Kupigwa marufuku kwa Micron kwailetea Marekani wasiwasi mkubwa

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG111437771335.jpg
China hivi karibuni ilitangaza kupiga marufuku kampuni za miundombinu muhimu nchini humo kununua bidhaa za Kampuni ya Micron ya Marekani inayotengeneza chip za kapyuta, baada ya kampuni hiyo kushindwa katika uchunguzi wa usalama uliofanywa na China. Tukio hili limeleta wasiwasi mkubwa kwa Marekani, ambayo inaona kwamba China imeanza kulipiza kisasi vitendo vyake viovu dhidi ya makampuni ya China kwa kisingizio cha “usalama wa taifa”.

Msemaji wa Wizara ya Biashara ya Marekani Matthew Miller amedai kuwa, marufuku hiyo imewekwa bila ya msingi, na itavuruga soko la chip za kampyuta. Lakini, kwa kweli, katika miaka ya hivi karibuni, kutoka Huawei hadi TikTok, Marekani imeweka vikwazo dhidi ya kampuni zaidi ya 800 za China kwa kisingizio cha “usalama wa kitaifa”. Katika mkutano na waandishi wa habari, mwanahabari mmoja alimuuliza Miller, ni kwa nini Marekani inaweza kupiga marufuku kampuni za China kutokana na usalama wa taifa, lakini China haiwezi? Miller alijibu kwa kusitasita, kwamba sababu ni kuwa China imesema inafungua mlango wake kwa kampuni za nje. Jibu hilo liliamsha swali lingine kutoka kwa mwanahabari huyo, ambaye aliuliza, je, si Marekani pia imesema inafungua mlango kwa wafanyabiashara?

Ingawa alichouliza mwanahabari huyo wa Marekani kilikuwa ni sawa, lakini hakufahamu vizuri madhumuni ya China, na kuchukulia kuwa China inataka kulipiza kisasi dhidi ya Marekani. Ukweli ni kwamba, hivi sasa Marekani ina wasiwasi mkubwa, kuwa licha ya Micron, China itaadhibu kampuni nyingine nyingi za Marekani, na hii inatokana na vitendo vibaya ambavyo nchi iefanya dhidi ya kampuni za China kwa kisingizio cha “usalama wa taifa”.

Hata hivyo, tofauti na vitendo viovu vya Marekani, hatua ya China dhidi ya Micron inatokana na uchunguzi wa wiki 7 uliofanywa na Idara Kuu ya Forodha ya China, pamoja na Ofisi ya Usalama wa Mtandao ya China. Uchunguzi huo uligundua kuwa, bidhaa za Micron zina hatari kubwa kwa usalama wa mtandao nchini China, haswa katika miundombinu muhimu ya habari. Kulingana na Sheria ya Usalama wa Mtandao na sheria nyingine husika za China, kampuni zinazoshughulikia miundombinu muhimu nchini China zinapaswa kuacha kununua bidhaa za Micron.

Micron sio kampuni ya kwanza iliyofanyiwa ukaguzi wa usalama nchini China, na ile kauli inayosema hatua ya China inalenga kampuni za Marekani haina msingi wowote. Jambo pekee ambalo tukio hilo linathibitisha ni kwamba, baada ya kukamilika kwa mfumo wa sheria wa China, shughuli zozote za kibiashara ni lazima zifuate sheria, na haziwezi kutishia usalama wa taifa la China.
 
China hakufai tena kwa uwekezaji,

Amazon imetangaza kufunga biashara zake mainland China huku Alibaba-China ikitangaza kupunguza wafanyakazi.,

Hali hii inakuja huku unemployment rate ikizidi kuongezeka siku baada ya siku.

Labour cost imezidi kukua maradufu, sera mbaya za kimahusiano na mataifa mengine, matishio ya vita, na sera mbaya za Afya zilizokuwa zinachochea lock down zimewafanya wawekezaji wengi kufikiria uwekezaji wao ndani ya China.
 
China hakufai tena kwa uwekezaji,

Amazon imetangaza kufunga biashara zake mainland China huku Alibaba-China ikitangaza kupunguza wafanyakazi.,

Hali hii inakuja huku unemployment rate ikizidi kuongezeka siku baada ya siku.

Labour cost imezidi kukua maradufu, sera mbaya za kimahusiano na mataifa mengine, matishio ya vita, na sera mbaya za Afya zilizokuwa zinachochea lock down zimewafanya wawekezaji wengi kufikiria uwekezaji wao ndani ya China.
Amka toka usingizini juzi tu apa kampuni ya magari ya Volkswagen wameomba kurudi kwenye soko la china baada ya kupata hasara iliyopitiliza ulaya ndio akukaliki gesi na mafuta bei juu ..yani ukizalisha kitu ulaya inabidi uhuze mara 2 ya bei ya mwanzo ili upate faida muda uwo uwo kuna wenzako wapo china wanafaidi gesi na mafuta ya bei chee nao wanatengeneza kitu kama chako kwa ubora ule ule tena kwa bei cheap kinachotokea ni watu kukupiga TKO ..
 
China hakufai tena kwa uwekezaji,

Amazon imetangaza kufunga biashara zake mainland China huku Alibaba-China ikitangaza kupunguza wafanyakazi.,

Hali hii inakuja huku unemployment rate ikizidi kuongezeka siku baada ya siku.

Labour cost imezidi kukua maradufu, sera mbaya za kimahusiano na mataifa mengine, matishio ya vita, na sera mbaya za Afya zilizokuwa zinachochea lock down zimewafanya wawekezaji wengi kufikiria uwekezaji wao ndani ya China.
Huko Marekani ndio kunafaa kwa uwekezaji? Kwanini unapenda kutumia kichwa chako kama kabati la ulimi?
Wakati Marekani anafanya haya hukuongea ila kwa kuwa kafanya China ndio mnaanza kuongea kama kuku aliyekatwa kichwa
 
Amka toka usingizini juzi tu apa kampuni ya magari ya Volkswagen wameomba kurudi kwenye soko la china baada ya kupata hasara iliyopitiliza ulaya ndio akukaliki gesi na mafuta bei juu ..yani ukizalisha kitu ulaya inabidi uhuze mara 2 ya bei ya mwanzo ili upate faida muda uwo uwo kuna wenzako wapo china wanafaidi gesi na mafuta ya bei chee nao wanatengeneza kitu kama chako kwa ubora ule ule tena kwa bei cheap kinachotokea ni watu kukupiga TKO ..
Hawezi elewa huyo unapigia ng'ombe gitaa
 
China hakufai tena kwa uwekezaji,

Amazon imetangaza kufunga biashara zake mainland China huku Alibaba-China ikitangaza kupunguza wafanyakazi.,

Hali hii inakuja huku unemployment rate ikizidi kuongezeka siku baada ya siku.

Labour cost imezidi kukua maradufu, sera mbaya za kimahusiano na mataifa mengine, matishio ya vita, na sera mbaya za Afya zilizokuwa zinachochea lock down zimewafanya wawekezaji wengi kufikiria uwekezaji wao ndani ya China.
Weee jamaa ni waajaabu sana aisee vp Amazon alivyopunguzaa wafanyakaazi haikuwa ishu au waajitoa ufahamu alafu Amazon hana wateja wengi China kama marekani na wala siyo kampuni popular kwenye eneo lakke china kama ilivyo Apple kwaiyo wadanganye vilaza wenzio
 
Weee jamaa ni waajaabu sana aisee vp Amazon alivyopunguzaa wafanyakaazi haikuwa ishu au waajitoa ufahamu alafu Amazon hana wateja wengi China kama marekani na wala siyo kampuni popular kwenye eneo lakke china kama ilivyo Apple kwaiyo wadanganye vilaza wenzio
Amazon hana wateja wengi China?

Unajua ni makampuni mangapi yamefunga virago since 2020 kuondoka China?

Nimezungumzia mazingira mazuri kiuwekezaji nikimaanisha sera zao za mambo ya nje na afya zinatishia uwekezaji.

Zaidi ya makampuni 5000+ ya ndani na nje ya China yamefunga biashara zao China. Hii imepelekea ongezeko kubwa la unemployment.

Selikari ya China inekiri mpaka wanaanzisha program za kupunguza unemployment kwa mfano saivi wameanzisha 1 million internship program lakini bado haionekani kuleta manufaa yoyote, pia wanafkiria kutoa 500 billion yuan kuboost uchumi wao na kuongeza nguvu ya ununuzi lakini bado inaonekana haitoleta manufaa yoyote.

Ukishavurugana na mataifa mengine kwa vitisho vya vita usitegemee kwamba utafika popote
 
Amazon hana wateja wengi China?

Unajua ni makampuni mangapi yamefunga virago since 2020 kuondoka China?

Nimezungumzia mazingira mazuri kiuwekezaji nikimaanisha sera zao za mambo ya nje na afya zinatishia uwekezaji.

Zaidi ya makampuni 5000+ ya ndani na nje ya China yamefunga biashara zao China. Hii imepelekea ongezeko kubwa la unemployment.

Selikari ya China inekiri mpaka wanaanzisha program za kupunguza unemployment kwa mfano saivi wameanzisha 1 million internship program lakini bado haionekani kuleta manufaa yoyote, pia wanafkiria kutoa 500 billion yuan kuboost uchumi wao na kuongeza nguvu ya ununuzi lakini bado inaonekana haitoleta manufaa yoyote.

Ukishavurugana na mataifa mengine kwa vitisho vya vita usitegemee kwamba utafika popote
China kavurugana na nani? US ndio anataka kuingilia mambo ya watu halafu unamsema China, Taiwan ni sehemu ya China dunia nzima inajua sasa unapo ipa silaha za kisasa lengo lako ni lipi? halafu unataka China akae tu kimya?
 
China kavurugana na nani? US ndio anataka kuingilia mambo ya watu halafu unamsema China, Taiwan ni sehemu ya China dunia nzima inajua sasa unapo ipa silaha za kisasa lengo lako ni lipi? halafu unataka China akae tu kimya?
Hakuna mtu anaependa mikwaruzano na vita, watu milion 25 wa Taiwan hawataki kuungana na çhina,

Anataka kutumia nguvu ya kijeshi kuivamia, so what?

Ameshaivuruga Hong Kong inatosha, sasahivi wanatumia rushwa kuivuruga solom island, hakuna mtu atamchekea CCP akiagiza PLA aivamie Taiwan, ni swaswa na kuiattack Democracy.

Autocratic leadership hauna nafasi na hautokaa upewe nafasi ya kuutawala huu ulimwengu.
 
Hakuna mtu anaependa mikwaruzano na vita, watu milion 25 wa Taiwan hawataki kuungana na çhina,

Anataka kutumia nguvu ya kijeshi kuivamia, so what?

Ameshaivuruga Hong Kong inatosha, sasahivi wanatumia rushwa kuivuruga solom island, hakuna mtu atamchekea CCP akiagiza PLA aivamie Taiwan, ni swaswa na kuiattack Democracy.

Autocratic leadership hauna nafasi na hautokaa upewe nafasi ya kuutawala huu ulimwengu.
Hizo ni internal affairs hakuna sababu ya US Na washirika wake kulivalia njuga, mbona US alivamia Iraq alipoona usalama wake upo hatarini? vip China maneno yawe mengi kwenye mambo yake ya ndani? Wana ajenda gani hawa watu
 
Amazon hana wateja wengi China?

Unajua ni makampuni mangapi yamefunga virago since 2020 kuondoka China?

Nimezungumzia mazingira mazuri kiuwekezaji nikimaanisha sera zao za mambo ya nje na afya zinatishia uwekezaji.

Zaidi ya makampuni 5000+ ya ndani na nje ya China yamefunga biashara zao China. Hii imepelekea ongezeko kubwa la unemployment.

Selikari ya China inekiri mpaka wanaanzisha program za kupunguza unemployment kwa mfano saivi wameanzisha 1 million internship program lakini bado haionekani kuleta manufaa yoyote, pia wanafkiria kutoa 500 billion yuan kuboost uchumi wao na kuongeza nguvu ya ununuzi lakini bado inaonekana haitoleta manufaa yoyote.

Ukishavurugana na mataifa mengine kwa vitisho vya vita usitegemee kwamba utafika popote
Wala usitumie nguvu sana, maadam umeshaweka zile facts za awali, nyingine zote zinazofuata uwe unawaitikia tu "Sawa" , "Sawq", "Nilikua sijui". Just like that.
 
Hizo ni internal affairs hakuna sababu ya US Na washirika wake kulivalia njuga, mbona US alivamia Iraq alipoona usalama wake upo hatarini? vip China maneno yawe mengi kwenye mambo yake ya ndani?
Ajenda ya China kuivamia Taiwan pia kunaziweka nchi nyingi hatarini, China ana ajenda yake ya kuextende its military power and existence over Pacific

Wanataka mpaka 2049 China iwe super power, what is behind this? Matokeo ya China kuwa na nguvu tumeyaona Hong Kong., the same wanataka kupenyeza utawala wao Taiwan, wakishamaliza kuichukua Taiwan, China ina agenda ya kupush utawala wao na kutawala kila kitu kilichopo kwenye wenyewe wanaita first island chain.

Watakachokifanya ndicho kama wanachokifanya sasahivi kwenye south China sea, wanainyanyasa Philippines, wanawanyanyasa wavuvi wa kifilipino tena kwenye maeneo yao yaliyo ndani ya EEZ Kisheria wakisema kwamba ni yakwao.

Waliextend power mpaka Indonesia kule chini kabisa mbali kabisa na China wakataka kugrab Kuna kisiwa kipo karibu kabisa na Indonesia, rais wa wakati huo akawatimua. Mchezo huu ndio utakaokuwa unafanywa baada ya kuichukua taiwan, watafata solom island to the next second island chain wenyewe wanadai.

Kwa kifupi Japan, Philippines, Australia, Solomon island, South Korea, Vietnam, Indonesia nchi hizi zote zinaiona China inahatarisha usalama wao.

Hakuna na hapana taifa litakubali Taiwan ivamiwe na china, no never.... hakuna nchi ya kidemokrasia itakubali Taiwan ipoteze Demokrasia yake hivi hivi tu eti kwa kisingizio cha internal affairs, hell no! What is human rights? Yaani tumekubaliana kulinda haki za binadamu basi kwa kuwa ni internal affairs kama unavunja haki za binadamu kwa watu zaidi ya milion 25 watu wakuangalie tu.
 
Ajenda ya China kuivamia Taiwan pia kunaziweka nchi nyingi hatarini, China ana ajenda yake ya kuextende its military power and existence over Pacific

Wanataka mpaka 2049 China iwe super power, what is behind this? Matokeo ya China kuwa na nguvu tumeyaona Hong Kong., the same wanataka kupenyeza utawala wao Taiwan, wakishamaliza kuichukua Taiwan, China ina agenda ya kupush utawala wao na kutawala kila kitu kilichopo kwenye wenyewe wanaita first island chain.

Watakachokifanya ndicho kama wanachokifanya sasahivi kwenye south China sea, wanainyanyasa Philippines, wanawanyanyasa wavuvi wa kifilipino tena kwenye maeneo yao yaliyo ndani ya EEZ Kisheria wakisema kwamba ni yakwao.

Waliextend power mpaka Indonesia kule chini kabisa mbali kabisa na China wakataka kugrab Kuna kisiwa kipo karibu kabisa na Indonesia, rais wa wakati huo akawatimua. Mchezo huu ndio utakaokuwa unafanywa baada ya kuichukua taiwan, watafata solom island to the next second island chain wenyewe wanadai.

Kwa kifupi Japan, Philippines, Australia, Solomon island, South Korea, Vietnam, Indonesia nchi hizi zote zinaiona China inahatarisha usalama wao.

Hakuna na hapana taifa litakubali Taiwan ivamiwe na china, no never.... hakuna nchi ya kidemokrasia itakubali Taiwan ipoteze Demokrasia yake hivi hivi tu.
US kila sehemu yupo sasa ubaya uko wapi Na yeye China kujitanua? US yuko mpaka Syria ambako Serikali inasema wala haija mpa mualiko, mimi naona huu ni wivu wa US na nchi za Magharibi, wao ndio wenye historia ya kuvamia nchi huru na kufanya uharibifu mkubwa miaka ya hivi karibuni sio China, ajabu waharibifu ndio wanakuwa waalimu wa watu wengine
 
US kila sehemu yupo sasa ubaya uko wapi Na yeye China kujitanua? US yuko mpaka Syria ambako Serikali inasema wala haija mpa mualiko, mimi naona huu ni wivu wa US na nchi za Magharibi, wao ndio wenye historia ya kuvamia nchi huru na kufanya uharibifu mkubwa miaka ya hivi karibuni sio China, ajabu waharibifu ndio wanakuwa waalimu wa watu wengine
Tunaomgelea ishu ya China na Taiwan!

Wewe unaona ni sawa kwa kilichotokea Hong Kong?

Hong Kong ilikiwa democratic kabla ya CCP kuextend mkono wake kule, sehemu ile ilikuwa huru na kila mtu alikuwa huru kuelezea chochote, tangu majamaa yaanzishe ukandamizaji Hong Kong imekuwa hamfai tena.
 
Back
Top Bottom