covid 19
JF-Expert Member
- May 9, 2014
- 8,042
- 20,045
Wakuu ipo hivi kwa mtazamo wangu nashawishika kusema kwamba utunzaji wa pesa ni kipaji si bure nishawaza kila aina iman juu ya utunzaji pesa hatimaye nimefikia hitimisho hivyo.
Nilishajitahidi sana na kujiapiza sana ila wapi yaani lazima tu itatokea kisanga cha kupelekea kutumia pesa niliyohifadhi au basi tu hizi statements za acha nitoe alafu nitarudishia ndio usiseme zinafilisi balaa.
Hivi wale watu ambao hata wakutwe na balaa gani hawatoi pesa walizohifadhi ni discipline tu au kuna namna wanakuwa hivyo automatic au ni wabinafsi sana au wachoyo au ni wanaroho ngumu tu. mimi mbona siwezi kumuona mtu anakufa njaa afu nina hela mfukoni basi nitatoa tu kiroho safi.
Binafsi naona utunzaji wa pesa ni kipaji kama vipaji vingine kama hujajaaliwa na Mungu huwezi, utaishia kujilaumu tu kulaumiwa.
Nilishajitahidi sana na kujiapiza sana ila wapi yaani lazima tu itatokea kisanga cha kupelekea kutumia pesa niliyohifadhi au basi tu hizi statements za acha nitoe alafu nitarudishia ndio usiseme zinafilisi balaa.
Hivi wale watu ambao hata wakutwe na balaa gani hawatoi pesa walizohifadhi ni discipline tu au kuna namna wanakuwa hivyo automatic au ni wabinafsi sana au wachoyo au ni wanaroho ngumu tu. mimi mbona siwezi kumuona mtu anakufa njaa afu nina hela mfukoni basi nitatoa tu kiroho safi.
Binafsi naona utunzaji wa pesa ni kipaji kama vipaji vingine kama hujajaaliwa na Mungu huwezi, utaishia kujilaumu tu kulaumiwa.