Zitto ni kijana shupavu, naweza kusema ni chachu ya vijana walioleta changamoto nzuri sana bungeni hata leo, sasa bunge limetambua wajibu wake badala ya kukubali kila kitu cha serikali. Ikumbukwe kuwa enzi za mzee wa urambo Zitto aliwahi kufukuzwa bungeni na kufungiwa kuhudhuria baadhi ya vikao kwa maslahi ya uhuru wa kutoa mawazo. Hakuna shaka Watanzania baada ya kuona umahiri wa Zitto hawakusita kuongeza wabunge wengine wa upinzani na hasa CDM. Idadi kubwa ya wabunge wa CDM bungeni imechangiwa kwa kiasi kikubwa sana na mwenendo wa Zitto bungeni.Kwa hili la kugombea Urais, simpendekezi Zitto kuwa mgombea wa CDM kwa sababu zifuatazo:1. Ni mpenda fedha mno kiasi kwamba akisikia harufu ya noti hukosa amani, hutamani kusaliti hata watu walio karibu naye ili mradi apate fedha.2. Ni mchanga mno katika siasa kiasi cha kupewa urais wa nchi hii, aendelee kugombea ubunge ili aimarishe upinzani bungeni.3. Ni mpenda madaraka hivyo hatawatumikia Watanzania kwa haki atafanya kazi kwa sifa ili awafurahishe watu fulani fulani. 4. Ni Mtanzania mwenye asili ya Burundi (sisemi kwamba siyo raia wa Tanzania), kwa tabia ya Warundi huwa hawasahau kwao. Kule Burundi kuna uhaba wa ardhi, akiwa rais ataitoa Kigoma kwa Burundi na kuifanya makazi yao hata kama ni kwa siri.Kwa upande wa Daktari Slaa simpendekezi pia kuwa rais kwa sababu zifuatazo:1. Ana uchu wa mapenzi, aliacha kazi ya upadri ili aoe. Tabia hii itamfanya ashindwe kuwatumikia Watanzania badala yake anaweza kuanzisha ligi ya kuoa vidocho akishindana na King Mswati.2. Ni mpenda fedha, hakutaka kuacha ubunge kwa hiari ili agombee urais hadi CDM walipomhakikishia kuwa hata akishindwa urais ataendelea kupokea posho sawa na mshahara wake wa ubunge. Hapa hakuwa na nia ya dhati ya kuwatumikia Watanzania bali maslahi mbele. Nyerere aliacha mshahara wa ualimu na kuchagua kuimarisha TANU bila malipo ya mshahara wala posho.3. Ni mshindani asiyekubali kushindwa. Katika uchaguzi uliopita alisusia hafla ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi kwa madai kuwa kura zilichakachuliwa. Maalim Seif alikubali mara zote kushindwa huko Zanzibar hata pale ilipoaminika (haikuthibitika) kuwa kura zilichakachuliwa; mtakumbuka enzi za Komandoo Salmin Amour v Maalim Seif (mara moja), Daktari Karume v Maalim Seif (mara mbili) na Daktari Shein v Maalim Seif (mara moja).4. Ni mdini sana, aliwahi kuwa padri na katibu mkuu wa TEC, akipewa nchi bila shaka ataiongoza kwa sera za Kivatikani au Kisayuni.Kwa maoni yangu wote hawa wawili viz. Zitto na Slaa hawatufai kuwa viongozi katika nafasi ya urais. Naomba uletwe mpambao mwingine.Inawezakana kabisa CDM ikashinda kiti cha urais 2015 lakini rais ajaye si mmoja wa viongozi waliopo ngazi za juu ndani ya CDM. 'Salvation shall come from the hills, the man shall rise and save the people at their hour of need' (Ngugi wa Thiong'o in the River between).