kibanda ameteswa na waajiri wake wa mwanzo ambao hakuagana nao vizuri baada ya kuacha kazi kwao
Kweli kwa ulichokiandika ni form four leaver 2012 Pole sana kama huna cha kucomment pls:tape2:
kibanda ameteswa na waajiri wake wa mwanzo ambao hakuagana nao vizuri baada ya kuacha kazi kwao
kubenea mwenyewe ni mzigo kwa taifa, ina maana hapo anashangilia na kufurahia kibanda kuumizwa.........shame on him
Naomba mtu anihabarishe...hivi kiujumla waandishi wa habari wanaopitia humu JF wana mawazo gani? Umoja wa waandishi wa habari upo kweli? Ndugu zangu mkiwaacha hawa manyang'au yatambe tu iko siku yatawapata na nyie. Kalamu mnazo na kalamu ndizo silaha zenu...kazi kwenu.
Gazeti
la Mwanahalisi lilikuwa linamilikiwa na Saed Kubenea lilifungiwa miezi
kadhaa iliyopita kwa sababu ambazo hazikuwekwa wazi iosipokuwa tu
uchochezi kufuatana na barua aliyoandikiwa na idara ya Maelezo.
Barua haikueleza ni uchochezi upi isipokuwa tu
inaaminika kutokana na habari gazeti lilikuwa likiandika kuhusiana na
kutekwa na kuteswa Ulimboka.
Mwanahalisi lilianza kufanikiwa kupata undani wa wa
kutekwa na kuteswa kwa mwanaharakati huyo kwani kidole kilianza
kuonyesha Ikulu kwa maana afisa mmoja wa usalama (TISS) ndiye mhusika
mkuu.
Baada ya kufungiwa Jujwaa la Wahariri (TEF)
lilimuona Kubenea ni mkosaji kwa kuandika habari zile na lilimtaka
akubali kosa kwa kuandika habari ambazo wengi wa wajumbe wa TEF katika
kikao kimoja waliona ni za majungu na wengine hata kudiriki kusema
Kubenea alikuwa anakwenda kinyume cha maadili ya uandishi.
TEF ilimtaka Kubenea ashirikiane na Jukwaa hilo ili
kumuombea kwa serikali gazeti lifunguliwe mradi tu kwanza akubali hilo
kosa lake.
Kubenea aliipuuza TEF kutokana na msimamo wake huo
wa ajabu na alikuwa anasusia vikao vyake.
Sasa hili la Kibanda limetokea ni kama lile lile la
Dr Ulimboka ikizingatiwa ile pattern ya tukio. Sasa sijui TEF
watawapinga wote wale watakaokuwa wanaandika habari kwa undani za
kuteswa kwa Kibanda kama habari hizo zinaonyeshea kidole wahusika ambayo
inaaminika ni wale wale waliomfanyia unyama Ulimboka?
Kwa maneno mengine ni kwamba iwapo wahariri
watagundua ukweli kuhusu kuteswa kwa Kibanda watatakiwa kufunga midomo
yao?
Kwa mtazamo wangu naona Kubenea amewaumbua sana TEF.
Nawasilisha
Naomba mtu anihabarishe...hivi kiujumla waandishi wa habari wanaopitia humu JF wana mawazo gani? Umoja wa waandishi wa habari upo kweli? Ndugu zangu mkiwaacha hawa manyang'au yatambe tu iko siku yatawapata na nyie. Kalamu mnazo na kalamu ndizo silaha zenu...kazi kwenu.
Kubenea ni mwandishi asiyeyumba, anaandika anachokiamini kwa sababu anafanya uchunguzi na kupata uhakika wa habari anyoiandika. Mwanahalisi ni gezeti pekee ambalo liliandika hahari kuhusu 11 shame names na kuwataja kwa majina baada ya mkutano ule wa mwembe yanga. kwakweli nalikosa sana Mwanahalisi. Ila DR. kikwete asidhani kuwa ccm itatawala milele na hivyo kitakuwa kichaka chake milele!!!!1
Kubenea ni muislamu japo anaishi maisha kama ya yesu kwani pamoja na kejeli na mateso hakuyumba hadi alipouokoa ulimwengu
mnaishia kumfariji kubenea jukwaani, mpelekeeni hela ya kula. tef ndo walishamtema hivyoo!. Sa si bora hata awe anahudhuria vikao vya tef apate bahasha, anajifanya ana misimamo!
Yaani wewe kwa uandishi huu lazima una zero...... Wewe ndie mzigo kwa taifa manake miaka yako minne umeipoteza bure kabisa....... Heri ungeimba bongo fleva sahizi ungekuwa mbali sana kimaisha........ Shame on you