Kuwahusu Karamagi, Rostam, na wenzao...

Kuwahusu Karamagi, Rostam, na wenzao...

ES hebu cross check na hao jamaa kwa sababu R.A alikwenda Nairobi na Precision Air ya usiku
 
Imetolewa mara ya mwisho: 28.11.2008 0146 EAT

• Uchunguzi faili la Karamagi wakamilika

*Ni kuhusu mkataba tete wa Buzwagi
*DPP Feleshi:Nimeshatoa mapendekezo
*Akina Mramba kupanda Korti Kuu leo

Na Reuben Kagaruki
Majira

IDADI ya vigogo wanaoendelea kuangukiwa na mkono mzito wa dola katika Serikali ya Awamu ya Nne huenda ikaongezeka, kufuatia kuwepo taarifa za kukamilika kwa uchunguzi wa tuhuma za kuliingiza taifa katika hasara kupitia mkataba wa Buzwagi uliosainiwa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Nazir Karamagi kwa niaba ya Serikali.

Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka ya Umma (DPP), imelithibitishia gazeti hili kukamilika kwa uchunguzi huo katika mkataba huo ambao uliibua mjadala nchini baada ya pamoja na mazingira mengine tete, mkataba huo kusainiwa nje ya nchi, mjini London, Uingereza.

Kauli hiyo ya DPP imekuja huku kukiwa kumetanda wingu zito la tetesi kuwa huenda Bw. Karamagi akafikishwa kortini muda wowote. Awali juzi iliaminika kuwa kigogo huyo angefikishwa kortini.

DPP, Bw. Eliezer Feleshi, akizungumza na Majira Dar es Salaam jana kupitia Msemaji wa Wizara ya Sheria na Katiba, Bw. Omega Ngole, alisema jalada la kesi hiyo lilikwishafanyiwa kazi na ofisi yake na kupelekwa ofisi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) tangu Septemba 9 mwaka huu.

"Jalada la Buzwagi lilipokelewa likafanyiwa kazi na kurudishwa TAKUKURU na kimsingi uamuzi wote ulifikiwa na ofisi mbili," alisema Bw. Ngole akimaanisha ofisi za TAKUKURU na ile ya DPP zililifanyia kazi kwa pamoja suala hilo.

Alipoulizwa ni lini jalada hilo lilifikishwa kwa DPP kwa mara ya kwanza, Bw. Ngole hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo.

Alipoulizwa ni lini jalada hilo litarejeshwa kwa DPP kutoka TAKUKURU kwa ajili ya kuwafikisha mahakamani waliohusika na kashifa hiyo, Bw. Ngole alijibu:

"DPP amepewa madaraka kisheria ya kukasimisha kwa chombo chochote kinachohusika kikawa na uwezo wa kisheria wa kuendesha kesi husika yenyewe."
Kwa mujibu wa sheria inayounda TAKUKURU, The Prevention and Combating of Corruption Act, 2007, taasisi hiyo inao uwezo kisheria kufungua yenyewe mashitaka na kuyaendesha baada ya kupata kibali cha DPP.

Iwapo DPP atakuwa ametoa kibali cha kuruhusu Bw. Karamagi kushitakiwa kwa tuhuma hizo na TAKUKURU ikaamua kufuata sheria, huenda Waziri huyo wa zamani aliyelazimika kujiuzulu kwa kashifa ya Richmond, akawa kiongozi wa tatu wa ngazi za juu Serikalini kuburutwa kortini.

Tayari mawaziri wa zamani Bw. Basir Mramba na Daniel Yona hadi leo wako gereza la Keko, Dar es Salaam baada ya kukosa dhamana katika mashitaka ya kuiingizia Serikali hasara waliyofunguliwa mapema wiki hii.

Mkataba huo wa Buzwagi uliosaniwa Februari mwaka huu uliibua tafrani nchini hasa baada ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe, kusimamishwa kuhudhuria Bunge baada ya kuwasilisha hoja binafsi ya kutaka Waziri Karamagi awajibishwe kwa kile alichodai alilidanganya Bunge kuhusu namna mkataba huo ulivyoingiwa na faida ambazo Serikali inatarajiwa kuzipata.

Badala yake, Bw. Kabwe aligeuziwa kibao na kuonekana kuwa yeye ndiye aliyesema uongo na Bunge likaridhia adhabu hiyo dhidi yake, adhabu ambayo ilipingwa na wananchi mbalimbali.

Bw. Zitto pia alihoji kitendo cha Karamagi kwenda kusaini mkataba huo London kwa kutumia mfumo wa mikataba ya zamani wakati Serikali ikiwa inajadiliana na wawekezaji kurekebisha mikataba ya madini nchini.

Katika hatua nyingine, Mwandishi Wetu Rabia Bakari anaripoti kuwa leo Mahakama Kuu itasikiliza maombi ya Bw. Mramba na Yona ya kuitaka Mahakama Kuu iingilie kati kile watuhumiwa hao wanacholalamikia kuwa ni masharti magumu ya dhamana waliyowekewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Watuhumiwa hao kupitia mawakili wao waliwasilisha rasmi maombi yao hayo jana kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vilivyo karibu na watuhumiwa hao, rufaa hiyo itasikilizwa leo ambapo vigogo hao watawasilisha hoja za kupinga masharti ya dhamana kama yalivyotolewa na Hakimu Hezron Mwankenja wa Kisutu.

Mahakama hiyo iliwataka watuhumiwa hao kila mmoja kujidhamini kwa sh. bilioni 3.9 ambapo katika kesi ya msingi, washitakiwa hao wanadaiwa kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia serikali hasara ya sh. bilioni 11.7.

Bw. Mramba na Bw. Yona walifikisha mahakamani hapo juzi wakikabiliwa na mashitaka 13, ikiwemo matumizi mabaya ya ofisi, madaraka na kuisababishia serikali hasara ya Sh. bilioni 11.7.

Washitakiwa hao walisomewa mashitaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Hezron Mwankenja anayesikiliza kesi hiyo.

Mwendesha Mashitaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Joseph Ole, aliwasomea mashitaka watuhumiwa hao mapema wiki hii alidai kuwa, kati ya Agosti mwaka 2002 na Juni 14 mwaka 2004 jijini Dar es Salaam, washitakiwa wakiwa watumishi wa umma kama mawaziri walitumia vibaya madaraka.

Ilidaiwa kuwa kwa kupitia kampuni ya Alex Stewart (ASSAYERS) ya Uingereza iliyoingia mkataba wa kukagua kampuni za madini nchini ambapo kwa kupitia kampuni tanzu ya Alex Stewart (ASSAYERS) Government Business Corporation waliingia mkataba na kampuni tanzu kuzalisha madini ya dhahabu kinyume na Sheria ya Manunuzi ya Umma.

Katika shitaka la pili, ilidaiwa kuwa Mramba na Yona wanadaiwa kuwa Mei 28, mwaka 2005 wakiwa watumishi wa umma jijini Dar es Salaam, wakiitumikia serikali katika nafasi za Uwaziri wa Fedha na Nishati na Madini, kwa pamoja walitumia vibaya madaraka yao kwa kusaini mikataba ya kuiongezea kampuni hiyo muda wa miaka miwili wa kuendelea kuzalisha madini kuanzia Juni 2005 hadi Juni 2007 kinyume cha Sheria ya Manunuzi ya Umma.

Ole aliendelea kudai kuwa, katika shitaka la tatu wote wawili wanadaiwa kuwa kati Machi na Mei mwaka 2005 wakiwa watumishi wa umma, walitumia vibaya madaraka yao kwa kumualika Dk. Enrique Segura wa M/S Alex Stewart ( ASSAYERS) Government Business Corporation kusaini mkataba wa nyongeza wa miaka miwili kabla timu ya majadiliano ya Serikali kulifanyia kazi suala hilo.

Katika shitaka la nne, kati ya Machi na Mei mwaka 2005, washitakiwa wanadaiwa kuwa walitumia nyadhifa zao vibaya kwa kukaidi kupeleka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali suala la kodi kama ilivyopendekezwa na Timu ya Serikali ya Majadiliano, jambo ambalo lilisababisha mkataba uongezeke kwa miaka miwili bila kupitishwa na timu ya majadiliano.

Shitaka la tano, ilidaiwa kuwa mshitakiwa Mramba Oktoba 10, mwaka 2003 akiwa Waziri wa Fedha alidharau mapendekezo ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ya kutotoa msamaha wa kodi kwa kampuni hiyo.

Katika shitaka la sita, Mramba anadaiwa kati ya 18 na 19 Desemba mwaka 2003, akiwa Waziri wa fedha, alitoa kibali namba GN 423/2003 kilichotoa msamaha wa kodi kinyume na mapendekezo yaliyopendekezwa na TRA.

Katika shitaka la saba, Mramba anadaiwa kuwa Desemba 19, mwaka 2003 akiwa Waziri wa Fedha, alitumia madaraka vibaya kwa kutoa msamaha wa kodi kwa kampuni hiyo.

Ole, aliongeza kuwa shitaka la nane, Oktoba 15, mwaka 2004 akiwa Waziri wa Fedha alitoa kibali namba GN 497/2004 kilichotoa msamaha wa kodi kwa kampuni hiyo kinyume na mapendekezo ya TRA.

Shitaka la tisa, Mramba anadaiwa kuwa kati 14 na 15 Oktoba 2004, akiwa Waziri wa Fedha alitumia madaraka yake vibaya kwa kutoa kibali namba GN 498/2004 kilichotoa msamaha wa kodi kwa kampuni hiyo kinyume na mapendekezo ya TRA.

Katika shitaka la 10, Mramba anadaiwa kuwa Novemba 15, mwaka 2005 akiwa Waziri wa Fedha alitumia madaraka yake vibaya kwa kutoa kibali namba GN 377/2005 kilichotoa msamaha wa kodi kinyume na mapendekezo ya TRA.

Katika shitaka la 11, Mramba anadaiwa kuwa Novemba 15, 2005 akiwa Waziri wa Fedha alitumia madaraka yake vibaya kwa kutoa kibali namba GN 378/2005 kilichotoa msamaha wa kodi kwa kampuni hiyo kinyume na mapendekezo ya TRA.

Katika shitaka la 12, Mramba na Yona wanadaiwa kuwa kati ya Juni 2003 na Mei 2005 wakiwa na nyadhifa hizo za uwaziri kwa makusudi na kutowajibika waliruhusu mkataba wa kuzuia kulipa kodi ili kuipendelea kampuni hiyo na kuisababishia Serikali hasara ya Sh. 11, 752,350,148.00.

Katika shitaka la mwisho, Mramba anadaiwa kuwa kati ya 2003 na 2007 akiwa Waziri wa Fedha kwa makusudi alishindwa kuwa makini au kutotimiza wajibu wake alisaini vibali, kuruhusu kampuni hiyo kutokulipa kodi na kuisababishia serikali hasara ya sh. bilioni 11.7.
 
I wonder where is Mzee Kingunge who dared to lie to Tanzanians infront of Camera kuwa walioibua hii ni waongo na lengo lao ni kuleta distraction. Sasa hapa naona DPP anaweza kututhibitishia kuwa Mzee alitudanganyam if that is the case kuna haja ya kuangalia uwezekana wa kufikishwa mahakamani kwa conspiracy ya kujaribu ku-cover up wizi wa mali ya taifa. Nina hakika watu wa DPP mnasoma hili ni moja kati ya mambo yanayoweza kufanyiwa kazi. Kama watu wa TV mnarekodi hiyo ingekuwa poa sana kama mngetuwekea hapa na kuisikiliza kauli ya mzee kingunge na jamaa waliotangaza kuwapeleka kina Slaa mahakamani.
 
Wako pembeni wanapanga mipango ya siri ya kupambana na mama k maana wanadai ndiye mchawi wao, maana mkulu amewambia kua amechoka na kelele za mafisadi ndani ya ccm, wao kina kingunge wanadai hata mumewe mama k ni mchafu pia hii itakuwa very interesting!
 
Tayari mawaziri wa zamani Bw. Basir Mramba na Daniel Yona hadi leo wako gereza la Keko, Dar es Salaam


Hii sentensi ni kama vigumu kuamini imetokea. Kweli dunia duara, sijui kwanini jamaa walitengeneza hizo VIP cells huko keko. Lingekuwa jambo la maana sana kama wangepelekwa wanakoenda wahalifu wengine
 
Mkuu neno lingine la muhimu sana linalosahauliwa so far ni kwamba Yona ni m-bia na Mkapa kwenye kumiliki Kiwira,

haya ni maneno very soon yatakuwa na maana kubwa sana na hii kesi, watch!
 
Mkuu neno lingine la muhimu sana linalosahauliwa so far ni kwamba Yona ni m-bia na Mkapa kwenye kumiliki Kiwira,

haya ni maneno very soon yatakuwa na maana kubwa sana na hii kesi, watch!

Kuna moja najiuliza sana kwanini ya Yona haizungumziwi na Kiwira, ingekuwa picha nzuri sana kama ya Kiwira ingewekwa halafu Mkapa aachwe kwanza, ma yeye awe anafuatilia behind the scenes na ajue what is comong ahead of him.Tuko kwenye very interesting juncture. Lakini kuna habari moja inanishangaza sana. Hwat happens kama cabinet yote inatoa baraka kwa ufisadi, kuna possibility ya cabinet nzima kufikishwa mahakamani? I wonder kama scenario kama hii imefikiriwa na sheria zinaruhusu.
 
Wakuu FMES na Bubu ataka Kusema(BAK);

Big up!

Kuna mtu ameenda kucheki Kaburi la Nyerere? kunaweza kukawa na mabadiliko fulani.

Mawazo yake yanaishi, aliijenga Tanzania ya amani na hakutaka viongozi waovu,

nahisi karoho kake kanachezacheza kwa furaha

bY THE WAY MGONJA VIPI???
 
- dataz zaidi ni kwamba huko nyuma el na ra waliwahi kutaka kumsababisha ro atoswe lakini akaponea chupu chupu, sasa ni time ya payback nasikia moto unakuja, maana kuna special investigators wanaoshughulikia richimonduli tu na wako tayari kuwachukua wanaohusika, just a matter of time!

...kesho wakuu!
 
Kuna mtu ameenda kucheki Kaburi la Nyerere? kunaweza kukawa na mabadiliko fulani. Mawazo yake yanaishi, aliijenga Tanzania ya amani na hakutaka viongozi waovu, nahisi karoho kake kanachezacheza kwa furaha

I see kuna mkulu mmoja leo amenibonyeza kwamba siku za karibuni alimuona muungwana mahali akisikiliza wimbo wa "......Tanzania, Tanzania nakupenda kwa moyo wote....."

akaniambia "..kijana nimemuona kwa macho yangu machozi yakimtoka huku akiusikiliza huu wimbo, ndio maana sishangai haya yanayotokea sasa na sitasahu ile siku nilipomuona....".

kesho wakuu!
 
I see kuna mkulu mmoja leo amenibonyeza kwamba siku za karibuni alimuona muungwana mahali akisikiliza wimbo wa "......Tanzania, Tanzania nakupenda kwa moyo wote....."

akaniambia "..kijana nimemuona kwa macho yangu machozi yakimtoka huku akiusikiliza huu wimbo, ndio maana sishangai haya yanayotokea sasa na sitasahu ile siku nilipomuona....".

kesho wakuu!

Haya Mkuu
ila hii sentensi ni nzito sana. Itabidi tuiweke kwenye kumbukumbu
 
JK huenda alisikia huo wimbo akakumbuka nchi ilivyojaa vimwana wa nguvu chozi likamtoka; sio lazima iwe ni kwa sababu ya ufisadi.
 
I see kuna mkulu mmoja leo amenibonyeza kwamba siku za karibuni alimuona muungwana mahali akisikiliza wimbo wa "......Tanzania, Tanzania nakupenda kwa moyo wote....."

akaniambia "..kijana nimemuona kwa macho yangu machozi yakimtoka huku akiusikiliza huu wimbo, ndio maana sishangai haya yanayotokea sasa na sitasahu ile siku nilipomuona....".

kesho wakuu!

Haya Mkuu
ila hii sentensi ni nzito sana. Itabidi tuiweke kwenye kumbukumbu

Kweli wimbo ule unatia huzuni ukiona TANZANIA YA JANA NA LEO.

By the way ''Better late than never'' kama alilia basi tumeshalia wengi tukanyamaza! sasa zamu yake, ila lia yake yeye ina nguvu ate least tunaziona!

Mungu amsaidie iwe kwa utashi wake yeye, donors, usalama wa taifa n.k,


waberoya
 
*Ni kuhusu mkataba tete wa Buzwagi
*DPP Feleshi:Nimeshatoa mapendekezo



IDADI ya vigogo wanaoendelea kuangukiwa na mkono mzito wa dola katika Serikali ya Awamu ya Nne huenda ikaongezeka, kufuatia kuwepo taarifa za kukamilika kwa uchunguzi wa tuhuma za kuliingiza taifa katika hasara kupitia mkataba wa Buzwagi uliosainiwa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Nazir Karamagi kwa niaba ya Serikali.

Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka ya Umma (DPP), imelithibitishia gazeti hili kukamilika kwa uchunguzi huo katika mkataba huo ambao uliibua mjadala nchini baada ya pamoja na mazingira mengine tete, mkataba huo kusainiwa nje ya nchi, mjini London, Uingereza.

Kauli hiyo ya DPP imekuja huku kukiwa kumetanda wingu zito la tetesi kuwa huenda Bw. Karamagi akafikishwa kortini muda wowote. Awali juzi iliaminika kuwa kigogo huyo angefikishwa kortini.

DPP, Bw. Eliezer Feleshi, akizungumza na Majira Dar es Salaam jana kupitia Msemaji wa Wizara ya Sheria na Katiba, Bw. Omega Ngole, alisema jalada la kesi hiyo lilikwishafanyiwa kazi na ofisi yake na kupelekwa ofisi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) tangu Septemba 9 mwaka huu.

"Jalada la Buzwagi lilipokelewa likafanyiwa kazi na kurudishwa TAKUKURU na kimsingi uamuzi wote ulifikiwa na ofisi mbili," alisema Bw. Ngole akimaanisha ofisi za TAKUKURU na ile ya DPP zililifanyia kazi kwa pamoja suala hilo.

Alipoulizwa ni lini jalada hilo lilifikishwa kwa DPP kwa mara ya kwanza, Bw. Ngole hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo.

Alipoulizwa ni lini jalada hilo litarejeshwa kwa DPP kutoka TAKUKURU kwa ajili ya kuwafikisha mahakamani waliohusika na kashifa hiyo, Bw. Ngole alijibu:

"DPP amepewa madaraka kisheria ya kukasimisha kwa chombo chochote kinachohusika kikawa na uwezo wa kisheria wa kuendesha kesi husika yenyewe."

Kwa mujibu wa sheria inayounda TAKUKURU, The Prevention and Combating of Corruption Act, 2007, taasisi hiyo inao uwezo kisheria kufungua yenyewe mashitaka na kuyaendesha baada ya kupata kibali cha DPP.

Iwapo DPP atakuwa ametoa kibali cha kuruhusu Bw. Karamagi kushitakiwa kwa tuhuma hizo na TAKUKURU ikaamua kufuata sheria, huenda Waziri huyo wa zamani aliyelazimika kujiuzulu kwa kashifa ya Richmond, akawa kiongozi wa tatu wa ngazi za juu Serikalini kuburutwa kortini.

Tayari mawaziri wa zamani Bw. Basir Mramba na Daniel Yona hadi leo wako gereza la Keko, Dar es Salaam baada ya kukosa dhamana katika mashitaka ya kuiingizia Serikali hasara waliyofunguliwa mapema wiki hii.

Mkataba huo wa Buzwagi uliosaniwa Februari mwaka huu uliibua tafrani nchini hasa baada ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe, kusimamishwa kuhudhuria Bunge baada ya kuwasilisha hoja binafsi ya kutaka Waziri Karamagi awajibishwe kwa kile alichodai alilidanganya Bunge kuhusu namna mkataba huo ulivyoingiwa na faida ambazo Serikali inatarajiwa kuzipata.

Badala yake, Bw. Kabwe aligeuziwa kibao na kuonekana kuwa yeye ndiye aliyesema uongo na Bunge likaridhia adhabu hiyo dhidi yake, adhabu ambayo ilipingwa na wananchi mbalimbali.

Bw. Zitto pia alihoji kitendo cha Karamagi kwenda kusaini mkataba huo London kwa kutumia mfumo wa mikataba ya zamani wakati Serikali ikiwa inajadiliana na wawekezaji kurekebisha mikataba ya madini nchini.
 
yenye kichwa cha habari 'Kuwahusu Karamagi, Rostam, na wenzao...' nashangaa kwa nini mmeifunga wakati bado maswala ya wahusika hayajafikia tamati.

Shukrani.
 
Wakuu za saa hizi! Du leo nimechelewa kuja humu jamvini kweli. Jama tujuzeni yalojiri huko High Court. Vipi Mramba kapata dhamana? Ama ndo hivyo tena upande wa pili kakaa Mzee Msiba na upande ule kaka mtu ndo anamwakilisha Mzee wetu? Keki itapelekwa Keko nini?
 
Naomba kuelimishwa.
Mara nyingi nimekuwa nikisikia kuwa unapoongelea swala ambalo tayari liko mahakamani, unaingilia uhuru wa mahakama. Hizi kesi walizofunguliwa mafisadi, serikali haitatumia loophole hiyo kuwaziba midomo Mbowe & co ili wasiwaelimishe wananchi juu ya uhaini wanaotufanyia?
 
2. Jana Karamagi alijaribu kusaifiri kuelekea USA, akazuiwa uwanja wa ndege na kunyang'anywa documents zake zote, na kuchukuliwa "somewhere"
Kumbe passport bado anaimiliki yeye mwenyewe?
Anaweza akala border tu border akiingia Namanga akiibukia Somalia tumesha mkosa mbaneni huyo.
 
Looks like no updates regarding the bail of this guys. Its Kili time now,,,, Thank God its weekend!
 
Back
Top Bottom