Kutoka February 16 2010-mpaka February 16-2021 hapa Jamii Forums

KakaKiiza

JF-Expert Member
Feb 16, 2010
11,581
8,601
KUTOKA FEBRUARY 16-2010-MPAKA FEBRUARY 16-2021

MIAKA KUMI NA MOJA(11) KATIKA MTANDAO BORA TANZANIA WA JAMII FORUMS.


Leo ni siku ambayo kwangu naiona kama siku ya kishujaa muno,Nasema hivyo kwakuwa nimeweza kutimiza miaka 11 katika huu mtandao nimekuwa mwanafamilia wa huu mtandao,JF kama wengi wetu tumezoea kuiita naipenda na nitaendelea kuipenda kawa sababu nyingi ila moja kuu ni kunikutanisha na watu wengi sana tofauti kimawazo na kiitikadi,pili ni sehemu niliweza kupata maarifa mengi,na mengine naendelea kuyatumia katika kuendesha Maisha yangu!.Pia najivunia kujulikana na watu wengi unaposema KakaKiiza ukweli kati ya watu mia moja (100) wa JF jina hilo halikosi hivyo basi nikitu cha kujivunia kuwa na marafiki wengi kuliko maadui. JF ni sehemu ukiitumia vema basi utafahamu mambo mengi sana na pia utanufaika sana na JF.

Kuna mambo mengi kama binafsi nimenufaika nayo hasa kikubwa ni kuwa na network kubwa katika maswala ya kibiashara na kijamii katika nchi hii nan je ya nchi,na kwa mikoani nikifika nakutana na makundi ya JF yenye ukarimu mkubwa. Hii leo nitatoa shukurani za pekee katika WING YA ARUSHA YOU’RE SO AMAIZING WING EVER! Nawapongeza sana kwani naikumbuka 2014. Mlinikaribisha nikawajoin maandalizi yalikuwa mazuri sana nikafahamiana na nyinyi kwa ukaribu tukawa kama ndugu na tunaendelea kuwa ndugu na tutaendelea kuwa ndugu!Niwaombee pumziko la amani waliotangulia mbele ya haki Mungu awarehemu wote.

Pia katika kitu ambacho siwezi kusahau ni JF siku nilipopatwa Msiba mzito wa Marehemu mke wangu 2012. Niliweza kufarijiwa na watu wengi wanaJF kimawazo nawashukuru kila uchao wana JF.Nitakuwa mnyimi wa fadhira endapo nitamaliza bila kusema Asante kwa Uongozi mzima Jamii Forum Asanteni leo sina mengi.Nimengi sana ya kuyaeleza juu ya Jamii Forums
 
Itategeme Malengo yako na huu mtandao lakini watu ambao ni clean hatuogopi kukutana na watu hapo nyuma tulikuwa na utamaduni kila mwaka mpya tunaangusha party kubwa hivyo ambao tulikua na mioyo safi tuliinjoy sana Mtambuzi naomba uniitie lara1 tulianzishe tena!
Hapana aiseeee!
Nje ya hapa jukwaani huwa najifikiria mara mbili mbili,
Watu wema hawapo siku hizi, hivyo tufanyiane mzaha hapahapa jukwaani!
 
Kudos sana mkuu.

11 years!!!
Without ban.

What a milestone in this giant network!!!!!

Wengine tunaiga kwako kaka na rafiki.

Urafiki uliozaliwa na platform hii hii.
Tuko pamoja mkuu.
Mkuu tupo pamoja itabidi baada ya hii makitu yanitwa corolla sijui corona tutaomba kwa Maxence Melo tuombe kuoganaizi party la nguvu kwani nisiku nyingi hii kitu aijafanyika tujumuike tujiulize mengi sana nakumbuka tulianzishaga hadi miradi tukaishia kurushiana pesa ila sina uhakika mradi wa kilimo kama ulitake off as we speak au na wao walirudishiana pesa ila kwa sasa tupo uchumi wa kati linazungumzika tunaweza tukaanza upya kwani kwa sasa watu wapo serious na maisha kipindi kile watu walikuwa wakikaa home wanapiga pesa ila kwa sasa lazima usumbue ubongo!
 
Mafano ningekutana na Asprin wapi ila hii jf au Mtambuzi Jiwe Linaloishi Ben Mugashe Arushaone Dark City niwengi sana.
Hongera sana mdogo wangu kwa umri JF. Ni kweli wengi tumenufaika na mengi hapa. Mathalan mie sijawahi kujuta kufahamiana na member yeyote hapa. Tumeishi kama ndugu kuanzia kwenye pen names mpaka majina ya kweli na maisha halisi..

Big up JF

Ila bazazi mbona hujazungumzia ulivyokuwa unaniibia michuchu yangu niliyokuwa naikagua? Ngoja nikufichie siri kwa sasa
 
Hivi huyu KakaKiiza hajawahi kukusarandia? Sema tu ukweli mimi ni mvumilivu sana.

Jamaa sina imani nalo baada ya kuona liko close sana na Amber Rutty. Sijui likikuwa linamfundisha kwaya?... I dunno...


Aaahahahahahahhaaaa Baaaabuuuuuu....

Nimesoma ujumbe wako ghafla nimepata kiwi na kunywa Amarula.....😋

Sijui nikujeee saa hii tufanye chiazii....😉.

Uzuri wake sijawahi kukaa Kigamboni, hivyo niko salama kabisa kwa KKza, hakuna ukaguzi mwingine nimefanyiwa zaidi ya ukaguzi wako 😋😜.

Mishiii yuuuu.
 
Hongera sana mdogo wangu kwa umri JF. Ni kweli wengi tumenufaika na mengi hapa. Mathalan mie sijawahi kujuta kufahamiana na member yeyote hapa. Tumeishi kama ndugu kuanzia kwenye pen names mpaka majina ya kweli na maisha halisi..

Big up JF

Ila bazazi mbona hujazungumzia ulivyokuwa unaniibia michuchu yangu niliyokuwa naikagua? Ngoja nikufichie siri kwa sasa
We Babu upo?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom