Kupenda kunaniponza

Kupenda kunaniponza

Pole sana kwa hayo unayoyapitia kwa sasa.

Ili kukusahaurisha maumivu unayoyapitia kwa sasa inakubidi ukubariane na yaliyotokea na ujue kuwa adui wa furaha yako ni wewe mwenyewe na sio mtu mwingine yeyote yule.

Pili kama ukiweza kuiaminisha akili yako kuwa adui wa furaha yako ni wewe mwenyewe basi hapo utakuwa umepata ufumbuzi wa tatizo lako maana kama adui wa furaha yako ni we mwenyewe basi amua kuchagua furaha na achana na mawazo yanayoiba furaha yako

Tatu Iaminishe akili kuwa kuwaza ujinga na kujiumiza ni kijidekeza na unaweza ukawaza mambo mengine na yenye kukuretea furaha na kukusahaurisha yaliyopitaa.

Uchaguzi ni wako chagua furaha kwa kuyaacha yaliyopita au kuwa mtumwa wa mawazo kwa kuwaza yaliyopita yanayoumiza na kukuibia furaha yako.
 
Njoo na lako uje uone shuhuli yake.... mi nshaenda kutoa ushaur wangu wa pm nasubiri majibu hapa...
Ah ah ah uhii. Pm hapana y msitoe ushaur hapa hapa wengine tujifunze kutokana na makosa. Kwel kufa kufaana. Ipo siku watu watachat na baba zao humu. Mara ooh tuonane kitu unakuta mzee wako ah ah ah pm sio nzur aisee. Fake ID nazo zinasaidia
 
It's either ana tatizo lake binafsi la kuwa over-jealous kutokana na insecurities zake AU ww sio chaguo lake yani yupo na ww kujipunguzia nyege tu ila hakupendi Tutsi gl
 
USHAURI MZURI DADA,,,.........
mmezini mmefanya dhambi,..??
katubu dada,..hatukuumbwa duniani tuje kufanya dhambi,...Mungu anachukizwa na mwenye dhambi
japo watu wanashauri kana kwamba dhambi imekuwa kitu cha kawaida,....
mrudie MUNGU utubu,..huo ndo ushauri mzuri dada,..
utashauriwa apa na watu wata ku PM 4sure Wakutumie nawao,.
na utasahau kweli uliyotendewa na huyo kijana,
utapata mwanaume mwingine,atakuacha,.. hiyo chain na sanaa hiyo itaendelea utachezewa sanaaa2
na umri unaenda,..alaf mwisho wa siku unakuja kuolewa ushatumika sana,..mwishowe ndoa haidumu
maisha yako ya mapenzi yanakuwa ni kuhangaika2 all days,ila chanzo ulikiunda mwenyewe...
but unatakiwa ujue kusudi lako la kuwa hapa duniani,.....
wote vijana sis but kufanya dhambi ni dhambi,..
JITUNZE,MPENDEZE MUNGU,UMWAMINI YESU MUDA UKIFIKA UTAOLEWA NA UTADUMU NA NDOA YAKO,...
 
Ah ah ah uhii. Pm hapana y msitoe ushaur hapa hapa wengine tujifunze kutokana na makosa. Kwel kufa kufaana. Ipo siku watu watachat na baba zao humu. Mara ooh tuonane kitu unakuta mzee wako ah ah ah pm sio nzur aisee. Fake ID nazo zinasaidia

ha ha ha ha kuna ushaur mwengine uko ki binafsi zaid... embu chek pm yako sa hivi uone mfano wa huo ushaur.....
 
Siku Zote katika mahusiano yako ya kimapenzi jaribu kuupa moyo nafasi ya Kuvumilia hasa pale linapotokea suala kama hili.

Kuupa moyo nafasi Ya kuvumilia ni pale unapompa mtu asilimia chache katika moyo wako...

Wasichana wengi mmekuwa watumwa kwasababu mnajifanya mnajua kupenda... Mnajua kulia na kuvumilia kunyanyaswa.

Hakuna anayeingia kwenye mahusiano huku akitarajia kuumizwa..

Hakuna anayeingia kwenye mahusiano huku akitegemea kusalitiwa na kushushwa kwa thamani Yake...

Wote tunaingia kwenye mahusiano ili tuwe na furaha, tuheshimiwe, tupendwee na Kuthaminiwa.

Wakati mwingine utatamani ujiondoe kwake lakini hutaweza kwa kuwa tayari umemuweka ndani kabisa ya Moyo wako na kumtoa Hutaweza.

Ukiona Mwanaume Unayempenda Hajali wala kuyathamini mapenzu Yako, huyo sio wa kuishi wala kuwa naye tena.

Mapenzi ni Vile unavyoyapeleka lakini ukiona Hayakupi furaha Achana nayo fanya mambo Mengine
 
Pole sana mpendwa ila elewa tu kuwa kwenye mahusiano kuna milima na mabonde, vumilia endapo huyo ndiye Mungu kapanga uwe naye basi utakuwa naye tu.
 
Ah ah ah ah jaman watu mnajua kutumia opportunity loo
Opportunity never come twice, hebu na ww ni PM ili wakati wao wanazungumza ya kwao kule na sisi tuweka yetu sawa huku hahahahaha.......
 
Kazi ya moyo ni kusukuma damu uweze kuishi maisha marefu hii ya kupenda sijui mapenzi ni kiherehere chetu tu
 
Utazoea tu, maadam umeanza kabla ya kuolewa, utayaona matokeo yake mbeleni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom