Kutokana na madiliko ya hali ya hewa, ni muda muafaka kuwa na Wizara itakayoshughulikia Upandaji wa miti na kuzuia ukataji wa miti tu

Robert S Gulenga

JF-Expert Member
Jan 3, 2013
2,161
1,493
Ili kuweza kufikia kupanda na kukuza miti angalau bilioni 50 baada ya miaka kumi kutoka sasa, ambapo hali ya ukame inaweza kuwa ni mbaya zaidi kuwahi kutokea ni muda sahihi Serikali ikaazisha Wizara Maalum itakayoshughulikia Upandaji na ukuzaji Miti kufikia miti mipya bilioni 50, Wizara hii iwe chini ya Ofisi ya Rais.

Natambua kuna Wizara ya Muungano na Mazingira, ambapo Mh. Jafo anfanya vizuri, yawezekana kwa muundo ulivyo kea sasa si rahisi Wizara hii kupitia Taasisi zilizo chini yake kupanda na kukuza miti bilioni 50 baada ya miaka kumi ijayo.

Natambua kuna Wizara na ya Mali Asili, ambapo pia Mh. Pindi anafanya vizuri, lakini kupitia Taasisi zake kama TFS na majukumu mengine waliyonayo na wanatakiwa kukusanya maduhuli haiwezekani kusimamia kupanda na kukuza miti bilioni 50 bila kukata.

Pia Kuna Wizara ya OR-TAMISEMI, Kupitia Halmashauri wamekuwa na kampeni ya kupanda miti, sina hakika kati ya miti inayopandwa ni mingapi inasimamiwa katika namna ya kuhakikisha kuwa miti yote iliyopandwa haifi ukizingatia Halmashauri bado ina vipaumbele vingine kama kusimamia miradi ya Maendeleo na kukusanya mapato kwa ajili ya kuhudumia Wananchi.

Janga la ukame ni bomu linalokuja kulipuka, madiliko ya hali ya hewa na athari zake ni tatizo la Dunia, lakini kama nchi tunapaswa kuchukua hatua za makusudi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha tunapanda miti ya kutosha, turudishe misitu minene kila sehemu.

Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, umekuwa unasisitiza kupambana na ukame, Mh. Rais kwa unyenyekevu na ikikupendeza kama ujumbe huu utakufikia naomba tuwe na Wizara Maalum ya kushugulikia Upandaji na ukuzaji miti tu, Wizara ambayo itategemea Ruzuku ya Serikali ili isijihusishe na ukusanyaji wa mapato katika miti hiyo itakayoipanda, Wizara amabayo Waziri na Wataalam wake watakuwa site kupanda miti ili tuwe na misitu mikubwa tena iliyokuwepo huko nyuma.

Mungu ibariki Tanzania

Mungu mbariki Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan
 
Kipepeo akiruka Hongkong mabawa yake yanatibua muelekeo wa hali ya hewa Duniani.

..... Hali ya hewa sio localized issue.
 
Kipepeo akiruka Hongkong mabawa yake yanatibua muelekeo wa hali ya hewa Duniani.

..... Hali ya hewa sio localized issue.
Ni kweli mkuu pleo lakini Tanzania imeathirika saana na ukataji wa miti, tukiweza kupanda miti bilioni 50, despite kuwa hali ya hewa ni global issue lakini tunaweza punguza ukame mkubwa amabao unatunyemelea, Miti ni chanzo cha mvua
 
Kupanda miti hakuwezi kuwa suluhisho la maana kama biashara ya mkaa na kuni haitadhibitiwa na kupigiwa marufuku kabisa. Pia population control ni muhimu sana.
Ni kweli mkuu Yoda kumekuwa na ukataji mkubwa wa miti kwa ajili ya mkaa, yawezekana pia kuzuia imekuwa ngumu kwa sababu Taasisi zinazozuia zinatakiwa zikusanye maduhuli kutoka kwenye huo mkaa, ndio maana pengine ikiazishwa Wizara maalum itakayoshughulikia upandaji na ukuzaji miti na wala isitakiwe kukusanya mapato inaweza zuia hili
 
Ni kweli mkuu pleo lakini Tanzania imeathirika saana na ukataji wa miti, tukiweza kupanda miti bilioni 50, despite kuwa hali ya hewa ni global issue lakini tunaweza punguza ukame mkubwa amabao unatunyemelea, Miti ni chanzo cha mvua

Kwa taarifa yako hata Tanzania yote iwe na miti tu bila chochote ndani yake, haya mabadiliko ya tabia nchi ni ya dunia nzima.

Usitegemee ukiotesha miti Tanzania pekee ndio utaondoa huu ukame unaonyemelea dunia kwa kasi. Kibaya zaidi miti yenyewe tunayopanda sio ya asili bali ni ya kutengenezwa maabara. Miti huu haina uwezo wa kuvuta mvua zaidi ya kuwa kama Mwamvuli.
 
Kwa taarifa yako hata Tanzania yote iwe na miti tu bila chochote ndani yake, haya mabadiliko ya tabia nchi ni ya dunia nzima. Usitegemee ukiotesha miti Tanzania pekee ndio utaondoa huu ukame unaonyemelea dunia kwa kasi. Kibaya zaidi miti yenyewe tunayopanda sio ya asili bali ni ya kutengenezwa maabara. Miti huu haina uwezo wa kuvuta mvua zaidi ya kuwa kama Mwamvuli.
Yawezekana uko sahihi mkuu Tindo , lakini mpaka sasa dunia inaendelea kuchukua tahadhari namna ya kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi, moja ya hatua hizo ni Upandaji wa miti.
 
Ni kweli mkuu Yoda kumekuwa na ukataji mkubwa wa miti kwa ajili ya mkaa, yawezekana pia kuzuia imekuwa ngumu kwa sababu Taasisi zinazozuia zinatakiwa zikusanye maduhuli kutoka kwenye huo mkaa, ndio maana pengine ikiazishwa Wizara maalum itakayoshughulikia upandaji na ukuzaji miti na wala isitakiwe kukusanya mapato inaweza zuia hili

Watu wanakata mkaa kutokana na umasikini. Wanaohubiri kutokukata mkaa wao wana mapato makubwa huku wakiweza kumudu nishati zote kuanzia umeme, gas hadi solar. Na sioni watu wataachaje kutumia mkaa huku gas ikiwa inauzwa bei hii, na nishati ya umeme ni haba.

Kwa ujumla serekali yetu haina ufumbuzi wa nishati kwa bei ambayo kila mtanzania atamudu. Sana sana wataishia kufanya maigizo ya majukwaani ili kupata fedha za kupambana na mabadiliko ya tabia nchi, ili wakanunulie magari ya kifahari.
 
  • Thanks
Reactions: _ID
Yawezekana uko sahihi mkuu Tindo , lakini mpaka sasa dunia inaendelea kuchukua tahadhari namna ya kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi, moja ya hatua hizo ni Upandaji wa miti.

Miti inayopandwa ni sahihi au ni hii ya kutengeneza maabara? Nimeona sehemu nyingi inaoteshwa miti ambayo sio asili ya maeneo husika, huku miti asili ya maeneo hayo ikizidi kupotea.

Hii miti ya kutengeneza maabara ni sawa na kuweka miamvuli maeneo husika, lakini sio ya kurejesha hali ya hewa sahihi.
 
  • Thanks
Reactions: _ID
Watu wanakata mkaa kutokana na umasikini. Wanaohubiri kutokukata mkaa wao wana mapato makubwa huku wakiweza kumudu ...
Ni kweli mkuu Tindo kinachosababisha ukataji miti kwa ajili ya mkaa ni umasikini, lakini kwa namna ukame na athari zake ikiwa ni pamoja na kukauka kwa mitoo, ukosefu wa chakula, wanyama kufa, samaki kufa etc ni muda sahihi kuja na mkakati wa kukabiliana na hili kuliko kuanza kukabilina na janga kubwa huko baadaye. Yawezekana kujipanga kuangalia namna ya kutoa ruzuku kwenye gesi ili sisi Wanachi wa kawaida tuweze kumudu kutumia gesi
 
Tutaunda wizara ngapi sasa?
Hizi hapa chini ni wizara zinazohusika na miti.
1. Ofisi ya makamu wa rais Muungano (Mazingira)
2. Wizara ya maliasili
3. Wizara ya kilimo
4. Wizara ya maji na umwagiliaji
5. Mifugo?
6. TAMISEMI

Na zote zinatengewa bajeti kwa ajili ya kulinda au kupanda miti. Sasa nini mantiki ya kuja na wizara mpya? Nini kipya kitatokea?

Mimi nadhani tatizo kubwa ni kuwa serikali haijawahi kuwa serious kulinda miti na mazingira, kinachoendelea ni kampeni za kupanda miti za kisanii ili kuvuta pesa na posho. Utaambiwa kuna miti milioni moja imepandwa mikoa fulani, lakini ni miti hewa (haipo) ni takwimu za kutengeneza ili wahusika waonekane wamefanya kazi kuhalalisha upigaji wa pesa.


Sasa nini liwe suluhisho la kudumu?
Nitakuja hapa JF na mapendekezo yangu kwa kina, nadhani nitaandika thread inayojitegemea.
 
Kwa taarifa yako hata Tanzania yote iwe na miti tu bila chochote ndani yake, haya mabadiliko ya tabia nchi ni ya dunia nzima. Usitegemee ukiotesha miti Tanzania pekee ndio utaondoa huu ukame unaonyemelea dunia kwa kasi. Kibaya zaidi miti yenyewe tunayopanda sio ya asili bali ni ya kutengenezwa maabara. Miti huu haina uwezo wa kuvuta mvua zaidi ya kuwa kama Mwamvuli.
Ethiopia wanepanda miti bilioni 20 tu
ndani ya miaka 4 saivi wana mvua za kutosha na chakula cha kutosha kwa nini isiwe kwa Tanzania?
 
Miti inayopandwa ni sahihi au ni hii ya kutengeneza maabara? Nimeona sehemu nyingi inaoteshwa miti ambayo sio asili ya maeneo husika, huku miti asili ya maeneo hayo ikizidi kupotea. Hii miti ya kutengeneza maabara ni sawa na kuweka miamvuli maeneo husika, lakini sio ya kurejesha hali ya hewa sahihi.
Inawezekana tatizo ni Taasisi zinazosimamia na Upandaji wa miti pia zina lengo la kukusanya mapato, hivyo wanapanda miti ambayo ipo kibiashara zaidi au inayowahi kukomaa mapema bila kujali je inafaida kwa mazingira, kuepusha hilo, ikiwepo Taasisi au Wizara ambayo haitakuwa na lengo la kukusanya mapato itazingatia haya
 
Wazo zuri sana ila linataka muamko wa.wengi na wananchi lazima wasaidie sana kwa hili

Kwa ushauri barabara zote zipandwe miti sambamba na ujenzi wake
Miti mingi sana hukatwa pia wakati wa kuzitengeneza

Biashara ya mkaa haitaisha duniani hivi hakuna miti isiyofaa kwa mkaa tukaipanda kwa wingi
 
Ni kweli mkuu Tindo kinachosababisha ukataji miti kwa ajili ya mkaa ni umasikini, lakini kwa namna ukame na athari ...

Sioni haya matamanio yake yakifikiwa kwani walioko madarakani ni wafaidika wa hizo biashara za umeme na gas. Na pia naendelea kusisitizia kupambana na mabadiliko ya tabia nchi sio suala la Tanzania pekee, bali ni global. Na kwa mwendo huu wa kuotesha miti ya maabara ni kama kupoteza muda. Inshort dunia inaenda kufikia mwisho.

2050 ikifika hata kama miti itakuwa imepandwa mara 10 ya iliyokuwa kabla ya kuanza kuchafua mazingira, bado tatizo litakuwa ni hili hili. Suluhisho ni kuotesha miti ya asili kila eneo kwa wingi iwezekanavyo, na mipango miji ni lazima, sio kila mtu anajenga nyumba yake atakapo.
 
Hili la wanasayansi kuja na miti isiyofaa kwa mkaa kabisa ni wazo bora sana
Wazo zuri sana ila linataka muamko wa.wengi na wananchi lazima wasaidie sana kwa hili

Kwa ushauri barabara zote zipandwe miti sambamba na ujenzi wake
Miti mingi sana hukatwa pia wakati wa kuzitengeneza

Biashara ya mkaa haitaisha duniani hivi hakuna miti isiyofaa kwa mkaa tukaipanda kwa wingi
 
Inawezekana tatizo ni Taasisi zinazosimamia na Upandaji wa miti pia zina lengo la kukusanya mapato, hivyo wanapanda miti ambayo ipo kibiashara zaidi au inayowahi kukomaa mapema bila kujali je inafaida kwa mazingira, kuepusha hilo, ikiwepo Taasisi au Wizara ambayo haitakuwa na lengo la kukusanya mapato itazingatia haya

Sioni taasisi au wizara isiyojali pesa kwa sasa. Kwa ujumla nikisikia kupambana na mabadiliko ya tabia nchi huwa naona kama tunaigiza tu. Nitajie mtu au taasisi yoyote uliyoona ikikusanya mbegu za miti ya asili ili kupanda zaidi ya miti ya kibiashara.
 
Tutaunda wizara ngapi sasa?
Hizi hapa chini ni wizara zinazohusika na miti.
1. Ofisi ya makamu wa rais Muungano (Mazingira)....
Mkuu Zanzibar-ASP ni kweli kuazisha Wizara au Taasisi nyingine ni gharama kubwa, lakini hakuna gharama inayoweza kuzidi athari za mabadiliko ya tabia ya nchi kwa sasa, ni bomu kubwa saana.

Ni kweli Wizara ulizozitaja zinahusika na miti, lakini yawezekana kwa mwaka husika zimefanya shughuli nyingi zaidi za kimaendeleo kuliko Upandaji wa miti.

Changamoto ya kuwa na Wizara zaidi ya moja inayoshughulikia kitu kimoja ufanisi unaweza usiwe mzuri kama kuwa na Wizara itakayokuwa inawajibika kwa Upandaji wa miti tu, kwa sasa yawezekana takwimu zinasemwa miti imepndwa ni kweli lakini tatizo kubwa ni ufuatiliaji kuhakikisha miti iliyopandwa haifi, watu wanapanda mti na kuondoka hakuna ufuatiliaji tena.
 
Back
Top Bottom