Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Balozi , Dkt. Asha-Rose Migiro akifanya mahojiano na Crown Media ameeleza kuwa matukio ya vurugu za uchaguzi wa Oktoba 2025, yalishtua CCM
"Tutakumbuka kwamba tarehe 29 Oktoba ni tukio ambalo lilitushtua wengi, na sisi wana CCM tulishtuka zaidi. Halijawahi kutokea katika taifa letu na kwa hiyo tulipata mshangao, kulikuwa na kuduwaa, na kulikuwa na kutafuta muda wa kulitafakari kwa kina nini kimetupata sisi Tanzania baada ya miaka mingi ya kuwa nchi yenye utulivu, amani na mshikamano. Kwa hiyo lilichukua muda na tulihitaji kulitafakari hotuba ile ya Mheshimiwa Jaji Chande, ambayo ilitokana na kazi waliyoifanya yeye na wajumbe wenzake. Kwa hiyo ilichukua muda."
"Tutakumbuka kwamba tarehe 29 Oktoba ni tukio ambalo lilitushtua wengi, na sisi wana CCM tulishtuka zaidi. Halijawahi kutokea katika taifa letu na kwa hiyo tulipata mshangao, kulikuwa na kuduwaa, na kulikuwa na kutafuta muda wa kulitafakari kwa kina nini kimetupata sisi Tanzania baada ya miaka mingi ya kuwa nchi yenye utulivu, amani na mshikamano. Kwa hiyo lilichukua muda na tulihitaji kulitafakari hotuba ile ya Mheshimiwa Jaji Chande, ambayo ilitokana na kazi waliyoifanya yeye na wajumbe wenzake. Kwa hiyo ilichukua muda."