thnx kwa kutetea sie tuliozaa na tukaolewa mi natoa mfano wangu mwenyewe firs born wangu na babake hatuko pamoja kila mtu kivyake na namheshimu sana mme wangu mana kwa ujasiri wake ameweza kunikubali na akanioa na tuna amani tu suala si kurudiana na mwenzi wako unaeza oa asiye na mtoto akakubambikia pia by the way mbona wanaume mnazaa na mnaoa wasio na watoto acheni ubinfsi au hapa jf hv hamna watu waliozaliwa half siblings humu?au ndo mbwembwe tu!
Umeleta point muhimu kwa
angle nyingine. Assume mleta mada ndio angekuwa baba wa mtoto sehemu
nyingine, na anataka kuoa binti asiye na mtoto. Hii ingekaaje?
Nachomshauri mleta mada, kama kampenda binti amuoe tu, bila kujali kama
kazaa. Cha msingi ni upendo, mengine mbwembwe tu.
Ukioa mwanamke mwenye mtoto wa mwanaume mwingine, unakuwa mume mdogo. Kwa sababu huyo mwanamke tayari ana mume mkubwa.
So mnakuwa wanaume wawili mmeoa mwanamke mmoja.
Ni mtazamo tu.
Narudia na ntaendelea kurudia tena....... MAHAWARA HAWAACHANI!!. Usithubutu kutaka kumjua hawara wa mke/mme wako. UTAKUFA KWA PRESHA!!!Asprin atakuambia mahawala hawaachani, swala la kurudiana au kukumbushia mtoto sio sababu. Tena kama alimkataa akiwa mjamzito, inajenga chuki zaidi ya upendo. Hofu yako ndio hasara yako, toa mawazo negative na mtaishi happily after.
Halafu naona huyu hajampenda vya kutosha ndio maana anauliza mawazo ya watu. Live your life, ili usitafute wa kumlaumu pala yanapokushinda.
aisee....Usiniwekee maneno ambayo sikuyaandika. Hakuna popote niliposema kwamba msimamo wangu ndio msimamo wa jamii. Hao wanaofikia maamuzi ya kuoa wanawake wenye watoto hukaa na wazazi wao, ndugu zao na jamaa na marafiki na kuangalia uwezekano wa kufunga pingu za maisha. Na wao wakiafiki kwamba mtoto wao, ndugu yao, jamaa na rafiki yao aendelee na maandalizi ya harusi basi hutoa baraka zao. Acha mawazo finyu kwamba mwanamke akiwa na mtoto basi huyo hastahili tena kuwa mke. Muhusika kaja hapa kuomba ushauri badala ya wewe kutoa ushauri wako na kumuachia mwenyewe afanye maamuzi yake, unaanza kuhoji ushauri wangu. Acha hizooo.
Ukioa mwanamke mwenye mtoto wa mwanaume mwingine, unakuwa mume mdogo. Kwa sababu huyo mwanamke tayari ana mume mkubwa.
So mnakuwa wanaume wawili mmeoa mwanamke mmoja.
Ni mtazamo tu.
aisee....
Nawashangaa sana.Mwanamke mwenye akili timamu awezi kutembea na mtu alomzalisha na kumuacha maana hicho kitendo ni cha kinyanyasaji hasa kwa mwanaume mwenye uwezo wa kulea mtoto.
Pia jiulize kama issue ni mimba wangapi wanaolewa na walishatoa za kutosha?
Mwisho kabisa jiulize kwa maisha ya sasa mabinti wana hamia kwa wanaume ata miaka miwili bila ndoa na baadae wanazinguana anakuja kuolewa na kijana mwingine na habari zinakua chin ya kapet japokua binti anakua hana mtoto na x.sasa we ukimpata huyo je utasemaje?
Kwan wewe unamuoa mtoto au mama ake sion chakuumiza kichwa piga mimba tangaza nia fasta bora ulijualo halikusumbui.unaeza kuoa asiye na mtoto akawa hazai pia ama akakubambikiza watoto
kama utachunguza kwa umakini sana hapo tatizo lipo tena kubwa:
1.kwa nn aseme hv "nilivo muuliza kwa nn alinificha akadai angenikimbiza mapema kama angeniambia"
2.kwa nn ang'ang'anie hili "KWA SASA BINTI ANATAKA NIMUOE KWANI NIMESHAPATA KAZI"
mkuu bora ukosee kujenga nyumba ila sio kuoa!!!!!!!!!!:behindsofa:
Kwa kuwa ni mtazamo, acha uwe mtazamo. Siku hizi hata kama hamna mtoto na huyo mke, mnaweza kuwa wanaume hata watatu mmeoa mke mmoja bila kujuana, ila ni mmoja tu anaekuwa anajulikana rasmi. Hali ni mbaya kuliko tunavyofikiri.Ukioa mwanamke mwenye mtoto wa mwanaume mwingine, unakuwa mume mdogo. Kwa sababu huyo mwanamke tayari ana mume mkubwa.
So mnakuwa wanaume wawili mmeoa mwanamke mmoja.
Ni mtazamo tu.
Mtoto akiwa wa kike raha ila wa kiume lazima amtandike maana inafikia, bilogically, kuna wivu fulani kwa mama yake. Hapo ndipo kutandikwa hakuepukiki. Hata wewe kama baba ana mke mwingine ni hatari kwake ingawa sisi wanaume utasacrifice mtoto ili k yako iwe salama. Mama hawezi hata siku moja akasacrifice mtoto ati anatetea dushe.itategemea alivyomlie mie nimelelewa na baba mlezi (sipendi kumwita wa kambo maana namuheshimu sana) nampenda na mjali sana
Je hakuna usumbufu wowote unaoupata kutoka kwa baba mtoto wa mke wako?