Binafsi huwa naamini
1. mwanamke aliyepelekwa leba na mwanamme kamwe hamsahau huyo mwanaume no matter wat happens esp mimba ya kwanza
2. Mtoto ni kiunganishi baina ya wazazi. Always watakuwa na mawasiliano no matter wat happens.
3. Huwa naamini kujifungua its a live or die thing. its either mwanamke afe mtoto abaki au mtoto afe mwanamke abaki au wafe wote au wabaki wote. So mwanamke kuamua kumzalia mwanaume mtoto huwa ni upendo wa ajabu kiasi cha kuamua kurisk maisha yake kwa yule mwanaume.
Ni hayo tu. Akili za kuambiwa changanya na zako
Umeleta point muhimu kwa angle nyingine. Assume mleta mada ndio angekuwa baba wa mtoto sehemu nyingine, na anataka kuoa binti asiye na mtoto. Hii ingekaaje?Hivi mwanaume nae akiwa ameshawahi zalisha huko nje na anataka kuoa cjui inakuwaje.
labda wanawake walioolewa lakn kwa waliopata mimba wapo shule si ajabu hata hisia za mapenzi zikakata kabisa kwa jamaa. wengi uishia kulea mtoto tu.
nafkiria tu unawezaje kumpenda mwanaume ambae alichangia kwa namna moja au nyingne kuharibu future yako??!!!
kwa hiyo maneno yangu ni ya kukaririshwa sio?? Binafsi siwezi, nawaachia wengine waoe.
Hapo ndo nashangaaga wanaume hadi nabaki mdomo wazi
we ukiwa hata na watoto kumi tena kila mtoto na mama ake
unaoa tu na unaona ni haki yako ila ukikuta binti ana mtoto unaanza kugoogle kwenye vichwa vya watu
nini cha kufanya......aaaggrrr
Hapo kwenye bold ni kweli wamesacrifice mno manake once dada akisema nahisi nimekwama na hasa kipindi cha usichana wengi hukimbiwa na hata kukataliwa sasa hapo mama anakua ana maamuzi 2 either aitoe au alee kwa taabu na dhihaka nyingi toka kwa jamii na familia. Ktk hili nampenda sana mama mkwe wangu kwani alisacrifice mengi ili kumuokoa mwanae maana angeweza kucholopoa. Kuhusiana na michepuko nafikiri hii ni tabia ya mtu kwani hata walioolewa fresh kuna wanaokumbushia mahusiano yao ya zamani.waambie hao........ wanawake wenye watoto waheshimiwe na watu wote... wamesacrifse mengi sana.....
Dada kulea bao la mtu mwingine inahitaji ujasiri sana haswa unakuta mtt kishamjua baba yake
na kwa nini uoe/uolewe na usiyempenda?
Baba wa huyu mtoto yupo znz ila hana mpango na mtoto tangu azaliwe mpaka sasa sio kwa kuumwa wala sabuni Hivi karibuni mm ndio ninaepigiwa simu na mamake kama mtoto anaumwa na mm ninamtumia pesa anampeleka hospitaliMimi naona tatizo sio kuzaa (kuwa na mtoto), tatizo ni mtoto. Sio rahisi kumuoa mama na mwana.
Sasa basi muulize endapo baba wa mtoto anafahamika, anamtambua mtoto na kama anashiriki katika malezi ya mtoto.
Kama anazo sifa hizo hapo juu basi mtoto aende kwa Baba yake.
Kama hana hizo sifa hapo juu, basi mtoto abaki kwa bibi yake au kwa wajomba zake.
Mtanipinga sana ila huo ndio ukweli mtupu kiafrica africa. Mimi binafsi nimeshaletewa watoto wawili kutoka kwa wanawake tofauti ambao kwa sasa wameolewa na ndoa zao zina amani tele kwa muonekano wa nje, nami nalea watoto wangu kwa amani nikisaidiana na bibi yao, I love them, soon nitawaletea mama yao (step mother)
Nashukuru mkuu pamojadaah mkuu historia yako kimasomo inafanana sana na ya kwangu, anyway kaka kama ana sifa za kua mke wewe muoe tu, huyo mtoto hawezi kuwa kikwazo. go for your heart
Je hakuna usumbufu wowote unaoupata kutoka kwa baba mtoto wa mke wako?hata mie nimeoa mke ambaye nilikuta tayali ameshazaa na maisha yanaenda poa tu so go for her
Kwasababu ulishamuahidi haimaanishi kuwa lazima umuoe, ni vizuri mtu kutimiza ahadi ila kama ulivyosema unagwaya itasaidia nini wewe umuoe halafu msiwe na raha ndani ya ndoa, unasema unampenda sana kitu cha kujiuliza je kipi kina uzito upendo au mtoto aliye naye kama unahisi huyo mtoto ni ngumu kwako, bora usimpotezee muda maana atapata wanaoweza mudu hilo, kila mtu na uwezo wake, hata tukishauri vipi wewe unajua nini kimekujaza moyoni. Wewe ndio utakayeishi na huyo mdada, ninaweza kukusema nimeona walioa wenye mtoto na wanafurahia ndoa zao, wanachukulia mtoto kama wao na nimeona walioshindwa wakaacha mauhusiano ilipofikia swala la ndoa. Nitatoa mfano wa walioa naye ni bosi wangu (ni kijana chini ya miaka 30) yeye alimwambia mdada aache mtoto kwa bibi yake mpaka wao watapokuwa na mtoto wao, sasa wana mtoto mmoja na wamemleta yule mtoto toka kwa bibi. Nilimwelewa kuwa alikuwa anataka afurahie mwanzo wa ndoa wao wawili tu. Nakutakia mafanikio mema, fanya maamuzi na uwe muwazi kwa mdada....nilishamuahidi kumuoa nikipata kazi na sasa nimeajiriwa na wizara ya mifugo...Kwa sasa binti anataka nimuoe kwani nimeshapata kazi lakini nagwaya kuwa ni sawa kwa umri wangu kuanza na binti mwenye mtoto? Zingatia binti nampenda sana kwani alivyo huwezi amini kuwa ana mtoto na yeye pia ananipenda.
Baba wa huyu mtoto yupo znz ila hana mpango na mtoto tangu azaliwe mpaka sasa sio kwa kuumwa wala sabuni Hivi karibuni mm ndio ninaepigiwa simu na mamake kama mtoto anaumwa na mm ninamtumia pesa anampeleka hospitali
Ila akumbuke mtoto akikua lazima amdunde baba wa kufikia. Akiwa mdogo hakuna shida, shida zinaanza anapoanza kujitegemea hasa akiwa wa kiume