Kuvaa Hijab ni dini au udhaifu wa wanaume?

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,310
12,607
Binadamu wote wake kwa waume wanazaliwa wakiwa uchi kabisa, kuvaa nguo ipi na ivaliwe wapi na nani kwa sababu gani ni utashi tu wa wanajamii wenyewe. Bahati mbaya au nzuri Mwenyezi kuna maeneo na viungo vya mwili ambavyo alishavifunika yeye mwenyewe kwa sababu zake kwa kutumia nywele ndefu na nywele fupi kutokana na umuhimu wake na sababu zake. Mfano, Mungu amekifunika kichwa cha kila mtu kwa nywele ndefu bila kujali jinsia yake, kabila wala dini yake, Mungu akakifunika kinena cha kila mtu aliyebalehe kwa nywele ndefu tunazoziita mav*zi. Hakuishia hapo akakifunika kidevu na kifua cha mwanaume kwa nywele ndefu pia kwa sababu zake mungu mwenyewe. Hakuishia hapo akaifunika ngozi ya mwili ya watu wote kwa nywele fupi tunazoziita malaika kwa sababu zake pia, akatupa pia nyusi, kope na nyweli puani bila ya kumuomba. Hivyo kila nywele ilikuwa na sababu yake na ilitosha kabisa kuifanya kazi iliyokusudiwa kufunikwa na kukingwa. Hii ni kuonyesha kuwa Mungu anayajuwa mahitaji yetu yooote.

Ni nani ambae hataki kumuona mwanamke ambae asiyefunika nywele zake? Je, ni mwanamke mwenyewe kwa sababu zipi? Je, ni mwanaume kwa sababu zipi na je, ni Mungu aliyetufanya tuzaliwa uchi lakini akatufunika kwa nywele kwa sababu zipi?

Utafiti wangu kwenye hili ni kwamba, sio Mungu anaetaka wanawake wavae Hijab bali ni wanaume tu kwa sababu ya wivu na kujifanya kuwa wao ni dhaifu kwa kutazama tu nywele, matiti, mapaja na vitovu vya wanawake wakasahau kuwa Mungu angetaka asingeshindwa kuwafanya wanawake wazaliwe wakiwa na hijab tayari. Tuache ujinga wa kuwadhulumu wanawake kwa kujificha kwenye kichaka cha dini. Nini sio Hijab wala nywele za mtu.

Ona haya mauaji na maandamano ya kijinga kabisa, eti msichana hakuvaa hijab.

 
Duniani tunaishi kwa taratibu fulani tulizojiwekea au zilizowekwa kulingana na mahitaji au kukidhi madhumuni fulani.

Taratibu hizi zinaweza kubadilika kulingana na mahitaji ya wakati husika.
Lakini pia taratibu zinaweza kutofautiana baina ya eneo moja na jingine, tamaduni moja na nyingine, n.k

Kwa ambao dini yao inawalazimisha kuvaa mavazi ya aina fulani, acha wafuate taratibu hizo kwa mujibu wa dini yao.

Wale ambao dini haiwalazimishi kuenenda katika namna hiyo, acha wasiyafanye hayo.

Kinacholeta fujo na machafuko duniani ni kujaribu kulazimishana kufuata mfumo fulani mahsusi wa maisha.

Mungu yeye hana baya, alitoa haki kamili ya mtu kujichagulia namna ya kuishi, na kuwa tayari kwa matokeo (consequences) za chaguo hilo.

Dunia ngumu sana hii.
 
Mtoto anazaliwa na nywele zake Mungu alizeweka kwa maksudi ila
Wasabato wanaabiwa wasizisuke (sijui ndilo lilikuwa kusudi la Mungu?)

Waislamu wamaambiwa wazifunike (na ni kosa linalo weza kupelekea kifo uliziacha wazi ☺☺🤔🤔🤔) sijui ndio kusudi la Allah?
 
Ulichoandika hakina maana ni uchafu mtupu!! Haya usivae nguo uone ,Hayo mambo ni katika kuslow down mahaswi kutokana na Tamaa za kibadamu kinaweza kuchochea uzinifu .

Hakuna mahali umelazimishwa ila kama unataka kuifuata uislamu basi tii Sheria hyo kwa mwanamke kwa nn unapenda kufuatilia vitu havikuhusu ,nenda kaangalie masisters wanavaaje kanisani kama hujui hekima ya wao kuvaa ile hijabu ni ishu za kujistiri angalia na mapadre ulishawai kuona wapo padre kavaa kipensi, nenda hata ofisini uvae kipensi uone .
 
Ulichoandika hakina maana ni uchafu mtupu!! Haya usivae nguo uone ,Hayo mambo ni katika kuslow down mahaswi kutokana na Tamaa za kibadamu kinaweza kuchochea uzinifu .

Hakuna mahali umelazimishwa ila kama unataka kuifuata uislamu basi tii Sheria hyo kwa mwanamke kwa nn unapenda kufuatilia vitu havikuhusu ,nenda kaangalie masisters wanavaaje kanisani kama hujui hekima ya wao kuvaa ile hijabu ni ishu za kujistiri angalia na mapadre ulishawai kuona wapo padre kavaa kipensi, nenda hata ofisini uvae kipensi uone .
Mbona bongo wanawake hawavai na waislam sio wazinifu?
 
Duniani tunaishi kwa taratibu fulani tulizojiwekea au zilizowekwa kulingana na mahitaji au kukidhi madhumuni fulani.
Taratibu hizi zinaweza kubadilika kulingana na mahitaji ya wakati husika.
Lakini pia taratibu zinaweza kutofautiana baina ya eneo moja na jingine, tamaduni moja na nyingine, n.k

Kwa ambao dini yao inawalazimisha kuvaa mavazi ya aina fulani, acha wafuate taratibu hizo kwa mujibu wa dini yao.

Wale ambao dini haiwalazimishi kuenenda katika namna hiyo, acha wasiyafanye hayo.

Kinacholeta fujo na machafuko duniani ni kujaribu kulazimishana kufuata mfumo fulani mahsusi wa maisha.

Mungu yeye hana baya, alitoa haki kamili ya mtu kujichagulia namna ya kuishi, na kuwa tayari kwa matokeo (consequences) za chaguo hilo.

Dunia ngumu sana hii.
Ni dini gani iliyojenga viwanda vya kutengeneza Hijab, kanzu, suti au majuba? Mungu alitosha, anatosha na atatosha hata kesho, mavazi sio dini, hayatengenezwi na dini na wala hayatoki mwa mungu na hutaenda peponi kwa mavazi tu. Tunawaonea wanawake kwanini? Mbona wanaume nao wanatembe vichwa, vifua na mabaya vikiwa wazi? mbona wanawake hawahoji?
 
Kuvaa hijabu ni amri ya Mwenyezi Mungu kwa wanawake wote wa Kiislamu. Na hii inawasidia wenyewe wasiudhiwe hasa kutokana na maungo yao kuwa ya kuvutia kwa hivyo wakijisitiri hawapati usumbufu.
Haya mavazi ndio hayo hayo aliyoyavaa Mama yake Issa/Yesu (Yaani Mariamu) na ndivyo wanavyo vyaa masista wa katoliki.

QURAN 33: 59
" Ewe Nabii! Waambie wake zako, na binti zako, na wanawake waumini wajiteremshie nguo zao. Hivyo kutafanya watambulikane (kuwa ni wenye kujiheshimu) wasiudhiwe. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu."
 
Back
Top Bottom