Kushindwa uchaguzi ni pamoja na kuibiwa kura, kulikoni kulia lia

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,878
35,876
Penye ukweli pasi na kujali kambi ni heri kuusema. Vinginevyo tutaendelea kutwanga maji kwenye kinu milele.

Hongereni CCM Kwa kushinda chaguzi zenu na kama mabwege yakiendelea kulaza damu kazeni uzi hapo hapo.

Kwani malengo ya chama cha siasa nini? Si walisema "the end justifies the means?" Wacha walie lie mkiona yamelala au yako kihasara hasara nyie endeleeni kupita na kura kama vipi, zote kabisa!

Kwa hakika aliyelala usimwamshe.

Kwani nani aliwaambia CCM ni charity organization au hata kuwa ni watangaza dini?

Kutwa kucha wanalia wameibiwa chaguzi. 2024 na hata 2025 kama 2029 na 2030 watalia hivyo hivyo kama wamerogwa tu.

Nani ajuaye labda wao ni wapinzani wa kudumu. Kwamba walishajikatia tamaa au labda ndiyo iliyo core business yao?

Kwani hata wanachukua hatua zipi za maana kuona kuwa sasa au kesho wanaweza kushinda vipi? Kwamba iko wapi mikakati yao ya ushindi? Kwamba wako kusherehekea nyomi mikutanoni mwao, zisizotafsirika kwenye uwanda wowote wa maamuzi?

Kama ndivyo nini tofauti ya vyama hivi na kina TLP, CHAUMA, CUF, au hata na DP ya leo?

Kwenye uwanja wa mapambano mbinu zote dhidi ya adui ni halali. Yaani mbinu safi na hata chafu (overt and covert) zote ruksa. Kumbe sisi tunategemea kushinda kwa kudra za Mola? Kama ndivyo ni heri tukajisajili rasmi kwa akina Mwamposa, Lusekelo au hata kina Mwaipopo huko. Kwa mtaji huo tukawe tayari kupokea vibao shavu moja baada ya jingine bila ya kunung'unika.

Hivi huwa tunajihoji sawa sawa ndani kwa ndani au hata nje kwa nje? Kutambua tuko kamili na kweli tumedhamiria? Tunajua hii ni vita, siyo lelemama? Ya kwamba kama ilivyo kwa kumwua nyani hatupaswi kumwangalia usoni?

Bravo: TAL, Mwabukusi, Dkt. Slaa, Dkt. Nshala, Kamanda Mdude na nyote mliodhamiria kweli kweli.

Kwa hakika mlipo tupo!

Pumzika kwa amani Rev. Christopher Mtikila kama wale hukupata kupoa.
 
Ukiwa chama kinachokubalika hata ukiibiwa kura wananchi watakutetea. Ukiona unaibiwa kura na mambo yanaenda kama kawa jua kuwa "haushtui." Kosa ni lako.
 
Ukiwa chama kinachokubalika hata ukiibiwa kura wananchi watakutetea. Ukiona unaibiwa kura na mambo yanaenda kama kawa jua kuwa "haushtui." Kosa ni lako.

Hasa unapokuwa na wanachama 8m+ na waliopiga kura jumla hawafiki 15m
 
Penye ukweli pasi na kujali kambi ni heri kuusema. Vinginevyo tutaendelea kutwanga maji kwenye kinu milele.

Hongereni CCM Kwa kushinda chaguzi zenu na kama mabwege yakiendelea kulaza damu kazeni uzi hapo hapo.

Kwani malengo ya chama cha siasa nini? Si walisema "the end justifies the means?" Wacha walie lie mkiona yamelala au yako kihasara hasara nyie endeleeni kupita na kura kama vipi, zote kabisa...
....unakanyaga mafuta na break kwa pamojaee.... 😜 si mchezo!!!
 
Nimekusoma nikajikuta nacheka kama mazuri, kila siku kulia lia kama tuliambiwa CCM ni charity organisation!

Umeniamsha usingizini, kumbe huu wimbo wa CCM wameiba kura unatakiwa kufa automatically, kama CCM kuiba kunawawezesha wao kufikia malengo yao ni wazi wataendelea kuiba no matter what!.

Kama wakiendelea kuiba, nasi tukiendelea kulia wanaiba, kumbe CCM ndio wenye faida kwa sababu wanakuwa tayari wameshayafikia malengo yao, huku sisi wakulia lia ndio tunaendelea kutwanga maji kwenye kinu kila siku!.

Hapa tukubaliane tu ukweli mchungu, kama hatuwezi kuwazuia CCM kutuibia kwa vitendo, na sio kwa kulia lia kama ilivyozoeleka, bora tuwaache waendelee kututawala wapendavyo.
 
....unakanyaga mafuta na break kwa pamojaee.... 😜 si mchezo!!!

Tufike mahali tuelezane ukweli. Chama hata tovuti zake hakuna updates, hata vi online TV bora vya kina AYO. Macho sasa yapo kwenye ubunge 2024/25 kwa Katiba hii hii. Nini tofauti na kina Bulaya?
 
Nimekusoma nikajikuta nacheka kama mazuri, kila siku kulia lia kama tuliambiwa CCM ni charity organisation!

Umeniamsha usingizini, kumbe huu wimbo wa CCM wameiba kura unatakiwa kufa automatically, kama CCM kuiba kunawawezesha wao kufikia malengo yao ni wazi wataendelea kuiba no matter what...

Walisema penye nia pana njia. Tunashindwa vipi kuweka mikakati ya ushindi tukashinda? Kwa hakika si Kwa kulia lia. Tufike mahali tukubaliane kuibiwa na kukwiba ni sehemu ya mchezo. Kulia lia iwe marufuku!
 
Tufike mahali tuelezane ukweli. Chama hata tovuti zake hakuna updates, hata vi online TV Bora vya kina AYO. Macho sasa yapo kwenye 2024/25 kwa Katiba hii hii. Nini tofauti na kina Bulaya?
hapo sasa umekanyaga mafuta zaidi break kidooogo....🤓

Ila for sure, unayo hoja ya maana. Ni mwanasiasa uchwara pekee anaweza puuza ukweli huu na kisha akaendelea kusota huko chiniiii....

Only jabali la siasa makini can take this work for it...
 
Walisema penye nia pana njia. Tunashindwa vipi kuweka mikakati ya ushindi tukashinda? Kwa hakika si Kwa kulia lia. Tufike mahali tukubaliane kuibiwa na kukwiba ni sehemu ya mchezo. Kulia lia iwe marufuku!
Mikakati ya ushindi mara zote huwekwa, bahati mbaya hatuna uvumilivu wa kuisimamia mpaka matunda yaonekane.

Unapokuwa na mipango ya hakuna uchaguzi mpaka Katiba Mpya ipatikane, halafu ghafla wengine miongoni mwenu wanaanza kusema 2025 lazima nitamtoa fulani jimbo fulani, hayo kwangu ndio maandalizi ya vilio vya nimeibiwa kura...
 
hapo sasa umekanyaga mafuta zaidi break kidooogo....🤓

Ila for sure, unayo hoja ya maana. Ni mwanasiasa uchwara pekee anaweza puuza ukweli huu na kisha akaendelea kusota huko chiniiii....

Only jabali la siasa makini can take this work for it...

Tuko pamoja mkuu. Ninadhani pa kuanzia tunahitaji chaguzi huru kwenye hivi vyema. Ziwe primaries huru kweli kweli chini hadi juu.

Tukiwekeza kwenye demokrasia kamili kina Mussa na kina Haruni wapo wengi kulivusha jahazi.
 
Tuko pamoja mkuu. Ninadhani pa kuanzia tunahitaji chaguzi huru kwenye hivi vyema. Ziwe primaries huru kweli kweli chini hadi juu.

Tukiwekeza kwenye demokrasia kamili kina Mussa na kina Haruni wapo wengi kulivusha jahazi.
sure, pamoja sana brazaj
 
Mikakati ya ushindi mara zote huwekwa, bahati mbaya hatuna uvumilivu wa kuisimamia mpaka matunda yaonekane.

Unapokuwa na mipango ya hakuna uchaguzi mpaka Katiba Mpya ipatikane, halafu ghafla wengine miongoni mwenu wanaanza kusema 2025 lazima nitamtoa fulani jimbo fulani, hayo kwangu ndio maandalizi ya vilio vya nimeibiwa kura...

Mikakati ya ushindi isiyotekelezeka haina maana yoyote.

Nani hao waliokuwa wakubwa kuliko maamuzi yenye maslahi mapana ya chama? Kulikoni wanavumiliwa?

Nini tofauti ya kuwa na mikakati ya ushindi isiyotekelezeka au kutokuwa nayo?

Angalia CCM walivyokuwa na mikakati ya ushindi:

F4sPKnNWEAAexEo.jpeg


Kwa hakika hawalali hawa!

Kongole kwao.

Sisi je?
 
Penye ukweli pasi na kujali kambi ni heri kuusema. Vinginevyo tutaendelea kutwanga maji kwenye kinu milele.

Hongereni CCM Kwa kushinda chaguzi zenu na kama mabwege yakiendelea kulaza damu kazeni uzi hapo hapo.

Kwani malengo ya chama cha siasa nini? Si walisema "the end justifies the means?" Wacha walie lie mkiona yamelala au yako kihasara hasara nyie endeleeni kupita na kura kama vipi, zote kabisa!

Kwa hakika aliyelala usimwamshe.

Kwani nani aliwaambia CCM ni charity organization au hata kuwa ni watangaza dini?

Kutwa kucha wanalia wameibiwa chaguzi. 2024 na hata 2025 kama 2029 na 2030 watalia hivyo hivyo kama wamerogwa tu.

Nani ajuaye labda wao ni wapinzani wa kudumu. Kwamba walishajikatia tamaa au labda ndiyo iliyo core business yao?

Kwani hata wanachukua hatua zipi za maana kuona kuwa sasa au kesho wanaweza kushinda vipi? Kwamba iko wapi mikakati yao ya ushindi? Kwamba wako kusherehekea nyomi mikutanoni mwao, zisizotafsirika kwenye uwanda wowote wa maamuzi?

Kama ndivyo nini tofauti ya vyama hivi na kina TLP, CHAUMA, CUF, au hata na DP ya leo?

Kwenye uwanja wa mapambano mbinu zote dhidi ya adui ni halali. Yaani mbinu safi na hata chafu (overt and covert) zote ruksa. Kumbe sisi tunategemea kushinda kwa kudra za Mola? Kama ndivyo ni heri tukajisajili rasmi kwa akina Mwamposa, Lusekelo au hata kina Mwaipopo huko. Kwa mtaji huo tukawe tayari kupokea vibao shavu moja baada ya jingine bila ya kunung'unika.

Hivi huwa tunajihoji sawa sawa ndani kwa ndani au hata nje kwa nje? Kutambua tuko kamili na kweli tumedhamiria? Tunajua hii vita Siyo lelemama? Ya kwamba kama ilivyo kwa kumwua nyani hatupaswi kumwangalia usoni?

Bravo: TAL, Mwabukusi, Dkt. Slaa, Dkt. Nshala, Kamanda Mdude na nyote mliodhamiria kweli kweli.

Kwa hakika mlipo tupo!

Pumzika kwa amani Rev. Christopher Mtikila kama wale hukupata kupoa.
Ng'ombe
 
Back
Top Bottom