona magonjwa ya akili, watu kuongea wenyewe njiani kama machizi na msongo wa mawzo huenda ukatumaliza vijana tuliokopshwa na bodi.
Siyo kwamba hajakuelewa. Anachomaanisha ni kwamba huko bungeni unakoelekeza maombi yako hakuna watetezi. Serikali ikipeleka mapendekezo huko ujue yamepita tu. Jiandae kufunga tu mkanda.
 
Hawa Wabunge wanafiki ambao wanachukua rushwa ya milioni 10 ili wapitishe muswada uchwara, sijui kama watakuwa na msaada wowote kwenu. Kwa kweli huweza kumkata mfanyakazi makato ya asilimia kubwa kiasi hiki mpaka ashindwe hata kumudha gharama zake za kila siku za maisha. Hii si sawa hata kidogo lakini hakuna atakayejali vilio vyenu. Poleni sana.

Bodi ya mkopo wa elimu ya juu wana mpango wa kupeleka sheria bungeni itakayotaka kila mnufaika wa mkopo kuanzia 1994 hadi sasa kukatwa 15% ya mshahara wake kulipia mkopo wake. Lengo lao la kukata 15% ni kuharakisha malipo hayo ili na wengine wanufaike. Sipingi watu kukatwa ila napinga hii 15%, hii ni pesa nyingi sana na vijana tutajikuta tunakata tamaa ya kufanya kazi maana mwisho wa mwezi vijana watakuwa na hali mbaya.

Bodi wajue kuwa hawa wanufaika wanakatwa kodi PAYE, wanakatwa Bima ya Afya, wanakatwa na mifuko ya mafao mfano NSSF, wanakula maeneo ya kazi, wana familia zinawategemea, wamepanga nyumba, wanalipa maji na umeme. Jumla ya makato halali tu yanakaribia kufika
35% kwa sasa, kama HESLB watakata 15% huenda jumla ya makato yakafika 50% ya mshahara wa hawa wadaiwa.

Naomba kwa hili wabunge watuonee huruma bila kujali vyama vyao au kama nao wanadaiwa au lah. Walau iwe hata 10% ili jumla ya makato yawe chini kidogo, wajue pamoja na kukopwa bado sisi wachache tuliobahatika kupata ajira ni walipaji wa kodi waaminifu. Nashauri bunge liwape HESLB mbinu nyingine ya kuongeza mapato kama kusaka wadaiwa wengine na si kuwanyonga hawa vijana ambao tayari wameshajitokeza.
USHAURI wangu ni kwamba kwa wale ambao tulikopeshwa na hatujaanza kulipa tujipeleke wenyewe tuanze kulipa ili walipaji wawe wengi huenda ikazuia haya makato makubwa yanayopendekezwa.
 
Kama Mtumishi aliyeajiriwa ana utitiri wa makato yote haya kwenye mshahara wake.
PAYE---------- 18%
HESLB---------15%
PENSION--------6%
NHIF------------4%
WORKER UNION---2%

Jumla ASILIMIA 45.

*Hapo hatujajumuisha makato mengine mengi sana ambayo wafanyakazi wengi hukatwa kwenye mishahara yao kama Mchango wa Mbio za Mwenge, Usalama kazini, Mkopo wa Benki nk.
Na hapo hapo hakuna Posho, hakuna marupurupu, hakuna kupandishwa cheo na wala hakuna nyongeza ya mshahara.

Kwa style hiyo najaribu kujiuliza haya..

1/Moyo wa kuendelea kufanya kazi kwa bidii utatokea wapi?

2/Uaminifu katika maeneo ya kazi utatokea wapi?

3/Uwezo wa kuendelea kuishi unatokea wapi?

4/Amani na Furaha vinatokea wapi?

5/Uzalendo kwa nchi yako utatokea wapi?
 
mwenye shibe hamjui mwenye njaa. hivi Tanzania tuna bunge? ule ni mkusanyiko wa wapumbav.u waliochaguliwa na wananchi masikini, wajinga na washirikina ili tu kujaza hizo nafasi. wengi wao hawana upeo wowote, ni mbumbumbu wa kutupwa wanao tumikia chama na serikali yao tukufu inayo ongozwa na mtu asiye na upeo wowote wala utu. ukweli ni kwamba baadhi ya binadamu duniani tulizakiwa kwenye nchi masikini sana, inasikitisha kujua kwamba watoto wetu na watoto wao wataishi kwenye dhiki ile ile. ni kama laana tu. manina!!!
 
15% Itafanya watu watoroke kazini kwenda kutafuta vibarua.Hivi taarifa za watumishi si ziko halmashauri?kwanini wasichukue hizo data na kukata kwa utaratibu uliokuwepo.kwa sekta ya elimu naona inaenda kuzima maana 70% ya wadaiwa huko ni watoto wa maskini ambao hata leo posho zao za mwezi wameshagawana na ndugu zao.Ukimwambia alipe hata 10000 hana.Bunge lisimame kama bunge sasa.
 
Muliambiwa ni ile ile mkakubar yamewafika shingon mnaomba msaada hapo mnataka wabunge wa upinzani waendelee kipaza sauti na kukamatwa bila kuwapa support ata ya walau kuandamana..daaaah
 
Muliambiwa ni ile ile mkakubar yamewafika shingon mnaomba msaada hapo mnataka wabunge wa upinzani waendelee kipaza sauti na kukamatwa bila kuwapa support ata ya walau kuandamana..daaaah

Kaka ucha ukada kwenye mambo muhimu yanayotugusa sote, hakuna aliyesema wabunge wa upinzani tu ndiyo watutetee bali bunge zima. Hii habari ina athari kwa kila familia ya mtanzania masikini awe wa CCM au Upinzani.
 
Kama Mtumishi aliyeajiriwa ana utitiri wa makato yote haya kwenye mshahara wake.
PAYE---------- 18%
HESLB---------15%
PENSION--------6%
NHIF------------4%
WORKER UNION---2%

Jumla ASILIMIA 45.

*Hapo hatujajumuisha makato mengine mengi sana ambayo wafanyakazi wengi hukatwa kwenye mishahara yao kama Mchango wa Mbio za Mwenge, Usalama kazini, Mkopo wa Benki nk.
Na hapo hapo hakuna Posho, hakuna marupurupu, hakuna kupandishwa cheo na wala hakuna nyongeza ya mshahara.

Kwa style hiyo najaribu kujiuliza haya..

1/Moyo wa kuendelea kufanya kazi kwa bidii utatokea wapi?

2/Uaminifu katika maeneo ya kazi utatokea wapi?

3/Uwezo wa kuendelea kuishi unatokea wapi?

4/Amani na Furaha vinatokea wapi?

5/Uzalendo kwa nchi yako utatokea wapi?

Mkuu mbona PAYE inazidi hapo na hata hii mifuko wanakata 10% kwa 10% au 5% kwa 15% ya mshahara hiyo 6% ni mfuko gani? Japo kwa PAYE inategemea na mshahara wa mtu ila inazidi sana hapo. Hapo hujakatwa na Tanesco, Dawasco, Mwenye nyumba, Wazazi, Wakwe, Watoto, Wenye daladala na tumbo, usiwasahau na wadogo zako unaowalipia ada.
 
Back
Top Bottom