Kuwa kichaa sio mpaka kuokota makopo! Je, Tanzania tuna vichaa wengi kuliko tunavyojidhania?

Still reflecting on what you have just said which is very true by the way! But aren't you suffering from insomnia? Failure to sleep is a mental disease and if not treated timely may lead to further complications. I suggest that you see a doctor.
 
Wanabodi,
Saa hizi natafuta usingizi unagoma, hivyo nimeshuka jf, tutafakari pamoja kuhusu huu utafiti uliowahi kufanywa na kubaini kuwa kwenye kila Watanzania 4, mmoja ni kichaa!. Jee katika hizo sampling, inawezekana pia kukawa na baadhi ya viongozi wetu wa vyama, taasisi, mashirika, na serikali na taasisi zake?. Huu utafiti ulipotoka sikuuamini niliuona kama umekuwa exaggerated, lakini kadri siku zinavyokwenda na mambo yanavyokuwa, mwenzenu nimeanza kuuamini kwa kujifanyia self diognosis na kukuta ni kweli!. Wewe jiulize jee wewe ni mzima?, na kisha jiulize hivi sisi Watanzania tuu wazima kweli? !. Tufanyeje kuondokana na hali hii?.
93dabf10a9a1ea1c5395c14deb0a409c.jpg


Huu ni uzi wa swali, kuwa
Kuwa Kichaa Sio Mpaka Mtu Aokote Makopo!. Jee Kuna Uwezekano Tanzania Tunao Vichaa Wengi Kuliko Tunavyojidhania?!.

Kuna msemo usemao kuwa kichaa sio lazima mtu mpaka aokote makopo, ila kwa maneno na matendo ya baadhi ya sisi Watanzania wakiwemo baadhi ya viongozi wetu, nashawishika kabisa kuamini, kuna uwezekano wengine sio wazima kabisa kichwani ila pia sio vichaa kwa sababu hawaokoti makopo! .

Hoja hii imetokana na kutafakari kwa makini baadhi ya kauli, maagizo, na maamuzi yetu sisi kama Watanzania na viongozi wetu accross the section, na baadhi ya matendo yao yakiwemo maamuzi yao ,amri zao na hatua ambazo wanachukua kudeal na situations mbali mbali zinanithibitishia kuwa badhi ya wenzetu sio wazima kabisa kichwani na na mimi nikiwemo, hivyo wanahitaji kusaidiwa kujitafakari badala ya kushangiliwa tuu kwa kila wanachokifanya, hata wakifanya ndivyo sivyo, watashangiliwa tuu na kupongezwa! .


Vichaa Viongozi.
Kwa muktadha huo wa ukichaa, ukiwasikiliza matamko ya baadhi ya wanasiasa na viongozi wa serikali, na ukafuatilia matendo yao,amri zao na maamuzi yao, utakubaliana na mimi sisi Watanzania tuna vichaa wengi kuliko tunavyo jidhania.

What to do to help out.
Mtu kichaa hajijui kama kichaa mpaka atakapojulishwa ukichaa wake, na kujitafakari, ndipo atajigundua na kubadilika. Namna ya kuwasaidia viongozi wetu kujitambua, ni pale wanapotamka matamshi ya kiendawazimu, au kutoa maamuzi ya kiendawazimu, badala ya kuwashangilia wazomeeni ili wajitambue.

Kitendo cha viongozi hawa kutoa matamshi ya kiendawazimu na maamuzi ya kiajabu ajabu na sisi tukiwashangilia badala ya kuwakemea au kuwazomea, kunapelekea wote kuonekana ni vichaa!.

Hivi kweli Tanzania tumefika hapa kuwaacha vichaa hawa kufanya ukichaa wao huku sote tukishangilia tuu bila kukemea, jee sote ni vichaa au kuna wenzetu wanaona tofauti na wanaweza kusaidia tubadilike?.

Paskali
Ukizomea utashughulikiwa kama mhaini mkubwa nchini
 
Hata me naona hili ni kweli kati ya watu wanne ninaotembea nao mmoja wetu ni unsound but haijawahi kuwa ni mimi na Nafurahi kwa hilo.
 
Mi nionavyo kila binadamu ni kichaa ila kuna kuzidiana viwango tu.mwingine anasema sana,mwingine hasemi kabisa,mwingine msafi sana mwingine hataki kuona maji.nk.Tatizo hatujui lini kitalipuka na sifa kuu ya kichaa ni kukataa kuwa anaumwa. Nadhani hiyo tafiti iko biased.possibly kwa tz ni vichaa 3 katika kila watu 4.
 
Paskali unejitangaza rasmi wewe kichaa ama hujielewi!? Nenda hospitali mara moja chagua Muhimbili ama Mirembe watakusaidia. Kuna tofauti ya madness na psychiatry. Siyo vibaya ukitibiwa.
 
Paschal kwanini umewaza hivyo?

Kawaza jambo jema sana. Hebu fikiria msingi wa hoja yake (ambao tumeshaufahamu) uwe ni kweli na kwamba huyo mtu ni mmoja wa wagonjwa huoni hatari inayotukabili? Nani wa kumfunga kamba na kumpeleka pale Muhimbili au Dodoma kwa check up? Hakuna.
Na jee wanao fanya nae kazi kama wamegundua kuwa ana tatizo hilo unadhani watafanya nini? Ni kutumia advantage hiyo kujua mgonjwa wetu huwa anapendelea nini nasi tutafaidikaje kwa kutumia udhaifu wake kwa kile apendacho. Then two,three or four years ni disaster na hakuna atakayewajibishwa.
 
Ukichaa zaidi ingetokea sisi watanzania tungemchagua maMvi. Apo tungekua tumethibitisha kwelisisi nipunguani kwawale wanao tuzunguka.
 
Kuna kiongozi wa upinzani juzi katika kampeni ya udiwani alikuwa anasisitiza kabisa achaguliwe diwani wa ccm kwa kura nyingi sana.
 
Mkuu Pasco kwa kuwa ulizaliwa kipindi cha NJAA/MAYALLA ninakutangaza rasmi kuwa balozi wa kutangaza njaa na ukame unaowakabili watanzania kwa kipindi hiki.Ukiwa kama mwandishi wa habari huru tumia kalamu yako kupaza sauti.
Mungu akubariki
 
Back
Top Bottom