Kura ya maoni: Zitto vs Dr Slaa

Kura ya maoni: Zitto vs Dr Slaa

Ni nani ungependa agombee urais mwaka 2015 kwa tiketi ya CHADEMA?

  • Zitto Z. Kabwe

    Votes: 180 15.3%
  • Wilbrod P. Slaa

    Votes: 996 84.7%

  • Total voters
    1,176
  • Poll closed .
Status
Not open for further replies.
zitto atapata kura nyingi akigombea urais kuliko slaa,slaa ni mzee kwa sasa.
slaa ni mzee hafai kwenye uraisi?....ikulu hawabebi zege mkuu.mandela kaiongoza sauzi akiwa na umri gani?acha uvivu wa kufikiri..prof.mhongo ana umri gani lkn anainyosha wizara ..wakati vijana km akina ngeleja na malima walichemsha...uongozi co umri!
 
Jamani tuwe serious tunapohitaji Rais kama vile tunapokuwa serious tunapotafuta mke. Tanzania inahitaji rais na siyo mshikaji. Nakubaliana na zitto kuwa PM kwa miaka kumi ili aje awe Rais miaka 10 ijayo. 2015 tunahitaji rais si kama alivyotulagai JK kuwa ni kijana tukavimbewa sifa wakati vijana wamefanya vibaya kuliko watu wa makamo katika medali ya Dunia na afrika. Nyerere aliposema at least 45yrs ana maana kubwa sana lakini hizi age za akina kabila wa kongo tutakuwa wa mwisho kiuchumi kama wakongo! Nampenda zitto katika shit politics kama za watanzania lakini economic politics nitahama TZ kwa muda. Sorry ila asubiri 2025.
 
hii kitu inaweza ikamfanya zitto aichukia jf daima. ataona kama vile inamuumbua coz zitto ni kama sisimizi kwa dr. Slaa.
 
watu wamekupuuza mnafiki wewe


mnafki wewe uliyetumwa kumchafua Zitto kabwe utaisoma mwaka huu mlizani waislamu hatupo tupo ila huwa tunaingia na kutoka,

sasa uislamu wako unatusaidia nini sisi kama waTanzania? Hapa tunamjadili zito wala si dini yake... Lakini ulipogundua zito hakubaliki ni mnafiki kama wewe unaleta vioja na huruma za kidini,inashangaza sana ebu soma thread zote uone kama kuna sehemu umetajwa ukristo.. Hivi dini yako weak kiasi kwamba bila kusemwa semwa haitasikika? Mna matatizo sio bule.
 
Katika imani yako umekuwa spoiled,
unaamini kwa dhati kwamba,
maoni kinyume na imani yako,
ni batili na ni dalili ya upendeleo.
katika kura hii una nafasi ya,
kutumia nafasi yako kama member,
kumchagua umpendaye,
au kuto piga kura kwa kula jiwe,
una haki ya kutoa maoni yako binafsi,
huna haki ya kuingilia haki za watu wengine,
maelezo yako ni maoni yako binafsi,
yatoe lakini usiyafanye msahafu kwa wengine,
Padri, sheikh, mufti, askofu,kuhani,mzee wa busara?
uchaguzi ni wa mtu binafsi,

Hapa JF wote ruksa kujiunga,
nasikia tu kwamba,
80% ya population,
ya watu wa dini na imani moja kuu,
ni zaidi ya nusu ya Watanzania wote,
pia kundi hili la waumini,
ni watu wa kheri amani na unyenyekevu.
Naamini pia kwamba kundi hili la waumini,
ni 75% ya wanachama wa JF,
Sasa ikitokea kundi hili kumpenda zaidi Dr Slaa,
kwa sababu ya uwingi wao na tafakari yao,
wewe ni nani hata upinge na kubeza chaguo lao?
pia kuwa na mawazo ya kudhani ni upendeleo?
Waswahili husema Wengi wape.



subiri uone udini wa chadema watakavyomrukia ZITTO. wanajua zitto ni kichwa kupita hata huyo slaa lakini slaa wanampenda kwa kuwa ni PADRI.
 
Hii thread inalengo la kumchafua Zitto kutokana na kashfa ya kula mlungula
 
ni kweli jembe la kulimia zao la rushwa, lakini safari hii bei ya zao hili haramu limewekwa peupe......na sio kwenye black market kama walivyozoea.
zitto ndo jembe lenyeye we subiri:yawn::yawn:
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom