Kushushwa kwa viwango vya ufaulu.

Tasia I

JF-Expert Member
Apr 21, 2010
1,223
193
Wakuu,
Samahanini sana kama niko sana nyuma litaarifa, ila kuna hili suala la kushushwa kwa viwango vya ufaulu, naamini wengi tulilisikia na kulifuatilia kwa karibu na kuliewewa, isipokua wengi naamini hatukukubaliana nalo. Hatukukubaliana nalo kwa kua kwa logic rahisi sana, maelezo yaliyotolewa kua ndio sababu ya kushushwa viwango hivyo yalikua haya "make sense". Haya make sense kwa kua, sababu ya jumla/kuu iliyotajwa ya kushushwa viwango hivyo ni "kuboresha elimu" lakini ukiangalia hatua hii matokeo yake yatakua kuiporomosha elimu na kuiangamiza kabisa.

Swali langu la msingi hapa ni kua, hili suala limeishia wapi? na kama lipo vilevile, nini ni hatma ya Elimu ya nchi hii? je wananchi kama wananchi tuna nafasi gani katika suala hli? na je tumeitumiaje katika kutetea elimu ya nchi hii?

Asanteni.
 
Back
Top Bottom