Kwa hili la Bandari nipo 'Neutral' kwa mtazamo ufuatao

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,725
109,157
Mtazamo Chanya...

1. Bandari itaboreshwa
2. Ufanisi Kuongezeka
3. Biashara Kuimarika
4. Maslahi juu kwa Wafanyakazi
5. Huduma yao itavutia nchi nyingi Jirani
6. Mapato Kuongezeka
7. Urasimu Kupungua

Mtazamo Hasi
1. Mkataba kutokuwa na Ukomo ni Hatari kwa wenye Bandari

2. Vipengele vinachojichanganya Kimaelezo vinaleta Wasiwasi

3. Kwanini hakukuwa na Mchakato mrefu unaohusisha hata Wananchi ili Kuuelewa?

4. Msemaji wa Serikali badala ya Kuelezea Kiundani muda mwingi anautumia Kufoka. Kukosoa na kutuonyesha Watanzania kuwa hana Akili

5. Tunatulizwa kuwa DP World wako hadi Uingereza ila hatuambiwi kwanini katika Mataifa mengine Wameshindwa

6. Wanasiasa kuingilia Kutetea Mpango huu kunaongeza Shaka kuwa huenda tatizo halipo tu katika Mkataba na DP World bali hata Akili za Wanasiasa Wetu ( hasa Wabunge wa CCM ) nazo zina tatizo

7. Spika wa Bunge kutumia muda mwingi Kuvitishia Vyombo vya Habari vya Tanzania juu ya Kuandika kuhusu huu Mkataba wa DP World na Bandari yetu kunaonyesha kuwa huenda Mihimili Mikubwa miwili imeshalainishwa Kifedha na Waarabu ili Kuuza Rasilimali za Watanzania na Watanzania wenyewe

Nini Kifanyike?
1. Mchakato juu ya huu Mkataba uanze upya na uhusishe Watanzania Wote

2. Lugha ya huu Mkataba iwe ya Kiswahili ili hata tusiojua Kiingereza akina GENTAMYCINE tuuelewe

3. Watanzania tuwe Wavumilivu juu ya Ufadanuzi utakaolewa

4. Wanasiasa na Wabunge wasiwe Wasemaji Wakuu wa hili bali Wataalam wasio na upande ndiyo Wasikilizwe

5. Rais, Waziri na Msemaji wa Serikali wasione Aibu kuwaomba Radhi Watanzania juu ya hii Sintofahamu inayoelekea kuzaa Chuki na Hasira kwa Wadau na Wananchi

6. Tubakie na Utanzania Wetu na kamwe tusianze Kubaguana Kimakabila na Kijiografia kwani Sisi sote ni Watanzania

7. Wale Wanaotetea huu Mkataba wa DP World wasionekane ni Maadui kwani nao wana Hoja mahala lakini pia na wale ambao Wanaukosoa huu Mkataba wasipuuzwe, wasidharauliwe bali Hoja zao nazo zipimwe kisha kwa upamoja Wao kupatikane muafaka thabiti ya huu Uwekezaji wa hawa DP World kama Wawekeze au Wasiwekeze.

Mungu Ibariki Afrika
Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Ubariki Mtandao huu wa JamiiForums
Mungu Mbariki mno GENTAMYCINE

AMINA.
 
Tunaitaji mkatab wenye uwazi na ukweli,tunaleta wawekezaji hatuwauzii huu ni urithi wetu na watoto wetu na vizazi vijavyo, kama tutauza bandari basi vizazi vijavyo vitatusoma kama jamii ama kizazi kisichokuwa na akili katika uso wa Tanzania.

Tusisahau tunamsoma chifu mangungo kama chief asiye na akili na dhaifu,

Tunamsoma mkwawa kama shujaa aliye ipambania jamii yake ikibidi kufa ,Tuchaguwe moja tuwe mashujaa ama jamii ya kijinga kwa sababu ya watu wachache,tunataka mkatab wenye kikomo, mkataba unalenga kutoka fursa za Ajira ,mkataba wenye uwazi pia hatuuzi bandari,mkataba usio na kikomo ni mauziano ya bandari
 
Tunawaazima kwa muda,ili tujipange tukishindwa sisi watoto wetu wajipange,ama wajukuu ama vizazi vijavyo...
Mikataba Mungu nyerere hakuwa anaipitisha kwa kutuangalia sisi, basi na sisi tukiwa tunaangalia vitamin vyetu tukumbuke watoto wetu wataishi hapa ,wajukuu zetu wataishi hapa na vizazi vyetu hapa ndo kwao😥.

Tusitangulize vitamin ,tukiuza bandari tutakuwa tunamega nchi yetu watoto wetu watajua pale ni uarabuni na siyo Tanzania
 
Kusema ukweli mimi sijui kama mkataba ni mbaya ama mzuri lakini nahitaji kuekeweshwa zaidi kwani nimeingia shaka baada ya kuona jinsi watu wanavyolalama.

Mbunge anatumwa na wananchi kutusemea lakini inaoneka kwasasa kama mbuge anaweza kutoa maamuzi hata kama mwananchi hajaridhia, hii nalo linanipa shaka.

Kwanini wanasiasa wanatetea sana badala ya kutupa ufafanuzi wa mkataba tena kwa lugha nyepesi ili sisi wananchi ndiyo tuamue badala ya kututaka tukubali bila hata kuelewa.
 
Sawa kabisa, ila mkataba ni siri na hao wanaofanya makubaliano tuwaamini kwani haiwezekani wote tukaujua
Wawakilishi tunaowaamini ni bora

Hakuna kubezana bali wote tuwe wamoja kwa maslahi ya Taifa
Tusilie lie kisa tunashindwa kila kitu bali lazima tukubali mapungufu yetu

Tuache wizi
Hivi umeona wapi tapeli akaaminika?
Kama tunao viongozi matapeli kwanini tuwape kura? Piga chini hao ila na nyie tatizo moja tu mnauza utu wenu kwa thamani ndogo sana

Mali ni nini mbele ya maslahi mapana ya Taifa?
 
Utakosaje msimamo katika suala nyeti namna hii?

Ngoja nikusaidie kukutafutia msimamo kulingana na hoja zako nzuri zenye mizania ya merits and demerits, msimamo ni kwamba mpango wote kuhusu kubinafsisha bandari zetu umejaa mashaka na mizengwe hivyo usitishwe na uuanzwe upya kwa uwazi, and that is for the benefit of doubts.
 
Back
Top Bottom