Kura ya maoni: Zitto vs Dr Slaa

Kura ya maoni: Zitto vs Dr Slaa

Ni nani ungependa agombee urais mwaka 2015 kwa tiketi ya CHADEMA?

  • Zitto Z. Kabwe

    Votes: 180 15.3%
  • Wilbrod P. Slaa

    Votes: 996 84.7%

  • Total voters
    1,176
  • Poll closed .
Status
Not open for further replies.
mnamlinganisha Zito Na Slaa! Zito si saizi ya dr Slaa, mpigieni kura Zito Na mafisadi wenzake kwenye chama chake cha CCM kinachomtuma kuvuruga harakati za watanzania kujikomboa kutoka kwenye makucha ya wakoloni weusi.
 
Jaman slaa ndio kila kitu cos ni mwanasiasa jasiri sana asiyependa kutumiwa bali kutumikia kwa manufaa ya watz wote,slaa juu,chadema oyeee!!!
 
Nasikitika sana kuona hadi kipindi hiki cha sayansi na teknolojia kuna watanzania wasiojua kujibu swali au kuchangia mada, nawafananisha na viongozi wanaoingia madarakani na kusahau majukumu yao. Mtoa mada ni binadamu kama mimi na wewe, na sidhani kama alikua na lengo baya kuleta mada kama hii, ni nzuri na inaleta changamoto, cha msingi ni kuchangia kwa kwa ufasaha kama watanzania tulio na akili timamu sio kukurupuka na hoja zisizo na msingi. Nashangaa sana kuona wachangiaji wanaoingiza mada za udini au ukabila.
kURA
Kura yangu naiweka kwa Dr. Slaa
Ni kiongozi mwenye uzoefu wa muda mrefu kuliko Mh Zito,
Umri wake ni ndani ya sheria na si wa kuhitaji tena mambo ya ujana
Si mtu anaependa sifa zisizo na msingi
Hapendi kushukuriwa kwa jambo ambalo ni wajibu wake

Mtoa mada angenipa nafasi ningetoa sababu za ziada ila kwa kuwa aliweka kigezo naishia hapo.
 
Kwanza napenda kusema kuwa ZITTO ni kijana safi mchapa kazi muwajibikaji na mpenda mageuzi.
Ila kama nitaambiwa nipendekeze mgombea wa URais 2015 kwa CDM nitampendekeza DR SLAA
SABAU KUU NNE:
1. Kwa DR Slaa si Muoga kufanya maamuzi !
2. DR anauzoefu Zaidi
3. Zitto Tumpe muda walau 5 years za kuongeza Umri
4. Zitto wa sasa amepungua makali kidogo katika swala la kuiwajibisha CCM!
 
Kura yangu inatua kwa Dr. Slaa: 1. Ni kiongozi aliyejipambanua kua anaweza fanya maamuzi magumu kwa manufaa ya wote 2. Ni mwanasiasa mwenye uzoefu kuliko Zito 3. Anajiamini kwa kile anachokifanya akiwa na mkakati kamili wa jambo husika 4. Umri unaruhusu kwa taasisi ya urais tofauti na Zito.
 
Jamani! Hizi kelele zote za nini,humu ndani hata robo ya watakaopiga kura hatufiki ila tumeng'anga'na kupandiza chuki.msimamo wa chama nani anaujua? Katiba ya chadema inajieleza pia.chama bado kina vita na magamba hebu tukiimarishe kwanza raisi wananchi watajichagulia....hapa mkirudi mseme mnakokaa wenyeviti wa mitaa wangapi ni chadema huo ndo ushindi.
 
Mimi kama mwana harakati ninaye amini katika nguvu ya umma,nasema Zito Z Kabwe ni mtu wa kuangaliwa kwa makini maana haeleweki yuko upande upi!kama ni chadema damu basi namshauli awe na nidhamu,Dr,Slaa ndiye tegemeo la watanzania kwa sasa tunataka kiongozi kwanza na sio mtawala!Hivyo watu wenye usisiem kwasasa hatuwahitaji kabisaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!??????????.
 
Zitto bado kijana mdogo ila anauchu na madaraka, hivyo huwezi mfananisha Slaa Zitto labda akagombea kwao Kigoma.
 
Dr Slaa,mtu makini.unajua ili uweze kuongoza unahitaji vitu muhimu vifuatavyo:Kwanza ujitambue,pili uamini unacho amini,tatu usiegemee upande katika maamuzi,nne uzalendo iwe ndiyo dira yako na mwisho amani ya kweli na sio utulivu tu ndani ya ufisadi!!!!!!!!!!!?????????
 
None of the above! probaly Lowasa BUT he should tell tanzanians what happened:ballchain: richmond!!!! Why did he resign? Kikwete 0000! still travel left and right leaving the country and tax payers suffer! by the why what does he care? I wish..... cant talk no more he is a very sickening leader in Africa right now the most unpopular person i can ever think of
 
subiri uone udini wa chadema watakavyomrukia ZITTO. wanajua zitto ni kichwa kupita hata huyo slaa lakini slaa wanampenda kwa kuwa ni PADRI.
Nilijua mkigoma utayeasema tu haya. Sikulaumu!!!
 
Last edited by a moderator:
Tuache kelele nyingi, kama ungepewa mamlaka ya kumteua kati ya Zitto Zuberi Kabwe ama Wilbroad Peter Slaa kugombea nafasi ya urais mwaka 2015. Ni nani ungemteua? Na Kwa Nini? Toa sababu kuu nne TU.
Naona kuna agenda ya siri ndani ya kura hii na naamini ni mkakati wa magamba tulioelezwa na Wassira wa kuchochea mifarakano ndani ya chama. Haiingii akilini kuwashindanisha watu wawili wa chama hicho hicho, wenye lengo moja, la kuwang'oa wakoloni (CCM) eti ni nani anakubalika zaidi. Kura hii ya maoni ingependeza sana kama ingemshindanisha Dr. Slaa au Zitto na mtu kama Lowasa, Sitta, Migiro na wengine ndani ya CCM wenye wanaoonyesha kuutamani urais 2015. Hata hivyo naamini mbinu wanazotumia zitagonga ukuta kwani najua CHADEMA imesheheni watu makini kabisa ambao mara kadhaa walioweza kupangua mbinu za kihaini za maadui zao mapema na kuwaaibisha. Ingefaa sote tukalitambua hili na kuwa makini zaidi na magamba hawa ili kuyalinda mafanikio ya chama chetu.

 
Hapa ni Dr. Willbroad Peter Slaa!
Sababu
1. Ni mwanamageuzi wa kweli asiyeyumbishwa na aliyejitoa kwa mageuzi.
2. Msimamo wa anacho kiamini unadhihirika ktk matendo yake, tofaut na zitto, yeye haeleweki mara ashirikiane na Kafulila, mara ashirikiane na JK, kwel Zitto hatumwelewi. Hivi huu ukarib wa Zitto na JK maana yake nini?
3. Dr. Slaa anao uwezo mkubwa kama kiongozi wakupambanua mambo na kufanya maamuzi kama kiongozi.
4. Dr. Slaa ni kiongozi anayejali sana utu wa wanadam wengine.
Dr. Slaa tegemeo letu kuu, hakuna mwingine kwa sasa ndani ya cdm hata ndani ya majambazi ccm!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom