Nimewahi kuwa meneja wa kumbi za harusi kubwa tu hapa mjini.
Sherehe zote zinazo karibisha ndoa, harusi, send off , kitchen party na nyinginezo asilimia kubwa 85% ni michango ya watu. Matatizo hutokea kwenye michango, na mara nyingi ma bifu na viburi huibuka. Mtu asipo changa ndio mwanzo wa kutosalimiana na mahusiano huweza isha.
Wengi wa bwana harusi na bibi harusi asilimia kubwa unakuta mmoja wao ndie mwenye kipato cha wastani au mwajiriwa.
Tatizo linatokea pale ambapo Bwana harusi na bi harusi huingiza ela nyingi kutoka mifukonu mwao ili kufanikisha shughuli hizo kwa kukopa bank, jamaa nk
Kiufupi ni kwamba asilimia kubwa ya ninao wafaham na niliokutana nao wanaishi maisha ya tabu sana na huwezi amini ni huyu ndie alifunga harusi ya 40M. Wengi wao baada ya mazungumzo hujuta sanaa. Tukio la siku moja linakugharimu miaka 2-3 kwa kuishu kwa tabu sanaa.
Niliapa kabisa kamwe sita kuja fanya michezo hii ya kuigiza kama sina kipato kikubwa cha kuchezeaa. Mimi kama nitafunga harusi sinta mchangisha mtu yoyote hata sumni.
Pili harusi yangu haita zidi watu 50.
Asilimia kubwa ya wanao alikwa kwenye harusi ni wachangiaji, na wengi hutaka kuona ela yao waliochanga wanaifaidi vipi. Ikitokea tofauti kile anachokiona mezani hakiendani na ela aliyotoa majungu ndo huzalishwa hapa.
Harusi nyingi zina majungu, mara bi harusi hajapendeza, mara bi harusi sijui kabila gani, mara bi harusi kanunaa, mara harusi imepoaa, yanii ukumbini ni kuchoranaa tupuuuu.
Kwa ushauri wangu, vijana tusipende fame ya muda mfupi. Tusipende kufurahisha watu kwa muda mfupi alafu muda mrefu unagharamika wewe. Tusipende kuigaiga.
Kama huna uwezo wa hizi mambo, achana nazo, zinagharama sana, kuanzia kifedha hadi kisaikolojiaa.