Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Sii woga,
1. It is a political strategy! Wewe unadhani Slaa mwoga kuongea Bungeni? Mbona huyu jamaa mahiri sana hutoa hoja to challenge serikali?

2. Yaliyomtokea Zitto yaliwapa somo- CHADEMA wakaona wajipange vizuri! Slaa anaona akiongea na wananchi directly hoja yake itasikika- nao wananchi waatapata ukweli! Siasa you always assess strategies and move foward!
 
Mimi nitamuelewa mh Slaa iwapo atatueleza kwamba ameito hoja hiyo bungeni ili kuiboresha na kuisuka zaidi hoja hiyo halafu airudishe bungeni,na si tu eti anaiondoa bungeni kwenda kushitaki kwa wananchi, sijui anataka sisi wananchi tufanyeje, kwani sisi tuna mamlaka ya kuunda kamati kuchunguza suala hilo?

Hakuna umuhimu wowote wa kupeleka hoja katika bunge uchwara la CCM ambalo limeweka mbele maslahi ya chama chao kuliko maslahi ya Watanzania waliowachagua. Ndio bunge hilo hilo limekaa kimya katika kashfa mbali mbali zilizoibuka/zinazoibuka Tanzania katika miaka ya karibuni kuanzia IPTL, Net Group Problems, BOT, mikataba ya madini, Mkapa kufanya biashara Ikulu, Ununuzi wa ndege ya Rais, Rada, Magari na helicopter za jeshi, Richmonduli, Mkataba unaonuka rushwa na unaotishia kuifilisi TANESCO wa Kiwira Coal mining n.k.

Kasha zote hizo hilo Bunge uchwara halikufanya lolote ili kutetea maslahi ya Tanzania na Watanzania, sasa hii hoja hata kama ingefikishwa huko kwenye Bunge uchwara unadhani kungekuwa na mabadiliko gani!? If you have nothing important to say, it is better to keep quiet!!!
 
Mkjj alifanya naye maongezi kwenye simu hivi karibuni HAPA. Kwa jinsi Mkjj alivyo uliza maswali na jinsi Dr.Slaa alivyojibu, mimi kwa kweli namhisi/mwona huyu ni miongoni mwa wanasiasa wachache wa kuaminika kwa sasa... sijui hapo awali pia siwezi kujua mbeleni...lakini kwa sasa namwamini.

Kuhusu uhakiki wa source of information, ni kitu ambacho nawatakia watu wote wazingatie, si yeye tu. Wakati wote kutakuwepo na makosa ya hapa na pale, lakini muhimu ni kuwa na tahadhari.

SteveD.
 
Sii woga,
1. It is a political strategy! Wewe unadhani Slaa mwoga kuongea Bungeni? Mbona huyu jamaa mahiri sana hutoa hoja to challenge serikali?

Mzalendohalisi ,Ni politicla stratergy gani ambayo ni dhahiri haipeleki katika kusolve tatizo kwa kina? hebu niambie solution ya tatizo la kuliwa pesa za bot litapatikana vipi? bila kupitia bungeni? Au mheshimiwa Slaa haliamini Bunge? Na kama haliamini Bunge anendelea kukaa bungeni kufanya nini?

Yaliyomtokea Zitto yaliwapa somo- CHADEMA wakaona wajipange vizuri! Slaa anaona akiongea na wananchi directly hoja yake itasikika- nao wananchi waatapata ukweli! Siasa you always assess strategies and move foward!
CHADEMA kujipanga vizuri hilo swala halina mjadala,kama kujipanga vizuri ni kwa kuondoa hoja bungeni ili kuipitia upya halafu tena kuirudisha bungeni hapo mimi nakubali,lakini kuiondoa hoja mahala husika ambako ni bungeni bila malengo ya kuirudisha ni dhahiri kutaka kuia hoja hiyo na kisha kujikosha kwa wananchi eti kwa kuwashitakia.kama hii hoja haitapelekwa kujadiliwa bungeni hakutakuwa na stratergy yeyote ya msingi yenye malengo ya maslahi ya taifa. badala yake zitakuwa ni kaulimbiu za kisiasa zisizo na mantiki yeyote kwa maslahi ya nchi yetu
 
Duh! Ukimya wa Bunge uchwara kuhusiana na kashfa nyingine chungu nzima zinazohusu maslahi ya Watanzania huuoni! lakini unaona hili la Slaa kuondoa hoja Bungeni! Ama kweli ukipenda, chongo utaita....
 
Gamba la Nyoka,
Naomba usikilize Majibu ya Dr.Slaa HAPA ili uone maoni yake kwa hili swala unaloendelea kulishuku... Naona mengi unayo yahoji yameshajibiwa na yeye mwenyewe. Au haukubaliani na majibu yake binafsi? Ahsante.

SteveD.
 
Sasa wewe unamongelea huyo muimba taharabu? wote wanafanana na mwenzie muimba kwaya ndugu komba! Adhabu ya sharia imeshamuhukumu, kwani mwizi na anayetetea mwinzi adhabu yao ni kukatwa mkonoo!
 
Lowassa kuwekwa ‘kitimoto’ bungeni?

WAZIRI Mkuu, Edward Lowassa, huenda sasa akalazimika kujibu maswali ya papo hapo kutoka kwa wabunge, kutokana na kuanza kutumika rasmi kwa kanuni mpya za Bunge zilizofanyiwa marekebisho makubwa.

Wakati hayo yakitokea, wabunge kadhaa wameonya kuwa wakati umefika sasa kwa Bunge kuacha kukwepa wajibu wake wa kuisimamia serikali, kwani kwa kufanya hivyo Bunge linajipotezea hadhi yake.

Wakizungumza na gazeti hili jana kabla ya kikao chao cha kupatiwa maelezo kuhusu mkutano wa 10 wa Bunge unaoanza leo, wabunge hao walisema ‘urafiki’ unaojengeka baina ya Bunge na serikali hauwezi kulisaidia taifa.

Wengi wa wabunge hao waliokuwa wa upinzani walibainisha kuwa hoja zinazotolewa na kambi hiyo bungeni hazilengi katika kufanya siasa, kwani siasa zikiingizwa bungeni nchi haitasonga mbele.

Kutokana na hali hiyo, walitaka kutokuwapo kwa ubabaishaji wakati kanuni ya Waziri Mkuu kujibu maswali itakapoanza kutumika, na kusema kuwa hiyo itumike kama fursa ya kutoa maelezo kuhusu matatizo ya wananchi yatakayoulizwa na wabunge kwa niaba yao.

Hata hivyo, ingawa hiyo ni moja ya kanuni mpya zilizoingizwa kwenye toleo jipya la Kanuni za Bunge, jana haikuelezwa kinagaubaga iwapo itaanza kutumika mara moja sambamba na kanuni nyingine.

Kanuni hiyo ya Waziri Mkuu kujibu maswali ya moja kwa moja, imenukuliwa kutoka Bunge la Uingereza kulikotengwa muda maalumu kwa wabunge kumuuliza Waziri Mkuu maswali kuhusu mambo mbalimbali.

Kwa kawaida, maswali yanayoulizwa bungeni huwa yamewasilishwa muda mrefu uliopita katika wizara husika na watendaji kuyatafutia majibu yanayosomwa bungeni.

Ofisa Habari Mkuu wa Bunge, Ernest Zullu, jana alithibitisha kuanza kutumika kwa kanuni mpya na kusema kuwa kanuni iliyothibitishwa kuanza kutumika ni ile ya wabunge kuimba wimbo wa taifa katika mkutano wa kwanza.

“Kanuni zimeshakamilika ingawa hazijachapishwa, baadhi yake zitaanza kutumika mara moja na itakayoonekana mapema ni ile ya wabunge wote kuimba wimbo wa taifa...wabunge wataimba wote kwa maneno wimbo huo mara baada ya maandamano ya Spika,” alisema Zullu.

Hata hivyo, Zullu alisema kuwa katika masuala yaliyozungumzwa katika kikao cha faragha cha wabunge wote jana mchana, haikuelezwa iwapo kanuni hiyo ya Waziri Mkuu kujibu maswali nayo itaanza kutumika.

Alisema kwamba kilichojadiliwa na kukubalika katika kikao hicho cha wabunge ni kuanza kutumika kwa kanuni ya kuimba wimbo wa taifa pamoja na ile ya mavazi.

Aidha, Zullu alithibitisha kuwa ripoti ya Kamati Teule ya Bunge, iliyoundwa na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kupitia mchakato wa mkataba wa kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond Development (RDC) ya Marekani, itawasilishwa bungeni.

“Ripoti imeshakamilika na kama mnavyofahamu ilishawasilishwa kwa Spika. Imethibitishwa kuwa ripoti hiyo itawasilishwa bungeni katika mkutano huu na ikiwasilishwa document (nyaraka) hiyo itakuwa ni ya wazi...iwapo wabunge wataamua kuijadili watafanya hivyo,” alisema Zullu.

Pamoja na ripoti ya Richmond, pia Bunge litapokea taarifa za kamati zikiwasilisha kazi zake kwa kipindi cha mwaka 2007. Ripoti hizo zinaweza kujadiliwa na wabunge iwapo wataona umuhimu wa kufanya hivyo.

Kwa upande mwingine, mjadala kuhusu ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) unatarajiwa kuwa mkali hasa kutokana na kawaida ya ripoti hizo kuonyesha upotevu mkubwa wa fedha za serikali.

Mwaka jana, Rais Jakaya Kikwete aliagiza kuwa ripoti hiyo iwe inajadiliwa kwa kina katika ngazi mbalimbali ili kupata dawa ya upotevu wa fedha za serikali. Inatarajiwa kuwa wabunge watakitumia kikao hiki kutekeleza agizo hilo kwa lengo la kuisaidia serikali.

Majibu ya maswali 210 yameshaandaliwa na yanatarajiwa kutolewa katika mkutano huo wa 10 utakaodumu kwa wiki tatu. Sambamba na kujibiwa kwa maswali hayo, pia miswada kadhaa ya sheria itawasilishwa na kujadiliwa.

Wakati huo huo, Mchungaji Getrude Rwakatare anatarajiwa kuapishwa leo. Rwakatare anaingia bungeni kwa mara ya kwanza leo kupitia Viti Maalumu, kuziba nafasi iliyoachwa wazi na marehemu Salome Mbatia, aliyekuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.
 
Wacha tungoje mambo tuone moto utakavyo kuwa mkali huko Bungeni. Lowasa ataweza kweli ama watakalia hili hadi mwaka 2010?
 
hakuna cha maana hapo,ni mbunge gani anaweza kumuuliza swali EL, zaidi ya wawili watatu tena kwa kumpongeza ktk kufanikisha kumaliza tatizo la umeme na kujenga shule nyingi kama ilani ya uchaguzi inavyosema.
 
hakuna cha maana hapo,ni mbunge gani anaweza kumuuliza swali EL, zaidi ya wawili watatu tena kwa kumpongeza ktk kufanikisha kumaliza tatizo la umeme na kujenga shule nyingi kama ilani ya uchaguzi inavyosema.

Peleka swali kwa mbunge wako!!! umwambie amuuze PM, akashindwa weka barazani tujadili,

Play your part first!!!
 
NAdhani hiyo itakuwa njia bora ya kumfanya EL kuachia ngazi kwa hiyari kutokana na moto utaomwakia au hata kwa kushinda kutoa majibu sahihi kwa Wabunge. Tusubiri wakti mwafaka.
 
Mwisho wa Tanzania ,ikiwa mambo yamefikia katika kuimbishana ,kweli hatuna wajenzi tuna wasanii.Bora siku ya kwanza spika atoe sapraiz ,aimbe mmoja mmoja uwone vioja.
 
NAdhani hiyo itakuwa njia bora ya kumfanya EL kuachia ngazi kwa hiyari kutokana na moto utaomwakia au hata kwa kushinda kutoa majibu sahihi kwa Wabunge. Tusubiri wakti mwafaka.

Ibrah:

Your Idea is powerfull and finaly if all wont work.... Tutatafuta njia nyingine..ref thread ya petition ya kumuondoa EL
 
Lowasa kujiondoa kwa maswali mazito ni msamiati mzito kwa wana CCM wale wa Bungeni.
 
NAdhani hiyo itakuwa njia bora ya kumfanya EL kuachia ngazi kwa hiyari kutokana na moto utaomwakia au hata kwa kushinda kutoa majibu sahihi kwa Wabunge. Tusubiri wakti mwafaka.

Usinifurahishe mie... majibu ayatoe wapi? kama alishindwa jibu la swali la mtoto wa darasa la saba?? atweza kweli kujibu maswali yaliyotoka kwa vichwa kama Slaa?? hapa wanatuletea ze comedy ya bure... labda wasiwe wanaonyesha live!
 
hakuna cha maana hapo,ni mbunge gani anaweza kumuuliza swali EL, zaidi ya wawili watatu tena kwa kumpongeza ktk kufanikisha kumaliza tatizo la umeme na kujenga shule nyingi kama ilani ya uchaguzi inavyosema.

Wanasiasa wetu wa ajabu mno jamani sijui wanalaana ama wamelogwa vitu vivyo wazi kwa maslahi ya taifa hawavipi umuhimu kabisa sintoshangaa comedian EL akaishiwa kupongezwa kwa kuleta mvua za Thailand...ujinga ujinga tu mradi mambo yanaenda
 
nyie hamjui lowasa anajua kuongea maneno 10,000 kwa dakika na baadaye sana ndo anakuja kugundua amesema kitu gani.... lol
 
Back
Top Bottom