hakuna maisha rahisi kama kuwa na gari. Binafsi nilianza na gari. Kuna siku nilikuwa na mizunguko mjini ofisi kama tatu, nilichukua teksi nikaenda pa kwanza, nikarudi,nikaenda pa pili nikarudi, pa tatu, wakaniambia rudi saa8, nikakimbia ofisi kwetu, saa 8 nikaita teksi iyo na kwenda...mizunguko yote haikuzidi kilometre25, jamaa akaniltea bill ya shilingi elfu 39,000 na waiting charge 5,000/= , sikukaa mwezi nikaagiza gari.
Ushauri tu kwa vijana wenzangu wanaoona future kuwa itakuwa nzuri basi jaribu ivi,
Nunua gari dogo lenye consumption ya fuel kuanzia km 10 per litre,mpaka 12, u shall never regret, service km 3000 sh 50,000 wakati kwa teksi hapo unadaiwa kama laki8 ivi,
Ujenzi utakuja wala usiwe na haraka.
Taadhari: Kama kipato chako ni kidogo,chini ya lak350,000/= tafadhari tumia daladala wala sio teksi wala kunua gari, sio dharau au kejeli bali ndo ukweli, fikiria hesabu ya haraka 350,000*12= 4.2 mil per year, hapa service tuweke hata laki200,000/= spea tuseme tu sh laki300 per anum na fuel laki6 p.a parking kwa mjini 360,000 na ule , ulishe familia. Kwa gari tayari ishakula minimum 1.5 mil, kodi tuseme una familia rum 2 tu sh 100,000/= thus 1.2 mil hapo utalia na kutupa gari.
Ila kama kipato ni kuanzia lak5, wakuu achana na taksi na daladala, tumia usafiri rahisi, private drive,
faida zake:
-Utaenda kokote kwa muda wowote unaotaka
-utasevu ela badala ya kutuima taksi km2 sh elf7 utatumia sh 500 kwa mafuta ya gari/ robo litre.
-Badala ya kukimbilia daladala na kuchafuka na kusababisha kufua kila siku, waweza kufika unakoenda unanukia,kiatu baniani mbaya, pasi bado nguo imesimama, nk nk
-Utasimama unapotaka na kuondoka unapoamua, eg unatoka posta kwenda pugu, unapitia kinondoni unasolve ishu, unaenda magomeni unamuona anayekusubiri, unapitia ubungu unabeba mifuko yako ya simenti3,.... nakuambia kwa daladla posta kinondoni 400 na umechafuka vilivyo, kino mpaka magomeni 400 na matusi ya konda, magomeni ubungo 400 umelipa elfu5 na konda anabisha eti change kashakupa,ubungo kwenda pugu na mifuko ya sementi 3 utalia na kusaga meno na route hii inakugarimu masaa 5 wakati private ni lisaa limoja tu.
utani//Kama haujaoa kama Gsana, aah aah ah nakuambia utang'oa chuma cha ghorofa, kama mtarajiwa hautawaza kumfuata moro au masaki au mkuranga, miguu minne haichezewi.
All in all, gari ni lubricant na access device ya other all activities you plan.
OMBI: ACHANA NA TAKSI VIJANA WENZANGU,TUTUMIE HII NJIA MBADALA.
Binafsi sina pesa ya kupandia taksi ndo maana nikanunua mwananjenje!bata mweupeeee!