Kutapeliwa

Kutapeliwa

MREJESHO.
Nashukuruni nyote mlonisaidia kwa mawazo na michango, ishu inaelekea kukamilika about 70%.

MPANGO WA KUFATILIA
Ilikua hivi last week tarehe flani nliamua nianze kuifatilia hii ishu, maana kipindi chote iko nlkua sifatilii wala sikuwahi kumpigia tena jamaa.

Sasa hyo tarehe nlienda kituoni nikaandikisha maelezo vizuri tu, wakaniomba nijaribu kuelezea description ya jamaa alivo nikawaambia vyote nnavovikumbuka kuhusu expression yake. Color, urefu, mwili..nk. Maana walinambia cases kama hizo za kutapeliwa kwa dzain hiyo zishafikishwa kama tatu kituoni pale na watuhumiwa hao wa utapeli namba zao wako nazo polisi pale, kwa hiyo mimi nlichotakiwa ni kuleta namba ya yule jamaa nlomkabidhi mashine ili nijaribu kulinganisha ni ipi kati ya namba zile.
Kwa kua siku hiyo sikutoka na namba ya jamaa ilibidi siku ya pili yake niende niwapelekee hyo namba. Bahati mbaya yule anaehusika na hizo namba hakuepo, nikasema sawa.

KUFIKA KITUONI
Sasa juzi jumatatu nikasema ngoja niende niwapelekee namba maana nilikua nishachonga na afande mmoja hivi aakanambia huyo jamaa anaehusika na hizo namba za matapeli leo atakuwepo. Basi nimefika pale nikaambiwa jamaa bado hajafika na atachelewa kuja kwa hiyo cha kufanya ni either niondoke nirudi baadae au nimsubirie. Basi nikajikaza nikasema nitamsubiri.

USO KWA USO NA TAPELI
Ikapita kama nusu saa hivi kuna jamaa alifika pale nlipokuepo ila sikua nimemuona alivoingia, basi me nikawa naendelea kufanya mambo yangu huku nimeangalia upande mwingine maana sikumtilia maanani. Kidogo akanambia kaka vp (alijua ni askari pale) nikamwambia fresh tu, nlvomuangalia hivi sura kumbe ndie yule jamaa aloagizwa kuja kuchukua ule mzigo, basi na yeye akawa amenikumbuka pale pale, akawa anarudi nyuma ili ajiandae kukimbia..amepiga hatua kama tatu hivi nikamshika mkono (maana kwa mwili wake mdogo asingewezea kunichoropoka) basi nikatembea nae hadi kwa afande mmoja pale nikamwambia ishu ilivokua, akabaki anafurahia mwenyewe.

Basi maaskari wakamuhoji pale akakubali kua mashine aliichukua, ila alivoichukua alimpelekea yule mshkaji wake alomtuma aje aichukue (yule ambae alinitafuta tufanye biashara).

Basi chap tukachukua gari hadi jamaa anapokaa (maana tulienda nae uyo tapeli), kufika tukamkuta jamaa. Ila mshkaji akagoma kwamba yule dogo hakumpa mashine. Ikabidi tumchukue pale twende nae kituoni. Wakaendelea kumueka virungu huko ila bado hakukubali. Basi ikabidi wamuweke lock up. Ikawa usiku umeingia nikaondoka.

Leo nimeongea na dada yake(alichukua namba yangu jana) akasema aliweza kuongea nae na akakubali kua mashine aliichukua, ila aliiuza na hamkumbuki aliemuuzia ni nani. Ko akanambia hapo itabidi wapambane wanipe tu hyo hela au waninunulie mashine ingine.

Mimi kama mimi sitaki kesi, ninachohitaji tu ni jamaa anilipe hela yangu au mashine tu basi mambo yaishe. Lakini sitaki apate dhamana, itabidi ndugu zake wapambane mpaka waipate hyo hela...then wakishaipata yote ndo mambo mengine ya kuachiliwa yafuate.

Asanteni sana kwa ushauri wenu na critiques, na matusi (kwa wachache wale). Naamini tutaendelea kua familia. Nakaribisha maswali, maoni na hoja.

"I rest my case"
 
Wakuu habari yenu, jana kuna kitu nlimuuzia jamaa fulani hv. Yeye alisema yuko mkoani, so ikabidi tufanye arrangements ili tukutane na ndugu yake alieko Dar uko, ili nimpe mzigo wake.

Baada ya yule ndugu yake kuuona na kuridhika, ikabidi ampigie mteja wangu kwamba mzigo uko vizuri. Nikawa nimeongea nae akasema atanitumia kwenye number ya airtel iko kiasi tulichokua tumekubaliana. Kwa kua mimi sina number ya airtel ikabidi nimwambie rafiki yangu kuwa kuna muamala utatumiwa kwenye simu yake maana yeye ana line ya airtel.

Basi, kama baada ya dakika nane yule rafiki yangu anaetumia line ya Airtel akanambia ameona pesa imeingia kutokea NMB. Mimi nikasema sawa, nikamkabidhi yule ndugu yake mzigo tukaachama pale.

Ile message inaonekana imetokea NMB, kwamba katumia huduma ile ya benki mkononi kunitumia hela. Basi, kwa kua ilikua ni jioni sana hata mabenki yalikua yamefungwa nikasema asubuhi ya leo nitawahi bank nikaihangaikie. Cha ajabu nafika bank wananiambia hakuna muamala wa dzain hiyo kwa benki yao. Sikukata tamaa ikabidi niwacheki pia kwa mitandao yao ya kijamii (instagram) ila majibu yakawa ni yale yale.

Mteja wangu nliefanya naye biashara, wakati niko bank nilikuwa najaribu kumpigia ila hakupatikana, ila dakika 20 kabla ya kuanza kuandika huu uzi nlijaribu kumpigia akasema ngoja amcheki wakala ambae alimtumia kunitumia hiyo hela. Ndo niko namskilizia hapa.

Naombeni ushauri kama kuna mtu anaweza kuwa na idea na hiki kitu au anaeweza kuwa na wazo lingine anisaidie wakubwa.

Natanguliza shukrani.

View attachment 1488552View attachment 1488553
Pole sana mkuu. Ukisimamia hili vizuri utamkamata huyo tapeli. Kwanza kama sio meseji ya nmb itakuwa na namba ya mtu binafsi pale mwisho wa hiyo msg.

Jaribu kuweka hela kwenye hiyo namba iliyokutumia msg. Pata jina la mpokeaji. Nenda polisi umchukulie RB huyo mwenye hiyo namba. Huyo ndiye atakaye kulipa hela yako. Fatilia, nadhani kuna kitengo cha polisi maalum cha wizi wa kupitia simu -sina uhakika- sasa hivi simu zote zimesajiliwa kwa alama ya vidole. Mwenye simu atapatikana. ata kama ametupa laini mtandao unaweza kutoa namba za watu wa karibu waliokuwa wanawasiliana na hiyo namba yake. Hawa wakibanwa watamtaja.
Mwenye kusajili hiyo laini ndiye atakaekulipa hela sababu alimsajilia mwizi laini, kumaanisha anamfahamu.
 
Back
Top Bottom