Kalumbesa
JF-Expert Member
- Nov 24, 2010
- 1,013
- 356
Hawa matapeli wamecharuka sana, ila cha ajabu unaweza ukakuta mtu amesoma hii post but still anaingizwa mjini.
Kweli mkuu,umenikumbusha kuna jamaa yangu aliwahi pigwa sound ubungo akauziwa sabuni kwa kutoa simu yake na kuongezea hela akiamini ananunua simu kali zaidi.Baada ya muda mrefu kupita kama miezi 10 hivi akikatiza tena maeneo ya ubungo,jamaa mmoja akamwonyeshea simu kali huku akimfuata mwanangu cheki kitu ya ukweli,akamjibu sihitaji nyie mnauzia watu sabuni..jamaa akamwambia embu shika hii uicheki sabuni hii? mimi nimetoka kumwibia mtu hapo kwenye gari..jamaa kucheki akaona si sabuni wakaanza kuongea lugha ya biashara,mwisho wa siku akaondoka na sabuni tena.