Kupanda treni kwenda Moshi ni kujidhalilisha

Kupanda treni kwenda Moshi ni kujidhalilisha

Tunarudi nyuma miaka 25. Nimejiuliza yale Mabenzi, Vogue, Wachagga waliokuwa wanayatumia kwenda kwao December yameenda wapi?

Hadi kufikia usafiri wa kizamani namna hii?

View attachment 1284152
Unasema 'Kupanda treni kwenda Moshi ni kujidhalilisha. Hayo mabenz...mliyokuwa mkipanda yako wapi?' Haya ndiyo mawazo yanayotufanya tusiendelee. Yaani unaendesha benz ili tu watu wakuone. Wenzetu Ulaya wanasafiri kwa mabasi na treni kubana matumizi. Ukikuta watu kwenye kituo cha basi mjini London siyo kwamba hawana magari. Anaendesha gari mpaka kituo cha basi; anapaki hapo na kupanda basi kwenda kazini. Jioni anakuja anachukua gari lake na kurudi nyumbani. Wanaokwenda mbali zaidi wanapanda treni. Hela anazoziokoa anazitumia kwa shughuli zingine za maendeleo. Hiyo pia inaokoa mazingira kwa kupunguza moshi kwenye hewa; ajali zinapungua kwa kuwa magari ni machache zaidi; n.k. Sasa wewe na benz lako eti unataka wakuone watu. Hiyo haina tija. Ungeweza kufanya shughuli ya maana zaidi kwa hizo fedha unazookoa kwa faida yako binafssi na ya nchi nzima kwa ujumla. Kama utawekeza hizo fedha unazookoa kwa shughuli fulani ukaajiri mtu hiyo ni faida ya nchi. Tuondokane na mawazo yasiyo na tija.
 
Kuna kitu kimoja ambacho watu kama wewe hamuwezi kukielewa.

Ngoja nikupe scenario 2.

Umeitwa kwenye intavyuu moshi. Intavyuu inafanyika siku ya jumatatu. Sasa una option 2;

1. Upande basi Ubungo siku ya jumapili saa 12 asubuhi, (35,000) usafiri kutwa nzima ufike moshi saa 11 jioni. Ulale hotelini (30,000) uamke jumatatu uende kwenye intavyuu. Ulale moshi jumatatu, (30,000) uondoke jumanne asubuhi (35,000). Ushinde njiani ufike dar saa 2 usiku. Jumla = 130,000/- Muda masaa 60

2. Upande treni dar siku ya jumapili saa 10 jioni ukate ile ya ghali kabisa ya kulala (39,000) . Ufike moshi jumatatu saa moja asubuhi. Ujiandae uende kwenye intavyuu. Saa 10 jioni ukamate treni (39,000), saa mbili asubuhi jumanne uko dar unaendelea na shughuli zako. Jumla gharama = 78,000/- Muda masaa 36.
 
Usafiri wa treni ni mzuri kwa hiyo timing waliofanya. Muda wa kuondoka ni jioni hivyo mtu unapiga dili zako fresh kwa siku husika.. jioni unashika usafiri... asubuhi unaibukia mkoa au jijini. Mimi naona ni usafiri mzuri.
 
Kama yanafika asubuhi ni vizuri sana. Wale wote watakaokosa usafiri ubungo wataenda steshen kupanda tren watafika asubuhi kwa gharama nafuu
 
Ng'wanamalundi, Hiyo ni london kwa mabeberu wao treni ni usafiri nafuu,hizo treni za jiwe amechukua yale mavichwa mabovu ndio katengeneza,unategemea huo usafiri kua wa hakika?utasikia mara limeharibikia porini na hiyo route linapita mbali na miji ni mombo tu ndio linapita mjini
 
Sio wote walikuwa wanapanda magari binafsi. Sasa ndio hao watapanda tren
Mleta uzi unapotoka, sio wote wanaoishi Kilimanjaro ni wachaga.
Watu wa Hedaru, Same, Mwanga hadi Moshi wengi ni wapare na makabila mengine.
Kuna wengi hawana uwezo.
Ndani ya wachaga wapo weengi sana ni choka mbaya kuliko hata Wagogo.
Kwanza ratiba za treni zimekaa vizuri hadi nami natamani kuipanda, inatembea usiku so hupotezi muda mwingi wa kazi.
Ukichukua daraja la kwanza unalala wee asubuhi ukiwasili unaingia kazini kama kawaida.
Wachaga pandeni treni muongeze muda wa kusaka mbesaa
Tunarudi nyuma miaka 25. Nimejiuliza yale Mabenzi, Vogue, Wachagga waliokuwa wanayatumia kwenda kwao December yameenda wapi?

Hadi kufikia usafiri wa kizamani namna hii?

View attachment 1284152
 
Ipo moja au? I mean kwa week inaenda iyoiyo au zinapishana
Kwa ratiba hii inaonyesha ni moja
IMG-20191205-WA0005.jpeg
 
Back
Top Bottom