Kuweni makini, utapeli mpya umeibuka Dar

Kuweni makini, utapeli mpya umeibuka Dar

Achana nao matapeli hao. Mie walinipigia kwa namba 0762534141 na+255755334988 nikawaeleza kuwa sina hela ila kama wanahitaji wanitumie walau milioni tatu kwa njia ya mpesa. Hawakusikika tena hadi leo. Wanajaribu namba hovyo hovyo halafu wanahakiki kwenye mpesa ili wajue jina lako.
 
Mkuu siyo jambo la busara kuileta hii taarifa hapa publick!nafikiri ulitakiwa kufanyia kazi hilo jambo na kupata ufumbuzi,matapeli wamejaa kila kona lakini haituzuii kufanya au kufatilia kwa kutumia uwezo wetu tulio nao na msaada wa watu walio karibu na sisi,tusikurupuke kwa mambo kama haya,kutulia ni jambo la muhimu sana bana,ningekuwa wewe ningelifanyia kazi kama nashindwa ningetafuta watu walio karibu na mimi wanisaidie,tujifunze kutulia,kumbuka kila siku hapa wakenya wanasema sisi bado sana,ni kwenye mambo kama hayo!!maybe wewe sio mfanya biashara!
hivi umemuelewa huyu ?! Watu bana !
 
Hawa jamaa wamejitambulisha kuwa wana kampuni ya uchimbaji mabwawa na wamepata tenda ya kuchimba mabwawa kwa ajili ya maji ya kunywa wanyama katika mbuga zetu hapa tanzania.wanadai ujuzi wa uchimbaji mabwawa waliusomea ujerumani. wanadai wakati wapo ujerumani waliongea na mjerumani mmoja ambaye ni mtaalam wa madawa ya kusafisha maji. wakadai zaidi kuwa waliongea na huyo mjerumani kuwa, mara watakapomaliza maliza kozi hiyo mjerumani huyo aliwaahidi kuwa angeweza kusupply hayo madawa ya kusafisha maji kwa bei ya dola 4900 kwa ujazo walinitajia nimesahau.wakaniambia kuwa madawa hayohayo yanaweza patikana katika kiwanda kimoja hapahapa tz kwa dola 4100. hivyo wameniambia nifikirie kama nina uwezo wa kusupply hayo madawa na baadae niwasiliane nao. naomba ushauri wandugu nisije kupiga penalti ikageuka kuwa kona.
wana mahaba gani na wewe mpaka wakupe hiyo tenda ya 'Richmond' !?
 
Huu ni ujumbe kwa wana JF wote, nataka mjua kuwa hakuna fedha za kupatikana kwa urahisi kiasi hicho, ni mafisadi wao kwa wao huwa wanapeana wala siyo kwa mwenzangu n amiye eti upigiwe simu kisha upewe dili, hakuna kitu kama hicho. Kama mtu utakuwa na tamaa utalizwa, ukipigiwa simu yoyote na mtu yeyote akitaka kukupa dili kuwa makini sana. Taarifa jamaa nasikia wana ofisi Manzese jijini Dar kazi yao ndiyo hiyo ya utapeli, huwa wanajifanya waganga wa kienyeji nk.
 
Mkuu siyo jambo la busara kuileta hii taarifa hapa publick!nafikiri ulitakiwa kufanyia kazi hilo jambo na kupata ufumbuzi,matapeli wamejaa kila kona lakini haituzuii kufanya au kufatilia kwa kutumia uwezo wetu tulio nao na msaada wa watu walio karibu na sisi,tusikurupuke kwa mambo kama haya,kutulia ni jambo la muhimu sana bana,ningekuwa wewe ningelifanyia kazi kama nashindwa ningetafuta watu walio karibu na mimi wanisaidie,tujifunze kutulia,kumbuka kila siku hapa wakenya wanasema sisi bado sana,ni kwenye mambo kama hayo!!maybe wewe sio mfanya biashara!
Sijaona tatizo la kuileta hii habari hapa manake inawasaidia wengi kuwagundua hao matapeli...

Vinginevyo labda na wewe ni miongoni mwa hao matapeli.
 
Huu ni ujumbe kwa wana JF wote, nataka mjua kuwa hakuna fedha za kupatikana kwa urahisi kiasi hicho, ni mafisadi wao kwa wao huwa wanapeana wala siyo kwa mwenzangu n amiye eti upigiwe simu kisha upewe dili, hakuna kitu kama hicho. Kama mtu utakuwa na tamaa utalizwa, ukipigiwa simu yoyote na mtu yeyote akitaka kukupa dili kuwa makini sana. Taarifa jamaa nasikia wana ofisi Manzese jijini Dar kazi yao ndiyo hiyo ya utapeli, huwa wanajifanya waganga wa kienyeji nk.
Thanks mkuu!
 
Usithubutu!!!!!!!!!Niliishatapeliwa na hao watu mwezi uliopita wamenitapeli pesa zangu nyingi. Wanashirikiana na wazungu koko watatu. Nimejaribu kwenda polisi mpaka sasa sijafanikiwa kuwakamata.
Hao jamaa wana mtandao wao wa Polisi na wanapofanya tukio Polisi hao huwa wako karibu na tukio ! Endapo 'deal' imeharibika basi wale Polisi wanafika eneo la tukio kwa kasi ya ajabu, wana waarrest, wanawapeleka kituoni baadae wanaanza (Polisi) kukudiscourage wewe mlalamikaji huku jamaa wakiwa mtaani wanawinda 'washamba' wengine !
 
Hivi utapeli huu wa madawa bado unaendelea tuu!
Cha msingi ni bora ikaeleweka kuwa "THERE IS NO SHORT CUT IN LIFE"
 
Afadhali wamebadili ile stori yao ya kigoma na madawa ya kuhifadhi nafaka manake mie kila wakinipigia na stori ile natamani kuwakatisha. Ila siwaachii, shurti niwasumbue na kuwazungusha mji mzima hadi giza liingie ndo niwaambie 'kamuambieni anaewapa taarifa zangu, alipoamkia ndo mie nilipolalia. Bado sanaaa, aongeze pumzi'
 
Kuna mshkaji aliingizwa mkenge na hao jamaa walijifanya wanafanya kazi UNHCR.
 
Nini kinawazuia wao kwenda kweny kiwanda hicho, si wawe na kitengo cha manunuzi.
 
mm nawatamani kweli hawa watu..., yani nataka nikimshika mmoja namfanya kitu nikimuachia anaenda kujinyonga mwenyewe kwa hiyari yake....,

Pamoja sana.
Naomba kwelikweli nipigiwe simu na watu hawa, nawanyonyoa wakiwa wazima. Uwezo ninao
 
Naomba usaidie kuwasiliana na waandishi wengine ili kuelezea utapeli unaoendelea hapa mjini. Tayari watu watatu ninaowafahamu walitaka kutapeliwa kwa njia hii.

Jamaa anakupigia simu na kujifanya anakufahamu sana. Anakuuliza kama bado unaishi Dar. Ukikosea ukisema ndio, anakueleza yeye yuko serengeti, na ana bosi wake ambaye ni procurement officer na anamependekeza kwake jina lako ili ufanye nao biashara ya kununua vaccine za wanyama pori kwa ajili ya tiba. Ghafla anakuambia subiri uongee na boss. Bosi anakueleza jinsi walivyo na pesa nyingi kwa miaka 2 za kununulia madawa kutoka German. Anataja vaccine anayoitaka haraka sana inaitwa Gustavic animal vaccine 68f 1000mls - 50 pairs.

Anakulalamikia jinsi alivyofanya biashara na dr mmoja akawatapeli kwa hiyo wanakupendekeza wewe kwani huwezi kuwatapeli.

Anakuambia mpigie dr huyo ambaye ni agent wa dawa hiyo umwulize bei. baada ya kupata bei anakuambia subiri accountant atakupia simu. huyo tapeli accountant akikupigia simu anakelezea jinsi walivyo na peasa na utalipwa cash kisha anakuunganisha na tapeli mzungu ambaye anakuambia uende haraka kusaini contract ya miaka 2 Double tree hotel masaki. Hapo sijajua ukifika watafanyaje kwani hawa jamaa zangu wamekuwa wakstuka kabla ya kufika double tree hoteli.

Inawezekana kuna watu wameshanaswa na hawa matapeli uchwala.
 
Kuna mfanyakazi mwenzangu alilizwa two milions. Halafu ni ajabu sana kwamba baada ya kuwakabidhi tu hiyo hela na kuondoka,ndipo alipojitambua kwamba ametapeliwa. Akajaribu kuwapigia simu hawakupatikana tena. Ni kama wana kamzizi fulani. Ukiingia laini tu, unatoa hela yako yote bila kujijua, utakuja kugundua wakati ushaibiwa.
 
kwa sasa wa2 wengi wameshashituka,walianza na ku supply madawa ya nafaka,ukiwa na tamaa za pesa za haraka haraka,utaumia.
 
...naona kitu kimoja tu hapa: WATANZANIA NI VIUMBE WASAHAULIFU. Hii inanikumbusha sana hadithi moja ya nguruwe na shamba la mihogo enzi zetu kule village. Ndio maana hata kwa tunaowania majimbo inabidi tuanze harakati mwaka 2014 mwishoni.
 
Hao ni wa siku nyingi na wanakuja na mbinu tofauti, mara spare parts, mara dwa za binaadam.

Nashangaa kuwa Serikali inajuwa hili, kwani lilishaongelewa kwenye mitandao lakini mpaka leo hao watu bado wanadunda, nna uhakika jeshi la polisilikiweka mkazo haichukui siku tatu.
 
Mi nishawahi kupigiwa na mtu akijifanya ana dili la sukari toka kilombero sugar na akajifanya namba yangu kapewa na rafiki yake ambaye simfahamu. Maswali ya hapa na pale pamoja kukufahamu kilombero kulinifanya nimpotezee
 
Back
Top Bottom