Kuoa kwa harusi au bila harusi kipi bora?

Kuoa kwa harusi au bila harusi kipi bora?

Siku hizi mtu akitaka kuoa kuna kuwa na event nyingi mara utasikia kutangaza uchumba, pete ya uchumba, kitchen part [wakati muolewaji ameishawah ishi na mwanaume mwingine kwenye sogea tuish miaka saba] mara ndo send off then harusi!!!! baada ya harusi jamaa anabaki hana kitu hadi vyombo vya ndani vya kuunga unga! mi naona Bora kuoana bila harusi ili fedha ya sherehe nifanyie mambo mengine!!!
Harusi sio lazima kivilee...ila ni vizuri ukafanya hii sherehe kulingana na kipato chako.

Halafu kwa mimi navyo fahamu sherehe ya harusi hugharamii wewe...watakaogharamia ni ndugu, majirani na marafiki.

NB. Kama ulitoa michango kwenywe sherehe za wengine.

Muhimu ni kufanya sherehe kulingana na uwezo wako wa kiuchumi. Wengine ni mwendo wa walu mweupe, maharage na soda tu.

ASANTE
 
Haiwezekani kwenye mazungumzo kusitokee mabadiliko.Ilianza gharama za ndoa na sherehe yake sasa tunaipanua hoja kwa nakshi za hoja zingine.Hii ni tabia ya fasihi hasa ya uandishi na kuongea.
huyu hana jipya ameona kila anachotaka changia kimezungumziwa! inshort ni haijui fasihi!
 
Sina shaka na hilo kaka,
Kichwa cha mada kinaonekana anatafuta majibu kutoka kwa wanajamvi, lakini pia wakati huo huo yeye katoa jibu la swali hilo hilo.
Ndio maana nasema kuna haja kichwa kubadilika ili kuchukua maana kamili ya mada..mfano: Harusi ipi ni bora kwako!?
Kwa kichwa hiki yeye anaweza toa jibu la swali lakini pia nafasi kwa wengine ikiendelea kuwepo kutoa majibu yao.
Tuko pamoja mkuu.
ahsante mkuu! je kuna mapungufu yapi kwa kichwa hiki?
 
Bila sherehe Maisha hayana maana Mkuu. Fanya sherehe kulingana na uwezo wako. Ila sherehe ni muhimu. Ukifanya jambo jema unapaswa kusherekea kama kuhitimu shule, kupata mtoto, kupona ugonjwa n.k. Kusherekea ni moja ya nguzo ya maisha.

Bila sherehe maisha hayana maana.
 
ahsante mkuu! je kuna mapungufu yapi kwa kichwa hiki?
Nimegusia kidogo juu ya kichwa kiweje, lkn anaweza akakitengeneza vizuri zaidi bila kuathiri mukhtadha mzima, Nina imani hawezi shindwa kukiunda vyema.
Asante.
 
Na mlivyo wasanii mnapenda kuitwa majina lainilaini na matamumatamu.Mimi mama Wegesa simuiti jina lainilaini.Namuita "my gunia la.mkaa" au siku nikifurahi zaidi namuita "my kabati"![emoji122][emoji122][emoji122][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Veeery sweet names!
Mfyuuuu uniite your kabati mm,.woiiii narudi kwetu[emoji23]
 
Back
Top Bottom