Mndengereko
JF-Expert Member
- Mar 24, 2011
- 7,319
- 3,432
Heshima kwenu wanajamavi,poleni na mihangaiiko ya kujenga nchi sisi wengine tuko busy na kuibomoa. Moja kwa moja niende kwenye topic kuna trend inayoendelea hivi sasa kwa wanandoa unamkuta mwanamke mzuri anavutia ana kila kitu ambacho mwanamke mzuri inabidi awe nacho. Akishaolewa sasa ndo shughuli inaanza utukunyema unamkuta mtu ananepeana mpaka kero na ule uzuri wote uliomfurahisha muoaji/mumewe umepotea.
Haeleweki tumbo liko wapi na nyama za ubavuni ziko wapi ukimuuliza oooh nimeridhika maisha mazuri, mume wangu ananipa kila ninachohitaji na nakula vizuri. Sasa kama wewe unakula vizuri na Rihanna asemaje? au unataka kutuaminisha kwamba wewe unakula vizuri kuliko Angelina Jolie ila mbona wao bado wana miili yao ile ile.
Kula vizuri sio tatizo tatizo ni kupangilia kula kwako ili kumaintaina uzuri wako/shape yako. Sio ishu wala nini umeolewa ulikuwa mzuri unavutia mtoto wa haja mume wako alikuwa hakuchoki ana hamu muda wote atembee na wewe basi maintain hiyo hali (uzuri wako) ili usimpe vishawshi visivyo vya lazima mumeo na aendelee kukutamani all the time. Haijalishi mme wako ni mpole,mstaarabu au anakujali kiasi gani human being is selfish by nature kila mtu anapenda vitu vizuri so ni wajibu wako (sole responsibility) kumaintain uzuri wako ukijiweka hovyo mumeo anawezaa kutafuta vizuri.
Back to us boys/men na sisi kuna baadhi yetu wanajibweteka sana wakishaoa. Kabla ya ndoa tunajijali kula vizuri kwa wastani na vimazoezi viwili vitatu vya kudanganyia ilimradi kuweka mwili katika mpangilio. Shughuli inaanza mtu akishaoa anajisahau na kunenepeana hovyo mpaka unakuta mwanaume ana kitambi kikubwa kama mimba ya miezi minne kha!! Sio ishu wala nini ukimuuliza ana kwambia mama fulani fundi bwana anajua kukarangiza sijapata kuona.
binafsi hiyo haiwi sababu ya kutosheleza kuhalalisha unenepeanaji wako wa ghafla kama kuku wa broiler. Cha msingi ni kujipenda na kumaintain maumbo yetu.
Kwa kumalizia nisiwachoshe ni kwamba najua wengi wetu tukioa au wanawake kuolewa basi time hubana sana kutokana na ubusy wa majukumu ya kifamilia. Lakini ukweli jukumu la kumaintaini mwili wako na kukufanya uwe unaonekana kama wa mtu(romantic) ni letu wenyewe haijalishi upo busy kiasi gani. Na hili swala linatuhusu wote wala haijalishi kama ni mseja au umeoa/kuolewa.
Naomba kuwasilisha.
cc : ICHANA mwekundu Mr Rocky Tized Mashaxizo mshana jr Eshy m.s
Haeleweki tumbo liko wapi na nyama za ubavuni ziko wapi ukimuuliza oooh nimeridhika maisha mazuri, mume wangu ananipa kila ninachohitaji na nakula vizuri. Sasa kama wewe unakula vizuri na Rihanna asemaje? au unataka kutuaminisha kwamba wewe unakula vizuri kuliko Angelina Jolie ila mbona wao bado wana miili yao ile ile.
Kula vizuri sio tatizo tatizo ni kupangilia kula kwako ili kumaintaina uzuri wako/shape yako. Sio ishu wala nini umeolewa ulikuwa mzuri unavutia mtoto wa haja mume wako alikuwa hakuchoki ana hamu muda wote atembee na wewe basi maintain hiyo hali (uzuri wako) ili usimpe vishawshi visivyo vya lazima mumeo na aendelee kukutamani all the time. Haijalishi mme wako ni mpole,mstaarabu au anakujali kiasi gani human being is selfish by nature kila mtu anapenda vitu vizuri so ni wajibu wako (sole responsibility) kumaintain uzuri wako ukijiweka hovyo mumeo anawezaa kutafuta vizuri.
Back to us boys/men na sisi kuna baadhi yetu wanajibweteka sana wakishaoa. Kabla ya ndoa tunajijali kula vizuri kwa wastani na vimazoezi viwili vitatu vya kudanganyia ilimradi kuweka mwili katika mpangilio. Shughuli inaanza mtu akishaoa anajisahau na kunenepeana hovyo mpaka unakuta mwanaume ana kitambi kikubwa kama mimba ya miezi minne kha!! Sio ishu wala nini ukimuuliza ana kwambia mama fulani fundi bwana anajua kukarangiza sijapata kuona.
binafsi hiyo haiwi sababu ya kutosheleza kuhalalisha unenepeanaji wako wa ghafla kama kuku wa broiler. Cha msingi ni kujipenda na kumaintain maumbo yetu.
Kwa kumalizia nisiwachoshe ni kwamba najua wengi wetu tukioa au wanawake kuolewa basi time hubana sana kutokana na ubusy wa majukumu ya kifamilia. Lakini ukweli jukumu la kumaintaini mwili wako na kukufanya uwe unaonekana kama wa mtu(romantic) ni letu wenyewe haijalishi upo busy kiasi gani. Na hili swala linatuhusu wote wala haijalishi kama ni mseja au umeoa/kuolewa.
Naomba kuwasilisha.
cc : ICHANA mwekundu Mr Rocky Tized Mashaxizo mshana jr Eshy m.s