Kununua gari au kujenga nyumba

Kununua gari au kujenga nyumba

Mkuu chiwa mfuko 1 cement tofali 35?unataka kumtafutia mwenzio majanga.
teh...tehee... tofari nyingi tunazonunua ukiuliza vizuri mafundi wanakwambia wamepiga 45 kwa mfuko nyingine mpaka 60 wanachofanya ni kuchangaya vizuri udogo na maji mengi kwenye tofali ili likomae hata hivyo nyumba zetu nyingi tunajenga kwa kuishi vizuri miaka 30 hivyo linatosha kwa kuwa baada ya hapo tumechoka na watoto hawapendi plan za nyumba zetu kama wewe usivyopenda plan ya nyumba ya baba yako hata kama nzuri namna gani haiwezi kukupendeza ukilinganisha na nyumba yako ya miti.
hivyo inatosha wangu
 
Mmhh kaka me nnamiliki gari lakinI sI kwa mahesabu yako..service kila mwezi 100000???.kwahiyo mil9 kwa mwaka maana yake gari inakost kwa mwezi 750000 realy.?? Labda unamiliki gari ipi mwenzetu....me yangu walaaaa
100,000 kwa mwezi huwezi kuiona moja kwa moja kwa kuwa si kila mwezi matengenezo yanaweza kuwa makubwa lakin amini huo unaweza kuwa wastani kwa mwezi ikiwemo gharama za mataili break, boljoint ,grese na mengine mengi inategemeana na aina ya gari.
kuna gari siku hizi ukienda service fundi anakuja na laptop kuicheki tu 50,000 bado matengenezo hivyo inawezezekana weka vizuri hesabu zako utaiona
nimesema kwa sasa sina gari lakin naziona hizo gharama vizuri sana
 
Hakuna baba mwenye gari; kuna baba mwenye nyumba.
 
KUMILIKI NYUMBA NI RAHISI SANA KULIKO KUNUNUA GARI!

-Huwezi kuwa na laki moja ukaenda kununua tairi la nyuma leo na mwezi ujao ukapata laki mbili ukanunua dash board!
ila nyumba ukiwa na laki moja leo unanunua tofali kadhaa!,laki nne mwezi ujao unaongeza tofali na mifuko mitno ya cement
kitu kinaaanza kunyan yuka
 
usinunue gari wewe utaomba rushwa bure. Kwa jinsi boda boda zilivyo nyingi huna haja ya gari, panda bdbd tu jenga nyumba ya milioni zako80 utulie
 
100,000 kwa mwezi huwezi kuiona moja kwa moja kwa kuwa si kila mwezi matengenezo yanaweza kuwa makubwa lakin amini huo unaweza kuwa wastani kwa mwezi ikiwemo gharama za mataili break, boljoint ,grese na mengine mengi inategemeana na aina ya gari.
kuna gari siku hizi ukienda service fundi anakuja na laptop kuicheki tu 50,000 bado matengenezo hivyo inawezezekana weka vizuri hesabu zako utaiona
nimesema kwa sasa sina gari lakin naziona hizo gharama vizuri sana

mi nlinunua gari 2008 sikupata hizo shida hata kidogo for 2yrs, hivi wenzangu mwanunua make gani mbona mnacomplain complain? au ni 3rd hand cars!!
 
ni umasikini tu, kwa maisha ya sasa gari sio luxury item ni lazima kuwa nayo, yani mtu toka primary-sec-chuo-job unasota kwa mguu tu khaaa

linachosha acha tu........mie sina pesa tu ila ningekuwa nazo kitu cha kwanza ingekuwa gari hayo ya nyumba

yangefatia baadae saaaaaaaaana
 
Habari wadau, Nina rafiki yangu wa siku nyingi alinifuata hivi karibuni kuniomba ushauri, yeye ameoa na wamebahatika kupata watoto wawili, kwa sasa anaishi nyumba ya kupanga. Ameniambia yeye na mkewe wapo katika malumbano ya kuhusu kipi waanze kukifanya kati ya kununua gari ama kununua kiwanja na kuanza ujenzi!! Kipato chao kwa mwez jumla huwa kati ya sh lak 8 hadi mil 1 na lak 2. sijui ndugu zangu mngewashauri waanze na ujenzi au gari?

Wanunue gari halafu waiuze wanunue nyumba.
 
linachosha acha tu........mie sina pesa tu ila ningekuwa nazo kitu cha kwanza ingekuwa gari hayo ya nyumba

yangefatia baadae saaaaaaaaana

Tufanye mpango wa kuichukua ile corona kabla ya mwezi wa sita. Tutakuwa mafundi taratibu
 
atafute kiwanja kwanza,then anaweza kununua gari wakati anajikusanya ili aweze kujenga.
 
Jamani kuwa na usafiri sio anasa, ukiwa na Gari itakusaidia sana kwenye supervision ya ujenzi Wako. Ukiiba kapesa kidogo kazini unapitia duka la ujenzi faster unaweka kwenye Gari yako huyooooo moja kwa moja kwenye site yako. ILA sielewi Kwanini watu wana misconceptions Hii ya kuwa na Gari. Huu ni mtazamo binafsi

duuu kumbe wachanisimame kujenga kwanza.
 
Mmmh kweli mi hapa napata shule toka pande zote maana kiwanja sinaaa na gari siiiinaaa. Sasa somo linanitisha kweli hilo. Ngoja nikusanye nondo za wadau japo naweza toa ushauri wangu baadaye.

Mkuu uliyeleta hii hoja udumu maana imenifumbua.
 
nunua gari unapotoka asubuhi nyumbani kwenda kibaruani kula vichwa(pakia abiria hata kama ni wawili) na wakati wa kurudi fanya hivyo. Kama upo maeneo mazuri mfano mbezi au kibamba utapaka fedha kiasi kwamba gari litajiendesha lenyewe tena kama si mtu wa starehe unaweza kuweka akiba then mambo ya kujenga kwako ya takuwa rahisi.
 
Back
Top Bottom