Kupenda kwangu kukaa mwenyewe kunafanya asilimia kubwa ya watu wanaonizunguka waone siwapendi

holy spirit

JF-Expert Member
Nov 30, 2020
698
1,039
Habarini members, natumaini mnaendelea vyema na majukumu ya kujenga taifa.

Ningependa kupata msaada wa mawazo kutoka kwenu ni jinsi gani naweza kushughulikia swala hili. Mimi binafsi sio mtu mwenye roho mbaya, mambo ya chuki na wivu naweza kuongea kwa kujiamini kabisa kwamba sina kabisa. Napenda sana kuwa independent, kuna nyakati najichanganya na watu lakini muda mwingi huwa nautumia kukaa peke yangu. Hata nikiwa kwenye kundi la watu naweza kuchangia mada kidogo muda mwingine nanyamaza hadi niulizwe.

Shida kubwa inayonikumba kutokana na kupenda kwangu kukaa mwenyewe kunafanya asilimia kubwa ya watu wanaonizunguka waone siwapendi au siwathamini. Hii hali naona sasa inawaingia hata watu wangu wa karibu ndugu pamoja na wazazi. Napata maneno kama vile "we utakuwa mtu wa aina gani huwezi ata kukaa na mzazi wako mkaongea ukija nyumbani kusalimia ni kujifungia chumbani tu". Wazazi nawathamini pamoja na ndugu pia ila ndo nilivyo yani napenda kukaa mwenyewe nisome vitabu, social media n.k. nikionana na mtu tunajuliana hali tunaongea dakika kumi au kumi tano kila mtu anaendelea na mambo yake. Hata chuoni sikuwa mtu wa kupenda discussion nilikuwa nasoma mwenyewe tu hii ilikuwa inafanya watu waone najikuta genius huku mi wa kawaida tu.

Kubadilika ni ngumu kidogo ila tatizo langu ni kwamba nawezaje kuwaondoa watu hayo mawazo ya kwamba mimi siwathamini au nawachukia sababu nayaona hayo mawazo kupitia maneno yao huku uhalisia kutoka moyoni mwangu hauko hivyo.



Sent from my M10_Max using JamiiForums mobile app
 
Mimi pia ni kama wewe labda tunaweza kutofautiana sababu tu. muda mwingi nakuaga peke yangu kwanza kutokua na ajira inaninyima hata nafasi ya kujiamini na kujichanganya na watu pili nina changamoto ya kusikia vizuri kwaiyo naweza hata kujichanganya na nisielewe nini kinaongelewa. Nafikiri mwenzangu hauna changamoto kama zangu. Kama unatumia kinywaji(sio lazima uwe mlevi ukiwa unapiga mbili tatu tu inatosha) na una uhakika wa maokoto kila wikiend jichanganye pub zilizochangamka uko utapata washkaji.
 
Hali Kama Yako Nakumbuka Nasona Primary school Kuna Dogo ndo Ilikuwa Tabia yake Ila yule Mtoto Alikuwa Genius Kweli Yeye haongei na wala Wala Kucheza Kipindi Cha Mapumziko Yeye ni Kimya Dalasani Ndo Kabisa Sijawahi Kumuona anacheza Wala Kuongea Na Mtu yeyote na Sio Bubu ila Ikija Mitihani Namba Moja Kuanzia Darasa 1 Mpaka la 7 Na Miaka Hiyo kufaulu ilikuwa Ni Mbinde Kweli Kweli Yeye ndo Aliongoza Wilaya nzima Daah Maisha Haya Sijui Sasa hivi Yuko Wapi na Ana Inshu Gani maana Kama Kusoma Kufaulu Maisha Basi Yeye Atakuwa Mbali Sanaa
 
Mkuu kwanza hongera, Watu wengi ni NPC au non player characters watu hawa ni rahisi kuchanganyikana na kuzoeana na watu na watu wa tabia hizo kazi yao ni kupenda kufatilia kujua kuhusu maisha ya watu wengine. Na lengo lao ni kuweka obstacles kwenye maisha ya watu.

Na ikitokea mtu akiwa tofauti na wao huona kama ni kitu cha ajabu na inafikia hatua unaonekana una dharau.

Ukiwa player character au PC unapenda kuwa mtu huru usiyependa kujihusisha na mazoea na kuchanganyikana na watu kwani unapenda faragha yako.

Ni asilimia chache ya watu wa hivyo kuwa wakimya na wapole na KARMA yao inakuwaga ni ndogo na mara nyingi ni positive. Google hiyo NPC utaelewa zaidi
 
Nilikuwa kama wewe mamaangu alikuwa anapiga kelele sana kutokana na hiyo hali kipindi nipo home baada ya kuanza maisha yangu hapo ndo nilijua muhimu wa kuwa interacted na watu now nimefaidika na vingi sana na kufanikiwa kwa mamboyangu mengi yote sababu yaku jichangangaya na watu .
Aisee jitahidi utoke kwa hiyo hali sababu unakosa vituvingi sana unakosa fursa nyingi mno .unakosa deals nyingi sana za hela mingi trust me ongea na watu uvae viatu huu msemo haukukosewa sababu sasahivi hapa chochote nnachohitaji najua nimpigie nani chap issue solved wala situmii nguvu kuwaza.
Badirika mzee askwambie mtu maisha niwatu na watu ndio walio kuzunguka utaona mamboyako hayaendi kumbe wewe mwenyew ndo umejipiga lock
 
Chief hata sisi tupo kama ww tena ni wakimya sana...ila unapaswa kubadili behavior na ukubaliane na hali ya kuinteract na watu ili upate mengi zaidi kwenye safari ya maisha yako...
Mm nilijarbu kujilazimisha sana mpaka nikaweza ..
 
Nilikuwa kama wewe mamaangu alikuwa anapiga kelele sana kutokana na hiyo hali kipindi nipo home baada ya kuanza maisha yangu hapo ndo nilijua muhimu wa kuwa interacted na watu now nimefaidika na vingi sana na kufanikiwa kwa mamboyangu mengi yote sababu yaku jichangangaya na watu .
Aisee jitahidi utoke kwa hiyo hali sababu unakosa vituvingi sana unakosa fursa nyingi mno .unakosa deals nyingi sana za hela mingi trust me ongea na watu uvae viatu huu msemo haukukosewa sababu sasahivi hapa chochote nnachohitaji najua nimpigie nani chap issue solved wala situmii nguvu kuwaza.
Badirika mzee askwambie mtu maisha niwatu na watu ndio walio kuzunguka utaona mamboyako hayaendi kumbe wewe mwenyew ndo umejipiga lock
Ukiwa mkimya na hujafanikiwa wala huna deals zozote zile za kukuingia pesa inakua haina maana yoyote
 
Anasema Charles Bukowski "ISOLATION IS THE GIFT"

ule uwezo wa kukaa pekee yako ni zawadi kubwa sanaa kwa sabab,

1.Hakuna mtu atasumbuliwa na wewe, kwa kuwa wewe una amani na wewe basi moja kwa moja huwezi kusumbua wengine

2.Husumbuliwi na mtu maana binadam wanachosha kukaa nao mda mwingi

3.Huitaji external source ili uwe na furaha, excited au motivated, yaani you only need you ili mambo yako yaende

4.Akili inatulia unajua u-focus na kipi, what is most important to you, you see clearly through this darkness we call life

5. Mada za kijinga jinga zinakupitia mbali


Lakini usisahau pia loneliness ina gharama zake na unahitaji kuugharimia na unalevya kama addiction zingine

Kuhusu ndugu jamaa na marafiki tenga muda ongea nao cheka nao maana mwisho wa siku those are all you have

Maana kama wewe ndo mtu wa muhimu zaidi kwenye maisha yako hauna sababu ya kuishi
 
Anasema Charles Bukowski "ISOLATION IS THE GIFT"

ule uwezo wa kukaa pekee yako ni zawadi kubwa sanaa kwa sabab,

1.Hakuna mtu atasumbuliwa na wewe, kwa kuwa wewe una amani na wewe basi moja kwa moja huwezi kusumbua wengine

2.Husumbuliwi na mtu maana binadam wanachosha kukaa nao mda mwingi

3.Huitaji external source ili uwe na furaha, excited au motivated, yaani you only need you ili mambo yako yaende

4.Akili inatulia unajua u-focus na kipi, what is most important to you, you see clearly through this darkness we call life

5. Mada za kijinga jinga zinakupitia mbali


Lakini usisahau pia loneliness ina gharama zake na unahitaji kuugharimia na unalevya kama addiction zingine

Kuhusu ndugu jamaa na marafiki tenga muda ongea nao cheka nao maana mwisho wa siku those are all you have

Maana kama wewe ndo mtu wa muhimu zaidi kwenye maisha yako hauna sababu ya kuishi
Ukiwa huna kitu cha kukuingizia hela ..ndio utaelewa somo
 
Mimi pia ni kama wewe labda tunaweza kutofautiana sababu tu. muda mwingi nakuaga peke yangu kwanza kutokua na ajira inaninyima hata nafasi ya kujiamini na kujichanganya na watu pili nina changamoto ya kusikia vizuri kwaiyo naweza hata kujichanganya na nisielewe nini kinaongelewa. Nafikiri mwenzangu hauna changamoto kama zangu. Kama unatumia kinywaji(sio lazima uwe mlevi ukiwa unapiga mbili tatu tu inatosha) na una uhakika wa maokoto kila wikiend jichanganye pub zilizochangamka uko utapata washkaji.
Pole kwa changamoto hizo mkuu. Maokoto kidogo ya kusogeza maisha yapo mkuu. Japo unywaji wangu ni wa kistaarabu. Ntajitahidi kujichanganya nikiwa hayo maeneo

Sent from my M10_Max using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom