Kwa dalili hizi, hakuna Katiba Mpya!

Kwa dalili hizi, hakuna Katiba Mpya!

Mkuu, umenena vyema, hebu tuwekee viashiria vya kupata katiba ya kichama kama ulivyosema ili na wengine tuelimike zaidi ama kujifunza hatimaye kufumua uozo wote na kurudi kwenye njia sahihi kuelekea katiba ya taifa.

Suppose CUF wangekuwa majority kwenye hilo Bunge tusingekuwa na Katiba ya ki-CUF?
 
Suppose CUF wangekuwa majority kwenye hilo Bunge tusingekuwa na Katiba ya ki-CUF?

Nadhani swali hili litajibiwa vizuri na kill kwa kua ni yeye kadokeza dhana ya uchama.
 
Last edited by a moderator:
Okay umesomeka! Je, unafikiri ni kitu gani kinakwamisha mchakato wa Katiba?

Katika hali inayoendelea bungeni, ni wazi kua misimamo ya kisiasa/kichama ndiyo kikwazo kikubwa ktk mchakato huu.
 
CLOUDSTV:Mwenyekiti wa bunge la katiba Samwel Sitta amekiri kufadhaishwa na vurugu vinazofanywa na wabunge wa UKAWA na kusababisha bunge kuahirishwa kila mara!!
 
Mkuu itapatikana tu lkn je ni katiba tutakayoridhika nayo, hapa ndipo penye mjadala.
 
Manyani hayajioni makalio. Mnawasema wajumbe wamegawanyika kimakundi. na nyie jf hamjagawanyika kweli?
Hebu angalieni jinsi kila upande unavyovutia kwake.Huku Bucha kule Sky.
 
Wanakula posho ya bure! Sijui hiyo dhambi watatubia wapi kwa kuwa Wananchi hawatawasamehe! Leo siku ya 39 na hawajaanza kujadili hata ibara moja. Wamekula kila mmoja 300,000 mara siku 39. Wanabishania eti kura zisiwe za siri ziwe za wazi! Bahati mbaya siwezi kutukana lakini..wanatufanya wote ni wajinga!
 
je kinachotokea ni ujenzi wa mnara babeli ? kosa kubwa hii ni hatua ya juu. Tumeruka hatua ya msingi. Nguzo za katiba ni nini ? Haya yangeamuliwa kwanza hata kabla tume haijasonga mbele kwa rasimu ya pili. Turudi kwenye hatua tulioruka. Bunge lisitishwe twende kwenye kura ya maoni tunataka muundo gani wa nchi yetu.
TUNATAKA MUUNDO WA SERIKAL 3,soma rasim ya katiba hapa www.katiba.go.tz,usikulupuke,
 
Nasikiliza bunge la katiba live. Eh hiyo fujo inayoendelea utafikiri watoto wadogo!!! Hii rasimu ya katiba itapatikana kweli?

Tunachokiona hapo ni true reflection ya jamii ya Kitanzania ilivyo sasa. Ni ishara tosha za failed state, wenye macho na akili timamu uwezi ambiwa tazama.

Kwenye nchi zenye malengo na kujitambua, bunge ni chombo chenye hadhi na heshima kubwa lakini siyo Tanzania. Bunge la Tanzania huwezi hata kulifananisha na masoko ya nyanya sababu utakuwa umelipa hadhi. Bunge kwa Tanzania limekuwa kama tamasha linalowakutanisha wawakilishi kutoka mikoa mbalimbali kuja kusutana.


Wajumbe kwenye mabunge yenye hadhi huwa wanajadili ideas lakini Tanzania ni maneno ya khanga kutwa nzima sababu ndipo uwezo wetu wa kufikiri ulifikia. Na tunaona ni ufahali sana mtu kuongea maneno mengi yasio hata utafiti ndani yake.


Huko tuendako Mungu ndiye anayejua na hatutafanikiwa mpaka vijana wa taifa ili waitambue nafasi yao kwenye taifa hili ndipo tutaendelea la sivyo badala ya kwenda mbele tunajirudisha nyuma.


President of Uganda normally says " African we wont move forwards because most of the time we compare ourselves, who's tall than the others. There is no wisdom of two pygmies arguing at who is inch taller than others whilst at the end of the day they are all pygmies"
 
Tatizo limeletwa na ccm toka mwanzo wa mchakato wa katiba, sheriailikuwa mbovu kutokana na wingi wa wabunge wa ccm kwani walilazisha rais awe juu ya katiba. Na kitendo cha kujaza wanasiasa kwenye BMK ndio haya tunayoyaona. Na hapo ni bado kwani huo ni mwanzo tu huko mbeleni dhamira ovu ndio itazidi kidhihiri. Mpaka wajumbe 201 nao wanahongwa!!?
 
Tanzania imeingia gharama kubwa hadi sasa kwa kutumia vibaya kodi za wananchi kwa jina la katiba mpya wakati hadi sasa hakieleweki. naomba nitumie nafasi hii kuwaakumbusha pia wananchi kama haturidhiki na mwenendo wa bunge la katiba tunayo haki pia ya kupiga kura na maoni ya kutoridhika na kutokukubaliana na mwenendo mzima wa bunge la katiba
 
Kwa hali ilivyo ni dhahiri kuwa hakuna katiba mpya ya watanzania.



Ukawa ni nani hasa katika nchi hii. Ccm ni nani katika nchi hii. Katiba tunayoitaka si kwa ajili ya wanachama mil.3 wa ccm au mil. 3.5 wa ukawa. Hata wakiungana hawawezi kufika mil. 20 ambayo ni nusu ya watanzania. Tunataka katiba ya watanzania zaidi ya mil. 45 na si ya 0.0 ya wanasiasa.

Nasema hivyo sababu katika hali ya kushangaza sasa hivi ni majibizano kati ya vyama vya siasa na siyo wahusika wenyewe.
Hivi palikuwa na umuhimu gani kujaza wanasiasa katika kuandaa katiba? Asilimia kubwa ya wajumbe ambao ni wanasiasi ni vilaza (hawana uelewa wa sheria) hata kama ukawa wakirudi bado katiba kwa asilimia kubwa itakuwa ni kwa manufaa ya wanasiasa na siyo wananchi.

Wanasiasa wanachoangalia ni maslahi yao pamoja na familia zao. Ikiwezekana blk livunjwe halafu wateuliwe wajumbe wenye kujielewa siyo hawa vinyonga.

Asasi za kisheria wao wako wapi kama siyo vinyonga na bendera fata upepo? Kwa nini kweli kama wamekwenda kuwawakilisha wananchi wasiweke msisitizo wao? Asasi za kidini nazo kwa nini wamekubali wanasiasa kuwa wamiliki wa kuandaa katiba?

Mmepelekwa hapo si kuandaa katiba za vyama vya siasa! Wekeni siasa na uhasimu wa vyama pembeni, bila kufanya hivyo hakuna tokeo lolote bora litakalotokea.

Ni heri kuteua jopo la wanasheria tupu kuliko kutumia wanasiasa katika kuandaa katiba ya taifa letu.

Ccm na ukawa wekeni masilahi yenu ya vyama pembeni na muandae katiba itakayo wasaidia hata wazazi wenu. Wengi wenu ndugu zenu ni hohe hahe kutokana na mfumo wa katiba ya sasa. Hatutaki kujua nani muongeaji au ana mdomo zaidi ya wenzake. Muda hausimami. Kama mmeshindwa hiyo kazi acheni wananchi wajue mmeshindwa.
 
Ccm wanajua kabisa bila ushiriki wa vyama vikuu vya siasa hakuna katiba mpya,hata kama wakienda wao wakafanikisha hyo katiba mpya,italalamikiwa siku ya kwanza tu na ndiyo itakayotuingiza katika machafuko,kikubwa chama tawala waache uroho na ubinafisi,washirikiana na vyama vyote kuleta usawa

Wazanzibar waje kama wazinzibar na sio cuf na ccm na upande wa Tanganyika waje kama Tanganyika na sio ukawa na Tanzania kwanza,from there tunaweza enda kama Taifa moja na lugha za kejeri zikatoweka na kila Nchi ikadai masirahi yake kwa uwazi na sio kwa hisani kama ilivyo sasa

Tarehe5 bunge la katiba linaanza bila vyama vikuu 3 kuwepo ambao ni wadau wakubwa wa katiba hii na wao wameidai kwa miaka 25 ila wale waliopo ndani katiba hii haina faida kwao wala hasara,nways ngoja tuone akili zao zimeishia wapi kwa hili swala la Kitaifa na sio kichama
 
Ccm wanajua kabisa bila ushiriki wa vyama vikuu vya siasa hakuna katiba mpya,hata kama wakienda wao wakafanikisha hyo katiba mpya,italalamikiwa siku ya kwanza tu na ndiyo itakayotuingiza katika machafuko,kikubwa chama tawala waache uroho na ubinafisi,washirikiana na vyama vyote kuleta usawa

Wazanzibar waje kama wazinzibar na sio cuf na ccm na upande wa Tanganyika waje kama Tanganyika na sio ukawa na Tanzania kwanza,from there tunaweza enda kama Taifa moja na lugha za kejeri zikatoweka na kila Nchi ikadai masirahi yake kwa uwazi na sio kwa hisani kama ilivyo sasa

Tarehe5 bunge la katiba linaanza bila vyama vikuu 3 kuwepo ambao ni wadau wakubwa wa katiba hii na wao wameidai kwa miaka 25 ila wale waliopo ndani katiba hii haina faida kwao wala hasara,nways ngoja tuone akili zao zimeishia wapi kwa hili swala la Kitaifa na sio kichama

ubabe wa vyama wakaonyeshane kwenye majukwaa ya siasa. Bila katiba bora hakuna maisha mazuri na yenye amani kwa wananchi.
 
Kama ni kweli yanayosemwa leo juu ya ccm. Hapo ndipo pale ninapozidi kuamini kama prof. Mpangala alivyobainisha kuwa, katika changamoto tuliyoyafanya ni kuweka wanasiasa wengi kutuletea katiba bora. Lengo hasa la ccm ni kumobilize wananchi ili ijulikane kuwa wananchi wengine wanapenda vile ambavyo ccm wanafanya. This is too bad to our side.
 
Hakuna katibapya CCM wataka kupitisha katiba ya chama chao il I waendelee kututesa kwa miaka 50 mingine ole we nu wapenda maendeleo mtaendelea kuwapa maisha mazuri kina ridhiwani
 
Kama ni kweli yanayosemwa leo juu ya ccm. Hapo ndipo pale ninapozidi kuamini kama prof. Mpangala alivyobainisha kuwa, katika changamoto tuliyoyafanya ni kuweka wanasiasa wengi kutuletea katiba bora. Lengo hasa la ccm ni kumobilize wananchi ili ijulikane kuwa wananchi wengine wanapenda vile ambavyo ccm wanafanya. This is too bad to our side.

Panatia kinyaa sana kwa kweli: pale uliposema " Lengo la .......ni.......! Ni shida sana mdau wangu yaani wanasiasa na wapambe wao ambao hata million 10 hawafiki wanapoka mambo yote! Kwa kweli, moja ya kosa kubwa ni Wabunge wote wa BJMTZ na Wawakilishi wote wa BMZ kuwa woote ni wajumbe, ni kosa ambalo linatakiwa liwekwe kwenye wikipedia ili vizaz vijavyo wasirudie kosa hili!
 
Back
Top Bottom