Kutenguliwa Uafisa Habari ACT-Wazalendo

Kutenguliwa Uafisa Habari ACT-Wazalendo

hivi huwa hamna shughuli zingine nje ya siasa?
 
Mkuu hayo yote uliyoyabainisha kama makosa au sababu ya kutumbuliwa kwako kwa kufupi inaitwa njaa ya kichwa na akili kuhamia tumboni.
 
Pongezi kwa kuwa mzalendo, siku zote exercise thinking freedom inayobeba uzalendo kwanza daima
 
Siasa sio uadui jamani, kuleni mapapai , kondoo na mbuzi havina korona.
 
Ulifanya kosa kusifia upuuzi wa chama kingine hata kama ulikuwa nje ya page za chama chako. Huwezi kuona manager wa kitengo chochote cha Samsung anaisifia au hata kuijadili Huawei mbele ya watu. Mijadala hiyo ni confidential na inatakiwa kufanyika nje ya macho ya watu. Lini uliona Polepole anajadili mafanikio ya CUF? Sijui walikuokota wapi, tena cheo cha Afisa Habari unatakiwa uepuke makosa kama haya.
Kumbe ukiwa ndani ya chama unakuwa mtumwa?

Sasa tunalaumu nini kuhusu Polepole kutetea chama chake?
 
Mpaka tuje tuipate demokrasia ya kweli ni kazi sana udikteta umetamalaq kwenye vyama vya upinzani!
 
Walipashwa wakufukuze na chama
Hypocrite
Hamkawii kuunga juhudi za kipuuzi
Pongezi my foot
Well done ACT
FUKUZA tu wanafiki
 
Kumbe ukiwa ndani ya chama unakuwa mtumwa?

Sasa tunalaumu nini kuhusu Polepole kutetea chama chake?
Kama hataki utumwa anzishe chama chake. By the way ule sio utumwa, hakuburuzwa kupewa cheo ndo maana haijatumika nguvu kumtoa. Kuhusu mlevi Polepole kutetea chama chake, kumbe Covid-19 alipoifananisha na upinzani ni msimamo wa CCM?
 
Sufian Juma, pole kwa yaliyokukuta.

Sintaongea juu ya kutenguliwa wadhifa wako kwa kuwa siifahamu Katiba wala Kanuni za ACT.
Umesema hukujua kama ni kosa 'kumpongeza JPM kwa juhudi alizochukua kuikabili Corona'.

Naomba nikuulize swali.
Kwa nini JPM anasema tufuate maelekezo ya Wataalam wetu wa Afya wakati Wataalam wenyewe wamepigwa marufuku kuuelimisha umma?

Profesa Mohamed Janabi aliongea mambo yenye manufaa sana juu ya janga hili, kilichofuatia alinyamazishwa mpaka zikaenea tetesi za kufukuzwa kazi.

Uliyemtakia kheri, Mwigulu, amesikika akisema Corona iwe siri ya Taifa.
Je, ni kweli kheri hiyo uliitoa wewe mwenyewe, ukiwa na akili timamu, bila kushinikizwa na mtu yeyote, au kitu chochote?

Sufian, ninaomba majibu
 
Back
Top Bottom