Kutoka ndani ya moyo wangu

Kutoka ndani ya moyo wangu

Fixed Point

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2009
Posts
11,304
Reaction score
12,753
Wives uleta shida katika familia zetu na ukiwasikiliza sana unapotea
P square naona tatizo lao kubwa ni huyo mwenye mke aliye owa juzi juzi
Kabla sijaliongelea hili na-declare interest kuwa mimi ni MKE (WIFE).
Kuna ambao watadhani kuwa huu ni utetezi kwa sababu (huenda) nami nikakumbwa na hiki kimbunga siku moja.
Kutoka ndani ya moyo wangu nachukia sana sentensi kama hizi. Mara nyingi familia zinapoingia kwenye migogoro basi mtu wa kwanza kutupiwa lawama huwa ni mke wa mmoja au zaidi walioingia katika familia hiyo. Na mbaya zaidi mama katika familia hiyo anaweza kuwa mstari wa mbele kushikilia hilo, anasahau kabisa kuwa naye alikuwa mke kwenye hiyo familia. Huwa inasikitisha sana na sijui kwa nini watu wanawaza hivyo.
Napenda niwaeleze ndugu wa waume zetu kuwa sisi (wake) tunatambua umuhimu wa familia za waume zetu kuwa na umoja. Msifikirie kuwa kila kibaya ambacho mume anachokifanya kwa familia basi shinikizo linatoka kwa mkewe. Kuna wake ambao ni Blessings katika familia za waume zao, tusiendelee kuwakwaza kwa maneno kama haya.
Nawatakia uvumilivu wake wenzangu pindi tunaposikia maneno kama haya. Mungu anaona nia zetu NJEMA.
Mubarikiwe sana
 
ukweli na uongo at the same time.

Kuna baadhi ya wanawake wakiingia kwenye familia, inakuwa kama wamaeingia member alfu wa boko haramu. Sijui ni kwa kujua ama kutojua, wanachonganisha familia nzima. Hapa suluhisho huwa ni mume liyemleta boko haramu huyo, kama anajielewa ama anaweza kum-manage mkewe, mambo huwa nafuu. Ila kama ni mume -----, kasheshe, suluhisho la haraka huwa ni kkumtafutia mahali wakaishi na mkewe mbali na nyumbani, kidogo hupunguza mitafaruku. Kuna kaya jirani, waligombanishwa na wakamwana dah! Na hivi watoto wa kiume walikuwa 5, na wakamwana 5, walikuwa wanaishi jirani jirani tu. Sijui ikawaje hadi mama yao akatimuliwa sababu ya mkamwana, mjane yule akaenda kukaa kwa kijana wake mdogo wa kiume wa 6, ambaye hata hajaoa. Ila walikuwa na wifi yao aliyekuwa anaishi jirani, anauwezo wa kusutana na Dar nzima.

Na kuja shem wangu mmoja, mkewe ni kama alshaba, anagombana na mama mkwe wa miaka 80+, sijui hata anagombana naye nini. Kamfanya mumewe haelewani na mtu hata mmoja, ila mume naye ni bu sho ke tu nadhani. Basi unabaki kumhurumia tu lakini yeye anajiona mbabe wa ukoo.

Hapo kuna wanawake, ambao huwa kama baraka na chanzo cha busara kwa mume. Hata pale palipoonekana kuwa na mtafaruku, unakuta mke anafunika weakness za mmewe, labda kwa kuonyesha ushirikiano na nduguze zaidi. Hapa mfano ni wifi yangu, yale mambo ambayo braza hashiriki kabisa, kama ya kusalimia au kuuguza wagonjwa, wifi ndio mstari wa mbele, so ana cover sana hiyo weakness yake. Kiasi kwamba wao wakiwa tunashiriki kwao sababu ya wifi.

Kwa hiyo, kuna baadhi ya wake wanaleta amani, wengine kwa kweli ni hatari tupu.
 
Best, nimefurahi kukuona hapa tena. Hongera kwa majukumu.

changamoto lazma ziwepo, yupo aonaue sirini na huyo ndio wa kumfurahisha. Ila ukiona kelele zimezidi, kaa pembeni kimyaaa, afu watajofinza kwa vitendo.
Best, nami nimefurahi sana kukuona.
Najua changamoto ni lazma ziwepo lakini wasizizushe tu bila kuwa na uhakika.
Unajua nini best, kama mimi huwa nakaa pembeni mara nyingi tu ila najikuta narudi tena sababu siwezi kukaa pembeni, najua wananihitaji, lol!
Nafanya hivyo kwa ajili ya kumpendeza aonaye sirini tu na si mwingine
 
Mara nyingi lawama zinawaangukia akina mama (wanawake) pale migogoro ya kifamilia inatokotea na kufanya wao waonekane kuwa sababisho laikini si wanawake wengi wanaosababisha wakati mwingine hata wanaume ndo wanasababisha ila wa kulaumiwa ni ke sijui kwanini?
 
Mara nyingi lawama zinawaangukia akina mama (wanawake) pale migogoro ya kifamilia inatokotea na kufanya wao waonekane kuwa sababisho laikini si wanawake wengi wanaosababisha wakati mwingine hata wanaume ndo wanasababisha ila wa kulaumiwa ni ke sijui kwanini?
Trust me, mambo mengi huwa yanasababishwa na wanaume wenyewe, siyo kwa makusudi ila kwa kukosea tu kama binadamu wa kawaida, lakini lawama zooooteeeee kwa wake zao. Mi naona huwa wanatafuta mnyonge wao
 
Wana ukoo wanamjua mtoto wao alivyokuwa kabla ya kuoa. Kwa hivyo ni rahisi ku-associate mabadiliko ya tabia ya mtoto wao na mke aliyemuoa. Yapo kwa kweli, lakini pia yapo yasio ya kweli kwenye suala hili. Kwa hivyo ni vigumu kufanya generalisation (for or against).

Lakini cha msingi ni kuwa binaadamu ni dynamic na hivyo kubadilika ni sehemu ya maisha ili kuendana na mazingira na wakati. Kutegemea mtu aendelee ku behave vile vile (kwenye mambo yote) kama ilivyokuwa kabla ya kuoa, naamini sio realistic.

Ndoa zina mambo mengi sana na majukumu yanabadilika/yanaongezeka kadri umri unavyoongezeka. Wengi wetu bado hatujaikubali sana dhana ya "kutoka" kwa wazazi wetu na "kuambatana" na wake zetu. Wengi wetu tumeshindwa "kutoka" au wanaukoo hawataki "tutoke" na ndiyo sababu migogoro na malalamiko kama haya (kati ya ndugu/wazazi na mke) inaendelea kuwepo.
 
sawa...mnasaidia sana kwa uzuri na ubaya pia...ila uzuri ni mwingi zaidi, hasa ukipata mke anaejitambua...Ahsante Mungu kwa kunipa mke mwema!
Ni vizuri unaelewa kuwa una mke mwema. Ni jukumu lako kumlinda na hao ndugu.
Juzi kati kulitokea kisanga fulani kutoka kwenye familia iliyo karibu sana na sisi. Mke tunamfahamu kwa karibu sana, na mume pia. Mambo mengi huwa yanasababishwa na mume na sisi huwa tunakaa sana na huyo kaka kuongea naye. lakini cha ajabu, shutuma na matusi yoote toka kwenye familia ya mume yalielekezwa kwa mke.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mfumo dume ndiyo umeleta hayo yote...

Hata kama mume hasimamishi still mke ndo analaumiwa kuwa hazai..

Mbaya zaidi hata hizi dini za mapokeo zina ufuasi wa mfumo dume...
ha haaa, rafiki huo mstari wa pili umenifanya nicheke.......
si mpaka wajue kama nduguyo ana tatizo hilo!
 
Wana ukoo wanamjua mtoto wao alivyokuwa kabla ya kuoa. Kwa hivyo ni rahisi ku-associate mabadiliko ya tabia ya mtoto wao na mke aliyemuoa. Yapo kwa kweli, lakini pia yapo yasio ya kweli kwenye suala hili. Kwa hivyo ni vigumu kufanya generalisation (for or against).

Lakini cha msingi ni kuwa binaadamu ni dynamic na hivyo kubadilika ni sehemu ya maisha ili kuendana na mazingira na wakati. Kutegemea mtu aendelee ku behave vile vile (kwenye mambo yote) kama ilivyokuwa kabla ya kuoa, naamini sio realistic.

Ndoa zina mambo mengi sana na majukumu yanabadilika/yanaongezeka kadri umri unavyoongezeka. Wengi wetu bado hatujaikubali sana dhana ya "kutoka" kwa wazazi wetu na "kuambatana" na wake zetu. Wengi wetu tumeshindwa "kutoka" au wanaukoo hawataki "tutoke" na ndiyo sababu migogoro na malalamiko kama haya (kati ya ndugu/wazazi na mke) inaendelea kuwepo.
Umesema vema rafiki......
Watu hubadilika, hata bila kubadilishwa na wenzao. Wote tunatakiwa kulitambua hilo
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Mwanamke amchaye Bwana ndiye atakayesifiwa
Makwazo lazima yaje lakini ole wake ayasababishaye
Hekima ya mwanamke/mwanaume hujulikana zinapotokea changamoto
"...kumcha Bwana ndiyo chanzo cha hekima"
Amina.......
Tatizo mara nyingi zinapotokea changamoto huwa tunahukumu kabla hatujasikilizia kuona hizo hekima za watu wetu
 
Back
Top Bottom