Kwa dalili hizi, hakuna Katiba Mpya!

Kwa dalili hizi, hakuna Katiba Mpya!

Kwa siku za hivi karibuni wote tumeshuhudia ccm wanavyohujumu mchakato wa kupata Katiba ya Tanzania kwa Watanzania. Ni jambo la ajabu kwa asieelewa pale wapinzani walivyo anza kulalamika kuanzia mchakato wa awali wa kupata katiba mpya ulivyoonesha ccm watakuwa na wajumbe wengi kuliko taasisi na vyama vingine vya upinzani kwamba kunahatarisha na kunaweza kupatikana katiba ya ccm ni si ya wananchi. Jambo ambalo kwa sasa ndilo linalojidhihirisha na hata pale walivyolalamika kuhusu kanuni kuvunjwa na kuanza kwa Jaji Warioba kuwakilisha rasimu ya pili ya katiba kabla ya rais kufungua bunge la katiba kuna ambao walisema wana wasiwasi tu, lakini ndilo lililotokea matokeo yake rais alienda kupiga kampeni ya serikali mbili na kuligawa bunge na kujibu hotuba ya Jaji Warioba na kwenda mbali zaidi kwa kuwadhalilisha tume ya katiba ingawa maoni hayakuwa ya kwao bali ni ya wananchi. Na sasa kuna la kura ya siri na ya wazi, wote tunajua wajumbe wengi ni wa chama cha ccm ambao wameshaelezwa hawatakubaliana na rasimu ya pili ya katiba, na wanajua kuwa kuna wabunge wengi wa ccm ambao wanaweza kupiga kura kinyume na misimamo ya chama cha ccm ndio maana wanawashinikiza kupiga kura ya wazi ili waiteke demokrasia ya wajumbe. Jambo hili halikubaliki ni bora ccm waachwe watengeneze katiba yao badala ya kutuvurugia mchakato na kuharibu fedha za wananchi kwa kulazimisha wanayotaka wao. Ni bora wajumbe wote wasiokubaliana na hili ikibidi waufahamishe umma wa watanzania ili tutoke kama taifa na kupinga jambo hili ovu. Huu mchakato umetumia fedha nyingi sana za wananchi hatutakubali kuacha itikadi za kichama kuingilia mchakato huu.
 
Hayo wanayoyafanya yana mwisho, na mwisho wenyewe umekaribia. Jambo ambalo lingebaki likinishangaza ni iwapo wasingelitapatapa kama wafanyavyo sasa. CCM ingali na nafasi ya kubaki inaheshimika hata kisipokuwapo madarakani, lakini kikiendelea kama kinavyofanya sasa hata kitaishia kwenye "kaburi la sahau" kama KANU, UNIP, na wengineo kama hao. Ni vema CCM kutambua kuwa Katiba Mpya sio HISANI au suala linalotegemea KUDURA zao, bali ni suala la HAKI YA WATANZANIA WOTE. Wakumbuke hilo kwa kuwa "ipo siku". Zile nyakati za watu kulazimishwa kufikiri na kuishi kama jana zimepita, Watanzania wanataka kuiishi leo yao na leo hiyo ni leo.
 
Ugali mtam jamani waulizeni wenzenu wa Libya.
 
Nasikitika kwamba wajumbe wameingiza kampeni za vyama kwenye suala nyeti Kama hili! what a shame to my country!
 
Hili bunge linatutia aibu jamani nafikiri ni bunge la ratiba wanakamilisha ratiba then wapewe chao wasepe ni vurugu,matusi,vijembe kama kirabu cha pombe this is BS
 
watu wameingiza siasa kwenye jambo la msingi. alafu kuna kula gani inayopigwa kwa uwazi?
 
Ee Mungu okoa kodi zetu zinateketea dodoma :violin:acha nikung'ute gitaa kupunguza mawazo
 
kama sio masikini walienda kufanya nini kwa hao mawaziri.
 
Nasikiliza bunge la katiba live. Eh hiyo fujo inayoendelea utafikiri watoto wadogo!!! Hii rasimu ya katiba itapatikana kweli?
 
Back
Top Bottom