Kupigiana simu kwa wanandoa

Kupigiana simu kwa wanandoa

Habarini za asubuhi wakuu, natumai ni wazima sana. Leo nina swali kwa wanandoa au wenye mahusiano ya mbali, mimi mume wangu siyo kwamba anafanya kazi nje ya mkoa ila amesafiri kikazi kwa muda tu ana kama karibia miezi 2.

Ila mwenzangu huyu hapigi simu ni ujumbe tu, sasa mimi hicho kitendo kinaniudhi sana na akipiga kidogo utasikia dk. zimeisha, sasa najiuliza dk. zimeisha anaongea na kina nani?

Sasa swali langu kwa wanandoa hasa wenye upendo na wake/waume/wapenzi wao, wanaweza kaa hata siku 3 bila kumpigia simu mwenza wake, yaani ni kawaida au kuna shida pahala?

Naomba maoni yenu hasa kwa wanaume waliokuwa makini na wake/wapenzi wao, namaanisha wenye upendo wa Agape.
Marekebisho kidogo upendo wa agape sio upendo wa kimahaba yaani kati ya wapendanao kama mume na mke

Turudi kwenye mada; ninachojua mimi meseji ni mojawapo ya njia ya mawasiliano, jambo la msingi ni wewe kumpigia ikiwa unaona kwako kupiga simu ndo njia bora ya mawasiliano.

Wanawake sijui mnafeli wapi, mnakuwa wabahiri sana na wabinafsi. Yeye akiishiwa dk basi wewe mpigie mbona ni ishu ndogo sana bidada
 
Nikuambie tu Mkuu, kama mnawasilianakwa namna hiyo inatosha. Mambo ya ndoa yanautata sana, kuna jambo ambalo nyie mnavyolifanya na mnaliona la kawaida na huenda upendo upo ila mtu mwingine hapa JF atakuambia oooh mara unaibiwa mara blah blah..! Kwahiyo kama mnawasiliana kwa namna hiyo na hakuna shida nyingine acha kuyakuza bidada.

Jambo jingine nikuombe wewe na wanawake wenzako, kwa asili nyie wenzetu huwa mnapenda kutendewa zaidi ila kwenye kutenda ni zero. Nianze na jambo la kupigiana simu, hivi kwenye mahusiano kuna mahali imeandikwa mwanaume tu ndio anatakiwa kupig simu?? Unapoona yulo kimya jiunge dakika mpigie muongee vya kutosha sio lazima wewe tu ndio upigiwe. Hii tabia haya mke wangu anayo, niliwahi kumwambia wazi kama nimivyoandika hapa. Nashukuru Mungu amebadilika. Huwa anapiga tunaongea vya kutosha tu na mimi ikitokea ninazo dakika nampigia bidada tunaongea mpaka dakika zinaisha.
Sasa wewe ukiona yuko kimya, jiunge dakika 100 za mitandao yote alfu mpigie.
Alfu kusema, hizo dakika zinaloisha unajiuliza anaongeaga na nani zinaisha!?? Hivi kwanj kwenye simu yake ipo namba yako tu!?? Acha wivu wa kishamba utakufa mapemA na nimeona unapenda kuyakuza mambo, ohooo utaugua pressure muda si mrefu.
Ushauri mzuri sana, i wish ungemfikia pia wife... naufoward kama ulivyo aupate...
 
Kwa kipindi chote tulichokua pamoja hadi leo hii n kama tabia. Nkiamka asubuh lazma nimpigie haijalishi n mda gani. Na yeye pia hvo hvo in case akiamka before me.
After that ni mchana nkipata lunch break kazini lazma nimcheki mama watoto tuyajenge kidogo. Nkimaliza hapo ni usiku before sijalala (most times usiku anapiga yeye coz hua anazima mapema).
Personally sio mpenz wa kupiga sim lakn napiga because najua inampa faraja mwenzangu, so sioni shida. Na mara nyingi hata dk 10 za maongez hazifiki lakn yeye anaridhika.
Hata kama niko busy vipi, ntatafta hata dk 5 maybe nkiwa naenda msalani kumcheki kujua anaendeleaje then nakata waya nafanya mambo mengine.
Its all about priorities
Unazungumzia muvi gani hii mkuu!??
 
Mimi nilikuw hvyo ila nmebadlishwa
Nakuomb dm uje nkusaidia hilo tatzo mkuu
 
Aiseee....!!!

Mimi mvivu kuwasiliana mara Kwa mara pia na ni Ke. Nimevumiliwa nimechokwa, nimesemwa najikuta najitahidi ila siwezi.

So naweza sema labda kapata wa kumpigia na kumtext atakavyo au kaamua kunizoea.

Nawasiliana kukiwa na shida maalum inayohitaji kufanya hivyo na pia ni kutuma tu text, Kwa kweli kupiga ni mara chache mnoooooooo yaweza mwezi upite sijapiga.

Jamani muda wa kumisiana upatikane pia
 
Hyo ni life ya kila siku. Might seem as a movir for u, pole.
Pole ya nini tena kiongozi, huo upotoshaji wako wa kimandazi ku win akili za wadada wahapa Jf unazani zinanipa shida!?? Eti poleee, tuliza usimbe wako huko.
 
Nazidi kujifunza kila siku. Wengi wetu hii mitandao tunaichukua kama kuenjoy na tunapita lakin naamin kama uko conscious utazidi kubadilisha mtazamo juu ya mambo mengi.

Nilikuaga mtu mwenye pride sana yani ile ile. Nilikua kama wewe ndugu mleta mada. Kungoja kutumiwa message..kungoja kupigiwa..na tena namaind kabisa nisipotafutwa..tables turned aisee. Mbona nilinyooka.

Nikajifunza maturity is a very complex topic. Kuna mengi ya kubeba na kuacha along the road. Kuna mwandish aliandika akasema kama unaona mtu umeshasema juu ya jambo fulan na habadiliki badilika wewe.

Mpaka kumkubali kuwa nae it means alifit kwenye vigezo vya kuwa mume wako. Na uliahidi meng madhabahuni dada mzuri. Kwaiyo hii ndo katika shida yenyewe. Naomba umpende kama alivyo msela..usimuache. change your perception. Unapata vocha mpigie..muongee. inakuuma ongea nae mwambie. Asipobadilika badilisha mtazamo. Ona ni kitu cha kawaida kabisa. Kama anafanya majukumu yake na kukupenda ila hilo tu ndo dhaifu..basi mbebe...ndo dhaifu lake. Kama katika 100% ana 80% hiyo 20% ndo wewe sasa utaicover..

Usimfananishe na wanaume wengine eti kisa umeona fulan anapigiwa au flani alikua anampigia mpenzi wake basi na wewe unataka ufanyiwe ivo. Love sio pie (3.14) kwamba inafanana duniani kote. Kila mmoja ana namna anavyoexpress penz lake. Nakuaminia dada....be smart, be unique. Be more than ruby.
 
Mapenzi yapo moyoni usifanye vitu vidogo kuharibu penzi lenu kama Hapigi mpigie weye
 
Habarini za asubuhi wakuu, natumai ni wazima sana. Leo nina swali kwa wanandoa au wenye mahusiano ya mbali, mimi mume wangu siyo kwamba anafanya kazi nje ya mkoa ila amesafiri kikazi kwa muda tu ana kama karibia miezi 2.

Ila mwenzangu huyu hapigi simu ni ujumbe tu, sasa mimi hicho kitendo kinaniudhi sana na akipiga kidogo utasikia dk. zimeisha, sasa najiuliza dk. zimeisha anaongea na kina nani?

Sasa swali langu kwa wanandoa hasa wenye upendo na wake/waume/wapenzi wao, wanaweza kaa hata siku 3 bila kumpigia simu mwenza wake, yaani ni kawaida au kuna shida pahala?

Naomba maoni yenu hasa kwa wanaume waliokuwa makini na wake/wapenzi wao, namaanisha wenye upendo wa Agape.
Umeachwa we umeachwaaa @Lodymusic

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom