Kutokana na ushahidi unaoendelea kutolewa mahakamani, kwenye kesi ya ugaidi ya akina Mbowe, Rais Samia huna budi kumstaafisha IGP Sirro

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Imeandikwa kwenye Biblia, kitabu cha Mithali 14:34 "Haki huinua Taifa bali dhambi ni aibu ya watu wote" mwisho wa kunukuu.

Kwa huu mwendelezo unaoendelea kutolewa mahakamani Katika kesi ya ugaidi ya akina Mbowe, hakika ni aibu kubwa Sana kwa Taifa letu kuwa na Jeshi la Polisi, ambalo halitaki hata kufuata kanuni zao zinazojulikana kwa lugha ya kigeni kama "PGO" na badala yake linajifanyia mambo kivyake, kwa ajili tu ya kuwakomoa wapinzani na kuhakikisha wanaendelea kuwabakisha nyinyi CCM madarakani.

Rais Samia utambue kuwa hii kesi ya akina Mbowe, inafuatiliwa kwa karibu Sana na Jumuiya ya kimataifa na ndiyo sababu mabalozi mbalimbali wa nchi za magharibi wanahudhuria mfululizo kesi hiyo.

Hata hivyo ni majuzi tu umerudi kutoka kwenye mkutano mkubwa wa UN, ambako uliitangazia Dunia kuwa nchi yetu ina "vibrant democracy" na inazingatia kwa hali ya juu haki za binadamu.

Hivi haki gani za kibinadamu zinazofuatwa kwenye nchi yetu kama Polisi wenyewe hawataki hata kuzifuata kanuni zao wenyewe zilizopo kwenye "msahafu" wao wa PGO??

Kama Polisi wetu wanaweza kuthubutu kutaja kwenye ushahidi kuwa watuhumiwa walikutwa na madawa ya kulevya, wakati kwenye "charge sheet" hakuna tuhuma hiyo, hivi unadhani kweli Jeshi letu la Polisi linafanya kazi yake kwa weledi??

Hao Polisi wanaweza kutueleza alipo mtuhumiwa Moses Lijenje kama siyo wamemtanguliza ahera??

Wajibu wa kwanza wa Jeshi la Polisi nchini ni kulinda uhai wa raia na mali zao, sasa inapotokea Jeshi hilo ndilo linaongoza kuwapoteza wananchi wake, maana yake limeshindwa kutekeleza wajibu wao

Kama hutaweza kumstaafisha IGP Sirro kutokana na aibu kubwa aliyoiletea Taifa, Katika kesi hii ya uonevu wa hali ya juu, ya akina Mbowe, basi tutaamini kuwa Jeshi la Polisi, ni "kitengo" ambacho kipo mahsusi na kinalindwa na Dola hii ya CCM kwa lengo la kuendelea kuwabambikizia kesi za uongo wapinzani wa nchi hii, ili CCM iendelee kutawala milele!
 
HAITOSHI. Kuondoka kwa Sirro hakuleti nafuu yoyote bila ya kubadili mfumo mbovu ulioota mizizi ndani ya chombo hicho.

Kustaifishwa kwa mtu mmoja katika taasisi iliyooza habadili kitu.

Kama wameona Tanesco kuna ubovu na wakafanya mabadiliko makubwa, ni hivyo hivyo na kwenye taasisi nyingine . Uozo upo kila sehemu na huko polisi kunatakiwa kufumuliwa kabisa na kuanza kusukwa upya.

Ondoa takataka zote za akina Moroto na wengine ambao tabia zao zimekuwa za kukandamiza wananchi. Ni lazima pawepo na chombo cha 'oversite' kutazama mwenendo wa vyombo hivi vya ukandamizaji na kuhakikisha kuwa kazi zao zimo ndani ya mipaka waliyowekewa.

Sasa hivi polisi wanajitungia sheria popote wanapojisikia sheria zilizopo zinawanyima mwanya wa kuwakandamiza wananchi. Wanavunja sheria na hakuna wa kuwakemea.

Hii yote inatokana na kufanywa kuwa chombo cha kisiasa, kukitumikia chama cha CCM. Katika utaratibu mpya iwe ni marufuku kabisa kwa hivi vyombo vya dola kutumiwa na vyama vya siasa..
 
Dah... Mungu wa ajabu sana, sikuile jamaa anajifanya Mkristo Safi na Kumuhukumu Mbowe kwenye press conference yake hakujua kuwa hii kesi itakuja kumchafua na yeye pia na zaidi itamuanika rangi yake halisi..
 
Sirro alisema wafuasi wa Chadema wanamuona Mbowe malaika, hakujua kama wenzake walicheza mchezo kwenye kesi ya kutengeneza, sasa kwa ushahidi uliotolewa naamini anakuta kutoa ile kauli yake.
 
HAITOSHI. Kuondoka kwa Sirro hakuleti nafuu yoyote bila ya kubadili mfumo mbovu ulioota mizizi ndani ya chombo hicho...
Unaposhauri kubadili mifumo (naamini kwa maana ya utendaji) ya vyombo vya Dola, ukumbuke tatizo liko kwenye mifumo ya kufikiri kwenye bongo za watendaji na hasa WanasiHasa
 
Imeandikwa kwenye Biblia, kitabu cha Mithali 14:34 "Haki huinua Taifa bali dhambi ni aibu ya watu wote" mwisho wa kunukuu...
Hawezi kwakua anachokifanya Sirro kiko ndani ya sera na miongozo ya CCM, hivi umewahi kujiuliza kilichomtokea Kolimba kingekuwa kwenye kikao cha Chadema nini kingetokea? Akwilina aliuawa na polisi masikini yule binti hajui na hatajua nani alimpiga risasi kwa sababu polisi wslihusika, tukio la kulipuliwa kwa bomu Mwangosi walitupiwa Chadema kuhusika na bomu!

Kijana wa Morogoro kuuawa kwa risasi kisha kutupiwa Chadema, bomu la Arusha mkutano wa Chadema wakatupiwa Chadema, bahati nzuri la Manzese liliwalipukia wenyewe ndani ya gari hivyo wakashindwa kuwatupia Chadema, na mtukio yote hayo hakuna aliyehusika!

Kwahiyo suala la Sirro kuwajibishwa halitawezekana kwani ndio wanaoiwezesha CCM kudumu kwa amani.
 
Unaposhauri kubadili mifumo (naamini kwa maana ya utendaji) ya vyombo vya Dola, ukumbuke tatizo liko kwenye mifumo ya kufikiri kwenye bongo za watendaji na hasa WanasiHasa
Ninakubaliana nawe kuhusu "wanasiasa", na ndiyo maana katika uundaji wa mfumo mpya hawatakiwi kuwa wahusika wa uundwaji huo wa mfumo mpya.
Hiki ni chombo cha wananchi siyo mali ya chama chochote cha siasa.
 
Imeandikwa kwenye Biblia, kitabu cha Mithali 14:34 "Haki huinua Taifa bali dhambi ni aibu ya watu wote" mwisho wa kunukuu.

Kwa huu mwendelezo unaoendelea kutolewa mahakamani Katika kesi ya ugaidi ya akina Mbowe, hakika ni aibu kubwa Sana kwa Taifa letu kuwa na Jeshi la Polisi, ambalo halitaki hata kufuata kanuni zao zinazojulikana kwa lugha ya kigeni kama "PGO" na badala yake linajifanyia mambo kivyake, kwa ajili tu ya kuwakomoa wapinzani na kuhakikisha wanaendelea kuwabakisha nyinyi CCM madarakani.

Rais Samia utambue kuwa hii kesi ya akina Mbowe, inafuatiliwa kwa karibu Sana na Jumuiya ya kimataifa na ndiyo sababu mabalozi mbalimbali wa nchi za magharibi wanahudhuria mfululizo kesi hiyo.

Hata hivyo ni majuzi tu umerudi kutoka kwenye mkutano mkubwa wa UN, ambako uliitangazia Dunia kuwa nchi yetu ina "vibrant democracy" na inazingatia kwa hali ya juu haki za binadamu.

Hivi haki gani za kibinadamu zinazofuatwa kwenye nchi yetu kama Polisi wenyewe hawataki hata kuzifuata kanuni zao wenyewe zilizopo kwenye "msahafu" wao wa PGO??

Kama Polisi wetu wanaweza kuthubutu kutaja kwenye ushahidi kuwa watuhumiwa walikutwa na madawa ya kulevya, wakati kwenye "charge sheet" hakuna tuhuma hiyo, hivi unadhani kweli Jeshi letu la Polisi linafanya kazi yake kwa weledi??

Hao Polisi wanaweza kutueleza alipo mtuhumiwa Moses Lijenje kama siyo wamemtanguliza ahera??

Wajibu wa kwanza wa Jeshi la Polisi nchini ni kulinda uhai wa raia na mali zao, sasa inapotokea Jeshi hilo ndilo linaongoza kuwapoteza wananchi wake, maana yake limeshindwa kutekeleza wajibu wao

Kama hutaweza kumstaafisha IGP Sirro kutokana na aibu kubwa aliyoiletea Taifa, Katika kesi hii ya uonevu wa hali ya juu, ya akina Mbowe, basi tutaamini kuwa Jeshi la Polisi, ni "kitengo" ambacho kipo mahsusi na kinalindwa na Dola hii ya CCM kwa lengo la kuendelea kuwabambikizia kesi za uongo wapinzani wa nchi hii, ili CCM iendelee kutawala milele!
Usijdanganye na ushahidi wa mwanzo mwanzo, labda kama huna uzoefu na dynamics za ushahidi mahakamani, kuna ushahidi utakuja kupindua meza, kuwa mpole kabla hujavuka mto
 
Huyo ni wa kundi lile wa KUDEMKA anaogopa kumgusa anaweza akaanzisha varangati hadi AKAJUTA. Ngoja tuone Mkuu pia kumbuka jamaa aligoma hadharani kumkamata Gwajiboy na wa KUDEMKA hakutia hata mguno.

Imeandikwa kwenye Biblia, kitabu cha Mithali 14:34 "Haki huinua Taifa bali dhambi ni aibu ya watu wote" mwisho wa kunukuu.

Kwa huu mwendelezo unaoendelea kutolewa mahakamani Katika kesi ya ugaidi ya akina Mbowe, hakika ni aibu kubwa Sana kwa Taifa letu kuwa na Jeshi la Polisi, ambalo halitaki hata kufuata kanuni zao zinazojulikana kwa lugha ya kigeni kama "PGO" na badala yake linajifanyia mambo kivyake, kwa ajili tu ya kuwakomoa wapinzani na kuhakikisha wanaendelea kuwabakisha nyinyi CCM madarakani.

Rais Samia utambue kuwa hii kesi ya akina Mbowe, inafuatiliwa kwa karibu Sana na Jumuiya ya kimataifa na ndiyo sababu mabalozi mbalimbali wa nchi za magharibi wanahudhuria mfululizo kesi hiyo.

Hata hivyo ni majuzi tu umerudi kutoka kwenye mkutano mkubwa wa UN, ambako uliitangazia Dunia kuwa nchi yetu ina "vibrant democracy" na inazingatia kwa hali ya juu haki za binadamu.

Hivi haki gani za kibinadamu zinazofuatwa kwenye nchi yetu kama Polisi wenyewe hawataki hata kuzifuata kanuni zao wenyewe zilizopo kwenye "msahafu" wao wa PGO??

Kama Polisi wetu wanaweza kuthubutu kutaja kwenye ushahidi kuwa watuhumiwa walikutwa na madawa ya kulevya, wakati kwenye "charge sheet" hakuna tuhuma hiyo, hivi unadhani kweli Jeshi letu la Polisi linafanya kazi yake kwa weledi??

Hao Polisi wanaweza kutueleza alipo mtuhumiwa Moses Lijenje kama siyo wamemtanguliza ahera??

Wajibu wa kwanza wa Jeshi la Polisi nchini ni kulinda uhai wa raia na mali zao, sasa inapotokea Jeshi hilo ndilo linaongoza kuwapoteza wananchi wake, maana yake limeshindwa kutekeleza wajibu wao

Kama hutaweza kumstaafisha IGP Sirro kutokana na aibu kubwa aliyoiletea Taifa, Katika kesi hii ya uonevu wa hali ya juu, ya akina Mbowe, basi tutaamini kuwa Jeshi la Polisi, ni "kitengo" ambacho kipo mahsusi na kinalindwa na Dola hii ya CCM kwa lengo la kuendelea kuwabambikizia kesi za uongo wapinzani wa nchi hii, ili CCM iendelee kutawala milele!
 
Usijdanganye na ushahidi wa mwanzo mwanzo, labda kama huna uzoefu na dynamics za ushahidi mahakamani, kuna ushahidi utakuja kupindua meza, kuwa mpole kabla hujavuka mto
LOoooh!
Hapana.

Wewe unaona ushahidi gani wa "kupindua meza" iliyotengenezwa kibabe!
Ushahidi gani utakaokuwa mzito zaidi ya njia zilizotumika isivyo kihalali kupata ushahidi huo?

"...dynamics za ushahidi mahakamani"?; hizi dynamics zitasimamia nguzo zipi?
 
Imeandikwa kwenye Biblia, kitabu cha Mithali 14:34 "Haki huinua Taifa bali dhambi ni aibu ya watu wote" mwisho wa kunukuu.

Kwa huu mwendelezo unaoendelea kutolewa mahakamani Katika kesi ya ugaidi ya akina Mbowe, hakika ni aibu kubwa Sana kwa Taifa letu kuwa na Jeshi la Polisi, ambalo halitaki hata kufuata kanuni zao zinazojulikana kwa lugha ya kigeni kama "PGO" na badala yake linajifanyia mambo kivyake, kwa ajili tu ya kuwakomoa wapinzani na kuhakikisha wanaendelea kuwabakisha nyinyi CCM madarakani.

Rais Samia utambue kuwa hii kesi ya akina Mbowe, inafuatiliwa kwa karibu Sana na Jumuiya ya kimataifa na ndiyo sababu mabalozi mbalimbali wa nchi za magharibi wanahudhuria mfululizo kesi hiyo.

Hata hivyo ni majuzi tu umerudi kutoka kwenye mkutano mkubwa wa UN, ambako uliitangazia Dunia kuwa nchi yetu ina "vibrant democracy" na inazingatia kwa hali ya juu haki za binadamu.

Hivi haki gani za kibinadamu zinazofuatwa kwenye nchi yetu kama Polisi wenyewe hawataki hata kuzifuata kanuni zao wenyewe zilizopo kwenye "msahafu" wao wa PGO??

Kama Polisi wetu wanaweza kuthubutu kutaja kwenye ushahidi kuwa watuhumiwa walikutwa na madawa ya kulevya, wakati kwenye "charge sheet" hakuna tuhuma hiyo, hivi unadhani kweli Jeshi letu la Polisi linafanya kazi yake kwa weledi??

Hao Polisi wanaweza kutueleza alipo mtuhumiwa Moses Lijenje kama siyo wamemtanguliza ahera??

Wajibu wa kwanza wa Jeshi la Polisi nchini ni kulinda uhai wa raia na mali zao, sasa inapotokea Jeshi hilo ndilo linaongoza kuwapoteza wananchi wake, maana yake limeshindwa kutekeleza wajibu wao

Kama hutaweza kumstaafisha IGP Sirro kutokana na aibu kubwa aliyoiletea Taifa, Katika kesi hii ya uonevu wa hali ya juu, ya akina Mbowe, basi tutaamini kuwa Jeshi la Polisi, ni "kitengo" ambacho kipo mahsusi na kinalindwa na Dola hii ya CCM kwa lengo la kuendelea kuwabambikizia kesi za uongo wapinzani wa nchi hii, ili CCM iendelee kutawala milele!
Unanikumbusha shambulio la risasi 36 la watu wasiojulikana ambao had I leo hawatakiwi wajulikane
 
Ni kweli jeshi la polisi Tanzania linahitaji kufanyiwa overall kubwa mno ili lifanane na majeshi mengine Kama jwtz kiutendaji na Kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa kikatiba katika utekelezaji wa majukumu Yao.
Pia ni muhimu kikaundwa chombo kingine Cha kukagua shughuli zao za Kila siku Kama ilivyo Kwa kada nyingine Kama za ualimu na uhasibu. Mfano, mwalimu anasimamiwa na mwl mkuu, afisaelimu kata, maafisa elimu wilaya na mkoa, TSC na wathibiti ubora wa elimu. Watu wote Hawa wanamkagua mwalimu mmoja TU na kuwa na taarifa zake za kazi za Kila siku na pia wanashauri, kuonya na kuathibu pale mwalimu anapokiuka miongozo ya utendaji kazi. Inakuwaje jeshi la polisi halina idara za kuwathibiti, kuwaonya na hata kuwaadhibu wasitekekeleza kazi Kwa mujibu wa pgo zao?
Nashauri, pamoja na kufumuliwa na kujengwa upya kuanzishwe chombo kingine Cha kuwakagua, kuwaonya na hata kuwaadhibu wanaotenda kazi kinyume Cha taratibu zao yaani wasiozingatia pgo ambayo ndiyo miongozo wao Kama ilivyo muhtasari wa SoMo Kwa walimu.
 
Sirro alisema wafuasi wa Chadema wanamuona Mbowe malaika, hakujua kama wenzake walicheza mchezo kwenye kesi ya kutengeneza, sasa kwa ushahidi uliotolewa naamini anakuta kutoa ile kauli yake.
Yuko kama robot sijui hata Kama anatumia reasoning kabla ya kuongea
 
Back
Top Bottom