Kuteua Waziri mwanamke Wizara ya ulinzi ni sawa?

Hakuna kitu kibaya kama kuishi zama za ujima kifikra huku kimwili upo 2021.Kenya,South Africa,Macedonia, Spain,Netherlands na France ni mojawapo ya Nchi duniani zenye mawaziri wa ulinzi wanawake.Hao wenye fikira hizo fikiria wamelelewa na mama zao na bado wana mawazo kama wanaishi miaka 100 iliyopita.Kinachoangaliwa ni uwezo wa mtu sio jinsia yake.Kuna wanaume wengi wameaminiwa kwenye nafasi kubwa kubwa na wamekuwa failure kiutendaji na kiuongozi. Karibu wauaji viongozi na madikteta wote ni wanaume lakini hakuna anayenasibisha uwezo wao mdogo na ukatili wao na jinsia yao.
 
Nadhani mmeelewa kwanini baada ya Samia kurudi kutoka UN Dr.Mpango anasema eti aliogopa sana kubaki ofisini bila uwepo wa rais maana huenda kuna jambo lingetokea alafu angewajibika yeye.
 
Hii ni gender role stereotype...! Duniani kuna wanawake wangapi wamekuwa Mawaziri wa Ulinzi? Tuache hii notion ya patriarchy system...
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Idadi ya wanajeshi wanawake nchini ni ndogo sana. Wizara hii ni kama ni ya kiume zaidi katika muundo wake. Wanaume ni zaidi 90% ya askari wote. Kuwawekea Waziri mwanaume ni sawa na Wizara ya wanawake, jinsia na watoto kumteua mwanaume awe Waziri wao. Hii haifanyiki hata huko Marekani na uingereza na duniani kote walikoendelea.

Kwanini usawa huu wa jinsia usianzie kwanza kwenye kupata elimu, kilimo, uvuvi, uchimbaji, usafirishaji, uhandisi, sheria ya ndoa, na maisha ya kawaida?

Huwezi kuwezi kuweka Waziri mwanamke kwenye wizara ya uvuvi wakati 99% ya wavuvi ni wanaume.a
Aliyekwambia uvuvi na ulinzi ni kitu kimoja ni nani?. Masalia ya mfumo dume hamtaki kuamini kwamba mwanamke anaweza kuongoza wizara ya ulinzi, subiri mpate majibu yenu.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Nyie mnaoona ubaguzi ni kitu kibaya ndio nyie nyie huwa tunaungana hapa kubagua mashoga,kama mnafikiri ubaguzi ni kitu kibaya kabisa na kila mtu ana haki basi hata mashoga tusingewabagua nao tuwachukulie kama sisi tu.
Msingi wa unachokisema haupo kisheria.
Sheria zetu haziruhusu mahusiano ya kimapenzi ya watu wa jinsia moja.
 
Idadi ya wanajeshi wanawake nchini ni ndogo sana. Wizara hii ni kama ni ya kiume zaidi katika muundo wake. Wanaume ni zaidi 90% ya askari wote. Kuwawekea Waziri mwanaume ni sawa na Wizara ya wanawake, jinsia na watoto kumteua mwanaume awe Waziri wao. Hii haifanyiki hata huko Marekani na uingereza na duniani kote walikoendelea.

Kwanini usawa huu wa jinsia usianzie kwanza kwenye kupata elimu, kilimo, uvuvi, uchimbaji, usafirishaji, uhandisi, sheria ya ndoa, na maisha ya kawaida?

Huwezi kuwezi kuweka Waziri mwanamke kwenye wizara ya uvuvi wakati 99% ya wavuvi ni wanaume.
Huu ni ubaguzi tu ,mwanamke Kama anaweza apewe,shida tu Kama aliepewa ni kilaza
 
Idadi ya wanajeshi wanawake nchini ni ndogo sana. Wizara hii ni kama ni ya kiume zaidi katika muundo wake. Wanaume ni zaidi 90% ya askari wote. Kuwawekea Waziri mwanaume ni sawa na Wizara ya wanawake, jinsia na watoto kumteua mwanaume awe Waziri wao. Hii haifanyiki hata huko Marekani na uingereza na duniani kote walikoendelea.

Kwanini usawa huu wa jinsia usianzie kwanza kwenye kupata elimu, kilimo, uvuvi, uchimbaji, usafirishaji, uhandisi, sheria ya ndoa, na maisha ya kawaida?

Huwezi kuwezi kuweka Waziri mwanamke kwenye wizara ya uvuvi wakati 99% ya wavuvi ni wanaume.
Taliban kazini
 
Msingi wa unachokisema haupo kisheria.
Sheria zetu haziruhusu mahusiano ya kimapenzi ya watu wa jinsia moja.
Na ndio ubaguzi ambao tumeutengenezea sheria kabisa kwa maana ni ubaguzi ambao tumeuhararisha.
 
Tumia simu yako muangalie Mwana Mama Florence Parly,ana cheo gani huko France,kisha njoo uedit thd yako kua haijawahi kutokea Duniani Mwanamke kuongoza wizara ya Ulinzi.
Mwanamke sio tatizo, tatizo ni kwanini unamuweka pale na sio pale, Usimuweke kwakuwa Wizara ile haijawahi kuongozwa na mwanamke, Sasa ni zamu yetu. Hayo yatakuwa ni mashindano na malalamiko dhidi ya wanaume. Maana yake siku Rais akiwa mwanaume atawatoa wanawake na kuweka wanaume wenzake
 
Kila nikangalia kwenye hii thread ni Kama vile sioni mantiki kabisa zaidi ya ubaguzi tu.Ubaguzi ni ubaguzi hauchagui rangi,dini,kabila ama jinsia nayeyote anayeufanya ni KABURU haijalishi awe mweusi,mzungu,mchina au mtanzania mwenzetu ni KABURU TUUUUUUU......
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Mwanamke sio tatizo, tatizo ni kwanini unamuweka pale na sio pale, Usimuweke kwakuwa Wizara ile haijawahi kuongozwa na mwanamke, Sasa ni zamu yetu. Hayo yatakuwa ni mashindano na malalamiko dhidi ya wanaume. Maana yake siku Rais akiwa mwanaume atawatoa wanawake na kuweka wanaume wenzake
Kwani Mkuu,wewe una uhakika gani kua kawekwa kwenye hicho cheo coz jinsia yake?
Je kuna sheria kua wizara hiyo isiongozwe na Mwanamke?
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Rais cheo kikubwa zaidi ya waziri unajiuliza ni sawa huko mbona wapo Mageneral Wakina Mama kama General Mwakipunda huku wanaume hata mgambo hawajapita...Jinsia na utendaji ni vitu viwili tofauti kabisaa..
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Kila nikangalia kwenye hii thread ni Kama vile sioni mantiki kabisa zaidi ya ubaguzi tu.Ubaguzi ni ubaguzi hauchagui rangi,dini,kabila ama jinsia nayeyote anayeufanya ni KABURU haijalishi awe mweusi,mzungu,mchina au mtanzania mwenzetu ni KABURU TUUUUUUU......
Wewe huoni kama Kuna malalamiko dhidi ya wanaume kuziongiza wizara kwa muda mrefu? Ndio maana nasema background yetu na Mila zetu ziangaliwe wakati wa kuangalia uwezo, sifa na jinsia ya viongozi. Twende Polepole hasa kwenye wizara nyeti
 
Background zetu na mila zetu zipi?Zitaje.Unaiishi kwenye mfumo dume wa kuangalia jinsia kwanza na uwezo baadaye.Una watoto wa kike?Umewapeleka shule?Hamia Afghanistan mkuu mawazo yako na mila zako zinafanya kazi kule.Wanaangalia vigezo kwanza uwe mwanaume mengine kama akili,uwezo,elimu yatafuata baadaye kama kweli unazo hizi sifa.Unaposema twende polepole una maana gani?Miaka 60 haitoshi?Kwanza tumechelewa sana.Unaishi kwenye karne gani kifikra??
 
Hii ni gender role stereotype...! Duniani kuna wanawake wangapi wamekuwa Mawaziri wa Ulinzi? Tuache hii notion ya patriarchy system...
Na hizi notions ndizo zinazotuachia umaskini wa kutupwa. Ukitaka mafanikio ni lazima ujaribu mtu ambaye sio sehemu ya business as usual.

Mawaziri wanaume ndio hao kila siku wanaanzisha vita zisizokwisha, wamejawa na kiburi mpaka kinawapofua macho wanashindwa kuona.
 
Background zetu na mila zetu zipi?Zitaje.Unaiishi kwenye mfumo dume wa kuangalia jinsia kwanza na uwezo baadaye.Una watoto wa kike?Umewapeleka shule?Hamia Afghanistan mkuu mawazo yako na mila zako zinafanya kazi kule.Wanaangalia vigezo kwanza uwe mwanaume mengine kama akili,uwezo,elimu yatafuata baadaye kama kweli unazo hizi sifa.Unaposema twende polepole una maana gani?Miaka 60 haitoshi?Kwanza tumechelewa sana.Unaishi kwenye karne gani kifikra??
Polepole ninamaanisha
Hii ni gender role stereotype...! Duniani kuna wanawake wangapi wamekuwa Mawaziri wa Ulinzi? Tuache hii notion ya patriarchy system...
Zipo tabia ambazo ni kwa wanyama wote walioumbwa na Mungu zinazohusu me na ke kwenye kundi. Hizi ziko hivyo.

Kama tunataka usawa endelevu/sustainable, hatuna budi usawa huu uanzie kwenye ngazi za chini za jamii zetu na upande juu Polepole huku tukiendelea kujifunza na kuuzoea usawa huo. Usawa huu uanzie kwenye kaya watoto wa kike waonekane wakicheza mpira wa miguu, kuranda mbao, kuchomelea vyuma, kuvua, kuchunga, kuendesha bodaboda, kukwepa minazi, uongozi wa mitaa, vijiji, kata, taarafa na wilaya. Maana huko ndio kwenye chimbuko la usawa wa kijinsia. Shida yetu ni kwamba usawa huu unaanzia ngazi za juu kama ubunge wa viti maalum, uDC, RC na uwaziri, usawa wa aina hii una maatawi na majani lakini hauna shina na mizizi kwenye jamii, ni rahisi sana kunyauka maana unategemea zaidi hisani, huruma na upendeleo maalum. Ndio maana wanawake ni wengi sana lakini viongozi ni wachache bila sababu ya wazi.
 
Na hizi notions ndizo zinazotuachia umaskini wa kutupwa. Ukitaka mafanikio ni lazima ujaribu mtu ambaye sio sehemu ya business as usual.

Mawaziri wanaume ndio hao kila siku wanaanzisha vita zisizokwisha, wamejawa na kiburi mpaka kinawapofua macho wanashindwa kuona.
Sawa kabisa, Mimi nyumbani kwangu Nina watoto wa jinsia zote, lakini siwabagui kwenye kuwapangia majukumu na Wala sitaji kabisa jinsia ya watoto wakati namwambia nenda kaoshe gari, nenda kasimamie mafundi, nenda kamwagilie, nenda kaoshe vyombo, nenda kaogeshe mbwa, mbadilishe diaper mdogo wako. Yaani sisemi na nyie wavulana nendeni mkapike Leo maana dada zetu wamekuwa wakipika kila siku. Nikifanya hivyo itaonekana kama wasichana wamenilalamikia kuhusu kaka zao.

Hivyo watoto wangu tangu awali wanafahamu kwa baba utafanya kaazi zote.
 
Na hizi notions ndizo zinazotuachia umaskini wa kutupwa. Ukitaka mafanikio ni lazima ujaribu mtu ambaye sio sehemu ya business as usual.

Mawaziri wanaume ndio hao kila siku wanaanzisha vita zisizokwisha, wamejawa na kiburi mpaka kinawapofua macho wanashindwa kuona.

Polepole ninamaanisha

Zipo tabia ambazo ni kwa wanyama wote walioumbwa na Mungu zinazohusu me na ke kwenye kundi. Hizi ziko hivyo.

Kama tunataka usawa endelevu/sustainable, hatuna budi usawa huu uanzie kwenye ngazi za chini za jamii zetu na upande juu Polepole huku tukiendelea kujifunza na kuuzoea usawa huo. Usawa huu uanzie kwenye kaya watoto wa kike waonekane wakicheza mpira wa miguu, kuranda mbao, kuchomelea vyuma, kuvua, kuchunga, kuendesha bodaboda, kukwepa minazi, uongozi wa mitaa, vijiji, kata, taarafa na wilaya. Maana huko ndio kwenye chimbuko la usawa wa kijinsia. Shida yetu ni kwamba usawa huu unaanzia ngazi za juu kama ubunge wa viti maalum, uDC, RC na uwaziri, usawa wa aina hii una maatawi na majani lakini hauna shina na mizizi kwenye jamii, ni rahisi sana kunyauka maana unategemea zaidi hisani, huruma na upendeleo maalum. Ndio maana wanawake ni wengi sana lakini viongozi ni wachache bila sababu ya wazi.
Nimekuelewa, unachojadili sasa ni culture. Unapojadili gender roles mara nyingi huwa tunajadili culture siyo biological factor. Kuna tofauti ya gender na sex. Sex ni universal na ni biological factor na gender ni historically social constructed ambayo ina differ kutoka jamii moja na nyingine.

Tamaduni zetu nyingi za Kiafrika zinaongozwa na mfumo dume, ambao ndiyo huo umejenga hadi hizo gender role stereotypes. Kwamba labda kazi hizi ni za wanaume hizi za wanawake. Hii ni primitive notion. Ninachojua, wapo wanawake wanaweza kufanya kazi nzuri ambazo tunaamini zinapaswa kufanywa na wanaume.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Nimekuelewa, unachojadili sasa ni culture. Unapojadili gender roles mara nyingi huwa tunajadili culture siyo biological factor. Kuna tofauti ya gender na sex. Sex ni universal na ni biological factor na gender ni historically social constructed ambayo ina differ kutoka jamii moja na nyingine.

Tamaduni zetu nyingi za Kiafrika zinaongozwa na mfumo dume, ambao ndiyo huo umejenga hadi hizo gender role stereotypes. Kwamba labda kazi hizi ni za wanaume hizi za wanawake. Hii ni primitive notion. Ninachojua, wapo wanawake wanaweza kufanya kazi nzuri ambazo tunaamini zinapaswa kufanywa na wanaume.
Gender kwa afrika zinaanza kupewa mkazo kuanzia chini kabisa. Wasichana wenye akili wakimaliza shule na kufaulu badala ya kuendelea mbele wanalazimishwa kuolewa, haya ni madhara ya masuala ya gender.

Wasichana wanakutana na unyanyapaa wa kila aina maofisini, haya ni madhara ya masuala ya gender kijamii.

Huyu Mama alipokabidhiwa cheo ikulu rais aliongea ni kwanini kampa yeye cheo kwa uzoefu alioupata huko SADC, tumuache apige kazi.
 
Back
Top Bottom