Kutapeliwa

Kutapeliwa

Hii nchi wajinga mtachelewa sana kuisha,hata wanao utawaambukiza huo uzuzu.
 
Hiyo huduma ya Jamaa ambayo kimsingi ni kama geresha ina shabihina na huduma ya "NMB CARDLESS" ambapo pesa unaenda kutoa moja kwa moja toka ATM kwa kuingiza namba ya aliyekutumia, hizo code kisha kiasi.

Sasa hatari yake, kama huo muamala uko valid, watu wameshachomoa pesa, maana Jamaa ka expose kila kitu..
Yeah ni kweli hyo huduma ipo nmb pesa faster unatoa pesa kwenye ATM bila card unatoa kwa kutumia code tu!
 
Yaani akutumie pesa kwenye namba ya simu ila pesa ukachukulie bank!!! Kuna huduma ya hivyo kweli?

Pole we!
Hudum hyo ipo mkuu Nmb pesa faster unatoa pesa bila kuwa na card y bank unatoa kwa kutumia pin Kama hzo kwe SMS aliyotumiwa lakin hyo SMS ni fake!
 
Advanced huu utapeli hizi si private no, wahuni wamesha chonga za kupigia watu mjini.
 
hela ikitoka bank inaingia kwenye akaunt moja kwa moja na unatoa kwa wakala wa mtandao husika, sasa hiyo ya kwenda kutoa kwenye bank tena ni suala jipya,

2. Miamala yote ya pesa za mtandao lazima zinakuja na namba ya muamala(risiti) ya Huduma uliyofanya amabyo inaambatana na muda was kufanyika huo muamala, wewe hii yako haina namba ya risiti/muamala

3. jaribu kutembelea wakala wa nmb kama unaweza pata msaada, lakin kwakuwa umeshaanika siri utakuwa umeshaikosa hela

4. Mwambie jamaa yako aliyepokea hiyo hela kama hakuna namba ya simu kwenye phonebook yake kaisave yake kama hakuna mtu amemsave kama NMB.

5. Kama ana muda angilie vizuri centre number ya msg ilyoingia kama ya kutoka nmb au namba ya kawaida
 
Hampo serious na neno pesa!..ohh hata iweje siwez kosea
Tuseme nini kwenu tena wanawake?

Kiasili mwanamke akili yake imetulia.

Waliohusishwa kupewa taarifa na waume zao juu ya jambo linalotarajiwa kufanywa, likawa na harufu ya utapeli ndani yake, mara nyingi husaidia mno kuwashitua waume zao.

Lakini wanaume wasiopenda kuhusisha wake zao kwenye mambo yao ya pesa, mara nyingi hupigwa kimya kimya na kubakia na 'donda ndugu'.
 
Tuseme nini kwenu tena wanawake?

Kiasili mwanamke akili yake imetulia.

Waliohusishwa kupewa taarifa na waume zao juu ya jambo linalotarajiwa kufanywa, likawa na harufu ya utapeli ndani yake, mara nyingi husaidia mno kuwashitua waume zao.

Lakini wanaume wasiopenda kuhusisha wake zao kwenye mambo yao ya pesa, mara nyingi hupigwa kimya kimya na kubakia na 'donda ndugu'.
mbona wanawake ndo rahisi kutapeliwa
 
Wakuu habari yenu, jana kuna kitu nlimuuzia jamaa fulani hv. Yeye alisema yuko mkoani, so ikabidi tufanye arrangements ili tukutane na ndugu yake alieko Dar uko, ili nimpe mzigo wake.

Baada ya yule ndugu yake kuuona na kuridhika, ikabidi ampigie mteja wangu kwamba mzigo uko vizuri. Nikawa nimeongea nae akasema atanitumia kwenye number ya airtel iko kiasi tulichokua tumekubaliana. Kwa kua mimi sina number ya airtel ikabidi nimwambie rafiki yangu kuwa kuna muamala utatumiwa kwenye simu yake maana yeye ana line ya airtel.

Basi, kama baada ya dakika nane yule rafiki yangu anaetumia line ya Airtel akanambia ameona pesa imeingia kutokea NMB. Mimi nikasema sawa, nikamkabidhi yule ndugu yake mzigo tukaachama pale.

Ile message inaonekana imetokea NMB, kwamba katumia huduma ile ya benki mkononi kunitumia hela. Basi, kwa kua ilikua ni jioni sana hata mabenki yalikua yamefungwa nikasema asubuhi ya leo nitawahi bank nikaihangaikie. Cha ajabu nafika bank wananiambia hakuna muamala wa dzain hiyo kwa benki yao. Sikukata tamaa ikabidi niwacheki pia kwa mitandao yao ya kijamii (instagram) ila majibu yakawa ni yale yale.

Mteja wangu nliefanya naye biashara, wakati niko bank nilikuwa najaribu kumpigia ila hakupatikana, ila dakika 20 kabla ya kuanza kuandika huu uzi nlijaribu kumpigia akasema ngoja amcheki wakala ambae alimtumia kunitumia hiyo hela. Ndo niko namskilizia hapa.

Naombeni ushauri kama kuna mtu anaweza kuwa na idea na hiki kitu au anaeweza kuwa na wazo lingine anisaidie wakubwa.

Natanguliza shukrani.

View attachment 1488552View attachment 1488553
MUWE MNATOA ZAKA

USHAURI KAMILI AKUNA SLOPE KWENYE MAISHA BILA MUNGU UKIPOKEA HURUDISHI KWAKE WATAKUJA MADUMADU KAMA HAWA WANAKUNYOOSHA MKUU

KATUBU KAMA ZAKA HUTOI NA KAMA SADAKA UMEKUWA MBAILI NAKO TUBU BAADAYAHAPO MUNGU ATAFUNGUA MIRIJA MINGINE UTAPATA ZAIDO
 
Asante kwa kutambua ujinga wangu Kuhusu kumpa account, Soma vizuri tena boss. Ilikua jioni, so banks pia zilikua zishafungwa. Na pia nisingekubali aje akanitumie labda kesho yake. Ingekua ngumu ndugu yangu
Pole brother, achana na watu wasio na ufikirio
 
Back
Top Bottom