Kwa Baregu si sawa ila kwa Migiro ni sawa?

Kwa Baregu si sawa ila kwa Migiro ni sawa?

Parata

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2011
Posts
3,090
Reaction score
692
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dkt. Asha Rose Migiro kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Mheshimiwa Asha Rose Migiro ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Katibu wa NEC wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Professor Mwesiga Baregu aliondolewa kufundisha Chuo kikuu cha Dar es salaam kwa madai kuwa ni Mjumbe wa kamati kuu wa CHADEMA.

Je, hali hii inaasharia nini?
 
Hii inaashiria chama mbele utendaji baadae
 
Inawezekana ameshauriwa vibaya!
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dkt. Asha Rose Migiro kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Mheshimiwa Asha Rose Migiro ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Katibu wa NEC wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Professor Mwesiga Baregu aliondolewa kufundisha Chuo kikuu cha Dar es salaam kwa madai kuwa ni Mjumbe wa kamati kuu wa CHADEMA.

Je,hali hii inaasharia nini?

Kwamba huyu ndiye Jk na kama hukujua kuchukua za mbayuwayu changanya na zako utapata jibu
 
Hii inaashiria ubakaji wa demokrasia unafanywa na CCM.
Alafu huyu Asha Rose Migiro ipo siku atajuta kupuuza taaluma na kubebeshwa mzigo wa siasa.
 
Huyu mama sindiyo yule aliyeshindwa kazi kule umoja wa mataifa? Lakini poa vyuo vyenyewe sivinaendeshwa kisiasa zaidi
 
Unajua mkulu wetu huwa akiambiwa kitu na washauri wake hutenda bila kufikiria mara mbili mbili.

H
uu ni udhaifu mkubwa wa uongozi na ningependa waandishi wa nyombo vya habari waandae mjadala kuhusu hili maana lina maana sana katika siasa na elimu kwa ujumla maana kumuondoa Baregu kwa kisa tu ni mjumbe wa chama fulani cha upinzani na kumuweka madamee Migiro ambaye naye ni mjumbe pia kwenye siasa.

Hawa ndio viongozi ambao wakiondoka madarakani huwa tunawaona wakifungwa gerezani kwa matumizi mabaya ya madaraka,siku zinahesabika na hakuna mtu atakayebaki salama ambaye tunajua fika alitumia madaraka yake vibaya wakati akiwa madarakani.
 
Kuna mambo Tanzania wakati mwingine mtu inabidi ufurahi badala ya kukasirika
 

Professor Mwesiga Baregu aliondolewa kufundisha Chuo kikuu cha Dar es salaam kwa madai kuwa ni Mjumbe wa kamati kuu wa CHADEMA.

Hivi kumbe jambo hili ndilo lilomfanya asiendelee kufundisha UDSM? Mimi nilidhani ni kwa sababu alimaliza mkataba na wakamkatalia kufanya mwingine upya.
 
Ninyi ndo mnajua leo,nchi hii haijalishi unajua nini ila unamjua nani na unajishuku vipi kwake.Kamanda Baregu hakubaliani kugeuzwa mtumwa wa fikra nchini kwake hivyo ameamua kupambana ili kuleta mabadiliko.
 
Dr Asha Rose Migiro her appointed position of "Chancellor of OUT" is Ex-officio position i.e. she will not be involved in day to day management activities of OUT. Prof. Baregu was full time employee of a Government Institution...Government employees are not allowed to participate direct in political practice SAMRICH1
 
SAMRICH1

The two scenarios are distinguishable, Baregu was already retired, while Migiro is not. Wao walisema hivyo, lakini ni kwa vile alikuwa CDM anyway.
 
Last edited by a moderator:
...huyo mama anabebwa sana,UN mbeleko ilichanika waka mbwaga,ngoja tuone na hapo alipowekwa hatafanya nini?..."SIKU ZOTE ANAYEBEBWA HAJUI UMBALI WA SAFARI"...
 
Back
Top Bottom