Kupendwa sana na mtu usiyempenda

Kupendwa sana na mtu usiyempenda

DEGIJONZE

Senior Member
Joined
Jul 15, 2012
Posts
144
Reaction score
89
Habari zenu wana JamiiForums

Naomba kushare na ninyi hiki kitu maana kimekuwa kikinisumbua sana. Nimekuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na dada mmoja ambaye ametokea kunipenda sana na kweli yule dada ana sifa zote za kuwa mke ila tatizo liko kwangu moyo wangu unakuwa mzito sana kila nikijitahidi nioneshe mapenzi ya kutoka moyoni najikuta nashindwa kabisa na hisia zangu kwake wakati mwingine zinaisha kabisa.

Kila nikijilazimisha nifanye maamuzi ya process za ndoa najikuta moyo unagoma kabisa, yaani pamoja na kwamba ananipenda sana na yuko tayari kufanya chochote kwaajili yangu lakini mimi moyo wangu haupo kabisa kwake. Kila nikijitahidi nimpende najikuta nashindwa.

Naomba kama kuna watu walishawahi kupitia hii changamoto tushare uzoefu ili niweze kuamua kama ninaendelea naye au kila mtu ajue lake.
 
Najaribu kufikiria hadithi ya simulizi hii niipatie jina gani, kisha nikajikuta nimekumbuka walimu wanavyo fundishwa kufundisha..teh

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kupendwa sana na mtu usiempenda hiyo ni kero...
 
Binafsi nishajisemea nitampenda yoyote atakayenipa Attention yake hata kama ana sura kama ya big show (sorry nobody ugly ).
Lakini hata hao wa kunipa attention hamna kila naempenda kwake nakua mbingu na ardhi..
Usichezee bahati kiongozi..Utakumbuka halfu useme "Ningejua" mind you hakuna neno au sentesi yenye maana ikianza na neno ningejua
 
Sawa na huyu single mama mmoja, kinganganizi sijawahi ona, mbaya afu ana mtoto sasa nyodo nikinuacha hakubali nikijifanya wacha nimfariji anaanza jeuri.

Nadhani hanijui kuwa mimi ni nishai wacha nitamtolea uvivu..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukweli ni huu,wanawake wengi sisi wanaume tumekuwa tukiwapenda kwa vitu vya nje kama sura, nywele, macho, miguu, kiuno, makalio, kucha n.k bila ya kujali tabia ya muhusika,na kwakuwa wameshajua udhaifu wetu wanapambana sana kuhakikisha hivyo vitu wanaviweka katika mazingira ya kuvutia sana, sasa unapoingia kwenye mapenzi vile vitu unagundua kuwa sio halisi ndio pale hisia zinaanza kushuka,

PIA, kimaumbile sisi wanaume tunapopenda penzi letu linakua juu sana kabla ya kumpata muhusika, lakini ukishampata huwa lina shuka kwa kasi,unlike wanawake wao mwanzoni mapenzi hayawi makali sana,ila akishapatwa ndio penzi linakuwa kali sana kwahiyo mnakuwa kama mnapishana,that's nature.Ndio maana Mungu alikataza hata zinaa kabla ya ndoa kwani alijua hili, na pia hii imesababisha wanawake wengi sana kuishia kwenye kutendwa na kuachwa...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usimpotezee muda mtoto wa wenyewe
Kama moyo umekataa usiulazimishe moyo
Atampata atakayempenda na kuthamini pendo lake
Wanaume mnasumbua mjue
 
Changa vizuri karata zako mkuu, pima vizuri athari za uamuzi utakaochukua (iwe kumuacha au kuendelea nae) usije ukajutia maamuzi yako baadae.
 
Mkuu mpaka hapo ushanasa tayari,yaani ukishaona anakuita na unaenda kukutana naye ndio basi ameshakunasa.
Itaishia tu mikwara ya mdomoni na maneno matupu
Sawa na huyu single mama mmoja, kinganganizi sijawahi ona, mbaya afu ana mtoto sasa nyodo nikinuacha hakubali nikijifanya wacha nimfariji anaanza jeuri.

Nadhani hanijui kuwa mimi ni nishai wacha nitamtolea uvivu..

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni vyema kupendwa kuliko kupenda, oa chap. Siku ukioa unayempenda then akupe stress humo ndani, sisi tutakuwepo kukushauri usijinyonge.
 
Kupendwa Sana na mwanamke ni bahati Kama nawe utampenda kwani uwezekano wa kukusaliti ni mdogo, ila Kama umeshindwa kabisa kumpenda Basi mwache mapema, isije ukampa ujauzito binti wa watu akawa single mother,mtihani wa kumpa ujauzito binti usiyempenda ni mgumu sana.
 
Back
Top Bottom