Ndallo
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 7,619
- 4,292
Wakuu niko hapa kwenye jiji letu la Arusha maeneo ya stand kubwa ya mabasi naendesha gari kuelekea kupata chakula cha mchana, lakini kinachonichanganya mpaka kufikia hatua hii ya kuleta huu Uzi hapa ni kuhusiana na mvua inayoanza kunyesha hapa, wakati naendesha gari watu wanakatiza mbele ya magari tena hawayaogopi napiga honi lakini watu wanatembea polepole midhili yakutokuogopa kugongwa na magari! lakini muda si mrefu mvua ilipoanza kunyesha naona watu walewale wanakimbia midhili ya kama wanafukuzwa, sasa najiuliza hivi binadamu wanaogopa mvua halafu kwanini hawagopi kugongwa na magari? Nawasilisha.